< Numbers 13 >

1 Then spake Yahweh unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
2 Send for thee men and let them spy out the land of Canaan, which I am giving unto the sons of Israel, —one man each for the tribe of his fathers, shalt thou send, each one a prince among them.
“Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ambayo ninawapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mmoja wa viongozi wao.”
3 So then Moses sent them out of the desert of Paran, at the bidding of Yahweh, —all of them, great men, heads of the sons of Israel, were they.
Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.
4 And, these, are their names, —Of the tribe of Reuben, Shammua, son of Zaccur;
Haya ndiyo majina yao: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
5 Of the tribe of Simeon, Shaphat, son of Hori;
kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
6 Of the tribe of Judah, Caleb, son of Jephunneh;
kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
7 Of the tribe of Issachar, Igal, son of Joseph;
kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;
8 Of the tribe of Ephraim, Hoshea, son of Nun;
kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9 Of the tribe of Benjamin, Palti, son of Raphu;
kutoka kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu;
10 Of the tribe of Zebulun, Gaddiel, son of Sodi;
kutoka kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi,
11 Of the tribe of Joseph—of the tribe of Manasseh, Gaddi son of Susi;
kutoka kabila la Manase (kabila la Yosefu), Gadi mwana wa Susi;
12 Of the tribe of Dan, Ammiel, son of Gemalli;
kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali;
13 Of the tribe of Asher, Sethur, son of Michael;
kutoka kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli;
14 Of the tribe of Naphtali, Nahbi, son of Vophsi;
kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Wofsi;
15 Of the tribe of Gad, Geuel, son of Machi.
kutoka kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki.
16 These, are the names of the men, whom Moses sent to spy out the land, —but Moses called Hoshea son of Nun, Joshua.
Haya ndiyo majina ya watu ambao Mose aliwatuma kuipeleleza nchi. (Mose akampa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.)
17 So Moses sent them, to spy out the land of Canaan, —and said unto them—Go up, here in the South, Yea ye shall go up the mountain;
Mose alipowatuma wakaipeleleze Kanaani, alisema, “Pandeni kupitia Negebu, mwende mpaka nchi ya vilima.
18 And shall see the land, what it is, —And the people that dwell thereupon, Whether they are, strong, or weak, Whether they are, few or many;
Mwone nchi ni ya namna gani, na kama watu waishio humo wana nguvu au ni wadhaifu, iwapo ni wachache au wengi.
19 And what, the land, is, wherein they dwell, Whether it is, good, or, bad, —And the cities within which they dwell, Whether in camps or in strongholds;
Wanaishi katika nchi ya namna gani? Je, ni nzuri au mbaya? Wanaishi katika miji ya namna gani? Je, haina kuta au ngome?
20 And what the land is, Whether, fat, or, lean, Whether there is timber therein or is not, Then shall ye pluck up courage and take of the fruit of the land. Now the days, were the days of the first-fruits of grapes.
Ardhi iko aje? Ina rutuba au la? Je, kuna miti ndani yake au la? Jitahidini kadiri mwezavyo kuleta baadhi ya matunda ya nchi.” (Ulikuwa msimu wa kuiva zabibu za kwanza.)
21 So they went up, and spied out the land, —from the wilderness of Zin unto Rehob at the entering in of Hamath.
Hivyo wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka Jangwa la Sini hadi Rehobu, kuelekea Lebo-Hamathi.
22 Yea they went up in the South and entered as far as Hebron, and there, were Ahiman Sheshai and Talmai descendants of the Anak. Now, Hebron, was built seven years, before Zoan of Egypt.
Wakapanda kupitia Negebu hadi wakafika Hebroni, mahali ambapo Ahimani, Sheshai na Talmai, wazao wa Anaki, waliishi. (Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba kabla ya mji wa Soani ulioko Misri.)
23 And they entered as far as the ravine of Eschol, and cut down, from thence a branch with one cluster of grapes, and bare it on a pole between two, —also of the pomegranates and of the figs.
Walipofika katika Bonde la Eshkoli, walivunja tawi lililokuwa na kishada kimoja cha zabibu. Wawili wao wakalichukua lile tawi kwenye mti, pamoja na komamanga na tini.
24 That place, was called, The Ravine of Eschol ["Cluster-ravine"]—on account of the cluster, which was cut down from thence by the sons of Israel.
Eneo lile likaitwa Bonde la Eshkoli kwa sababu ya kile kishada cha zabibu ambacho Waisraeli walikikata huko.
25 And they returned from spying out the land, —at the end of forty days.
Mwishoni mwa siku arobaini wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
26 So they took their journey, and came in unto Moses and unto Aaron and unto all the assembly of the sons of Israel into the wilderness of Paran, towards Kadesh, —and brought back word—unto them and unto all the assembly, and showed them the fruit of the land.
Wakarudi kwa Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli huko Kadeshi kwenye Jangwa la Parani. Hapo ndipo walipotoa habari kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya hiyo nchi.
27 And they recounted unto him, and said, We entered into the land whither thou didst send us, and surely it doth flow with milk and honey, and, this, is the fruit thereof.
Wakampa Mose taarifa hii: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo inatiririka maziwa na asali! Hili hapa tunda lake.
28 Nevertheless surely mighty, are the people that dwell in the land, —and, the cities, walled in, exceeding great, moreover also, the descendants of the Anak, saw we there.
Lakini watu wanaoishi huko ni wenye nguvu, na miji yao ina ngome na ni mikubwa sana. Huko tuliona hata wazao wa Anaki.
29 Amalek, dwelleth in the land of the South; And, the Hittite, and the Jebusite and the Amorite, dwell in the mountain And the Canaanite, dwelleth by the sea, and by the side of the Jordan.
Waamaleki wanaishi Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanaishi katika nchi ya vilima; nao Wakanaani wanaishi karibu na bahari na kando ya Yordani.”
30 And Caleb stilled the people unto Moses, —and said unto them—Let us go straight up, and possess it, for we shall, surely prevail, against it.
Kisha Kalebu akawanyamazisha watu mbele ya Mose na kusema, “Imetupasa kupanda na kuimiliki nchi, kwa maana hakika tunaweza kufanya hivyo.”
31 But the men who went up with him said, We cannot go up against the people, —for stronger, are they than we.
Lakini watu waliokuwa wamepanda pamoja naye wakasema, “Hatuwezi kuwashambulia wale watu; wana nguvu kutuliko sisi.”
32 So they sent forth a rumour of the land which they had spied out, among the sons of Israel, saying, —As touching the land through which we passed to spy it out, it is, land that eateth up them who dwell therein, And all the people that we saw in the midst thereof, were men of great stature.
Wakaeneza taarifa mbaya miongoni mwa Waisraeli kuhusu nchi waliyoipeleleza. Wakasema, “Nchi tuliyoipeleleza hula watu waishio ndani yake. Watu wote tuliowaona huko ni majitu.
33 And, there, saw we the giants, sons of Anak [descended] of the giants, —And we were in our own eyes, as grass-hoppers, And, so, were we in their eyes.
Tuliwaona Wanefili huko (wazao wa Anaki wanatokana na Wanefili.) Tulijiona kama panzi machoni petu wenyewe, nao ndivyo walivyotuona.”

< Numbers 13 >