< Nehemiah 12 >

1 Now, these, are the priests and the Levites, who came up with Zerubbabel son of Shealtiel, and Jeshua, —Seraiah, Jeremiah, Ezra;
Hawa ndio makuhani na Walawi waliokuja pamoja na Zerubabeli mwana wa Shealueli, pamoja na Yoshua Seraya, Yeremia, Ezra,
2 Amariah, Malluch, Hattush;
Amaria, Maluki, Hatushi,
3 Shecaniah, Rehum, Meremoth;
Shekania, Harimu na Meremothi.
4 Iddo, Ginnethoi, Abijah;
Kulikuwa na Iddo, Ginethoni, Abiya,
5 Mijamin, Maadiah, Bilgah;
Miyamini, Maazia, Bilgai,
6 Shemaiah, and Joiarib, Jedaiah;
Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
7 Sallu, Amok, Hilkiah, Jedaiah, —these, were the chiefs of the priests and their brethren, in the days of Jeshua.
Salu, Amoki, Hilkia, na Yedaya. Hawa walikuwa wakuu wa makuhani na washirika wao katika siku za Yoshua.
8 And, the Levites, Jeshua, Binnui, Kadmiel, Sherebiah, Judah, Mattaniah, —over the choirs, he and his brethren;
Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na Matania, aliyekuwa akiongoza nyimbo za shukrani, pamoja na washirika wake.
9 and Bakbukiah and Unno their brethren, were over against them, in wards.
Bakbukia na Uno, washirika wao, walisimama pembeni yao wakati wa huduma.
10 And Jeshua, begat Joiakim, —and Joiakim, begat Eliashib, and, Eliashib, [begat] Joiada;
Yoshua alikuwa babaye Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa babaye Yoyada,
11 and, Joiada, begat Jonathan, —and, Jonathan, begat Jaddua.
Yoyada alimzaa Yonathani, Yonathani akamzaa Yadua.
12 And, in the days of Joiakim, were priests, ancestral chiefs, —of Seraiah, Meraiah, of Jeremiah, Hananiah;
Katika siku za Yoyakimu hawa walikuwa makuhani, wakuu wa jamaa; Meraya alikuwa mkuu wa Seraya, Hanania alikuwa kiongozi wa Yeremia,
13 of Ezra, Meshullam, —of Amariah, Jehohanan;
Meshulam alikuwa kiongozi wa Ezra, Yehohanani alikuwa kiongozi wa Amaria,
14 of Malluchi, Jonathan, —of Shebaniah, Joseph;
Yonathani alikuwa kiongozi wa Maluki, na Yusufu alikuwa kiongozi wa Shekania.
15 of Harim, Adna, —of Meraioth, Helkai;
Ili kuendelea, Adna alikuwa kiongozi wa Harimu, Helkai kiongozi wa Meremothi,
16 of Iddo, Zechariah, —of Ginnethon, Meshullam;
Zekaria alikuwa kiongozi wa Ido, Meshulamu alikuwa kiongozi wa Ginethoni, na
17 of Abijah, Zichri, —of Miniamin, of Moadiah, Piltai;
Zikri alikuwa kiongozi wa Abia wa Miyaamini. Piltai alikuwa kiongozi wa Maazia.
18 of Bilgah, Shammua, —of Shemaiah, Jehonathan;
Shamua alikuwa kiongozi wa Bilgai, Yehonathani alikuwa kiongozi wa Shemaya,
19 and, of Joiarib, Mattenai, —of Jedaiah, Uzzi;
Matenai alikuwa kiongozi wa Yoyaribu, Uzi alikuwa kiongozi wa Yedaya,
20 of Sallai, Kallai, —of Amok, Eber;
Kalai alikuwa kiongozi wa Salu, Eberi alikuwa kiongozi wa Amok,
21 of Hilkiah, Hashabiah, —of Jedaiah, Nethanel.
Hashabia alikuwa kiongozi wa Hilkia, na Nethanel alikuwa kiongozi wa Yedaya.
22 The Levites—in the days of Eliashib, Joiada, and Johanan, and Jaddua, were recorded as ancestral chiefs, —also the priests, unto the reign of Darius the Persian.
Katika siku za Eliashibu, Walawi Eliashibu, Yoyada, Yohana, na Yadua waliandikwa kama vichwa vya familia, na makuhani waliandikwa wakati wa utawala wa Dariyo wa Persia.
23 the sons of Levi, ancestral heads, were written in the book of Chronicles, —even until the days of Johanan, son of Eliashib.
Wana wa Lawi na viongozi wao wa familia waliandikwa katika Kitabu cha tarehe hadi siku za Yohana mwana wa Eliashibu.
24 And, the chiefs of the Levites, Hashabiah, Sherebiah, and Jeshua son of Kadmiel, with their brethren over against them, to praise—to give thanks, by the commandment of David the man of God, —ward joined to ward.
Wakuu wa Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia, na Yeshua mwana wa Kadmieli, pamoja na washirika wao, waliokuwa wamesimama mbele yao kumtukuza na kumshukuru, akijibu sehemu kwa sehemu, kwa kutii amri ya Daudi, mtu wa Mungu.
25 Mattaniah and Bakbukiah, Obadiah, Meshullam, Talmon, Akkub, were watchers, doorkeepers of the ward, in the storehouses of the gates.
Matania, Bakbukia, Obadiya, Meshulamu, Talmoni na Akubu walikuwa walinzi wa malango waliokuwa wakiwa wamesimama katika vyumba vya hazina penye malango.
26 These, were in the days of Joiakim, son of Jeshua, son of Jozadak, —and in the days of Nehemiah the pasha, and Ezra the priest the scribe.
Walitumika katika siku za Yoyakimu, mwana wa Yoshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za Nehemiya, gavana na Ezra kuhani na mwandishi.
27 And, at the dedication of the wall of Jerusalem, they sought the Levites, out of all their places, to bring them to Jerusalem, —to keep the dedication and the rejoicing, both with thanksgiving and with music, cymbals, harps, and with lyres.
Katika kujitolea kwa ukuta wa Yerusalemu, watu walitafuta Walawi popote walipokuwa wakiishi, wakawaleta Yerusalemu ili kusherehekea kujitolea kwa furaha, pamoja na shukrani na kuimba kwa ngoma, vinanda na vinubi.
28 So the sons of the singers gathered themselves together, —both out of the circuit round about Jerusalem, and out of the villages of the Netophathites;
Ushirika wa waimbaji walikusanyika pamoja kutoka wilaya iliyozunguka Yerusalemu na kutoka vijiji vya Wanetofathi.
29 also out of Beth-gilgal, and out of the fields of Geba, and Azmaveth, —for, villages, had the singers builded for themselves, round about Jerusalem.
Walikuja kutoka Beth-gilgali na kutoka katika mashamba ya Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji karibu na Yerusalemu.
30 And the priests and the Levites purified themselves, —and purified the people, and the gates, and the wall.
Makuhani na Walawi wakajitakasa, kisha wakawatakasa watu, milango na ukuta.
31 Then brought I up the rulers of Judah upon the wall, —and I appointed two large choirs, even to go in procession to the right, upon the wall, towards the dung-gate;
Kisha nilikuwa na viongozi wa Yuda kwenda juu ya ukuta, na mimi kuteua mikutano miwili mikubwa ya hao walioshukuru. Mmoja alienda upande wa kulia juu ya ukuta kuelekea lango la jaa.
32 and after them went Hoshaiah, and half the rulers of Judah;
Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda walimfuata,
33 then Azariah, Ezra, and Meshullam;
na baada yake akaenda Azaria, Ezra na Meshulamu,
34 Judah, and Benjamin, and Shemaiah, and Jeremiah;
Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia
35 and, of the sons of the priests, with trumpets, Zechariah—son of Jonathan—son of Shemaiah—son of Mattaniah, son of Micaiah, son of Zaccur, son of Asaph;
na wana wa makuhani waliokuwa na tarumbeta, na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Mataniya, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu.
36 and his brethren—Shemaiah and Azarel, Milalai, Gilalai, Maai, Nethanel, and Judah, Hanani, with the instruments of music of David, the man of God, —with Ezra the scribe before them;
Na pia jamaa za Zekaria, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda, Hanani, pamoja na vyombo vya muziki vya Daudi mtu wa Mungu. Ezra mwandishi alikuwa mbele yao.
37 and, over they fountain gate and straight before them, they went up by the stairs of the city of David, at the going up of the wall, —above the house of David, even as far as the water-gate, eastward.
Na kwa Lango la Chemchemi walikwenda moja kwa moja na madaraja ya mji wa Daudi juu ya kupanda kwa ukuta, juu ya nyumba ya Daudi, kwenye lango la Maji upande wa mashariki.
38 And, the second choir, was going over against them, I, following it, —with the half of the people upon the wall, above the tower of the ovens, even as far as the broad wall;
Na waimbaji wengine ambao walishukuru wakaenda upande mwingine. Niliwafuata juu ya ukuta pamoja na nusu ya watu, juu ya mnara wa vinyago, hadi kuta kubwa,
39 and above the gate of Ephraim, and upon the old gate, and upon the fish-gate, and the tower of Hananel, and the tower of Hammeah, even as far as the sheep-gate, —and they came to a stand, at the gate of the guard.
na juu ya lango la Efraimu, na mlango wa kale, na kwa lango la samaki na mnara wa Hananeli na mnara wa Hamea, kwa lango la Kondoo, na wakasimama kwenye mlango wa walinzi.
40 So the two choirs, came to a stand, at the house of God, —and I, and half the deputies with me;
Kwa hiyo, mikutano miwili ya wale waliomshukuru walipata nafasi yao katika nyumba ya Mungu, na mimi pia nikachukua nafasi yangu na nusu ya viongozi pamoja nami.
41 and, the priests—Eliakim, Maaseiah, Miniamin, Micaiah, Elioenai, Zechariah, and Hananiah, with trumpets;
Na makuhani wakachukua nafasi zao Eliakimu, Maaseya, Miyamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, na Hanania wenye tarumbeta,
42 and Maaseiah and Shemaiah and Eleazar and Uzzi and Jehohanan and Malchijah and Elam and Ezer, —and the musicians sounded, aloud with Jezrahiah who was over them.
Maaseya, na Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu, Ezeri. Waimbaji waliimba na Yezrahia kama wasimamizi.
43 And they sacrificed, on that day, great sacrifices, and rejoiced, for, God, had caused them to rejoice with great joy, moreover also, the women and children, rejoiced, —so that the rejoicing of Jerusalem was heard afar off.
Walitoa dhabihu kubwa siku ile, wakafurahi, kwa sababu Mungu alikuwa amewafurahisha kwa furaha kubwa. Pia wanawake na watoto walifurahi. Hivyo furaha ya Yerusalemu ikasikiwa toka mbali.
44 And there were set in charge, on that day, certain men, over the chambers for the treasures, for the heave-offerings, for the firstfruits, and for the tithes, to gather into them, out of the fields of the cities, the portions appointed by the law, for the priests, and for the Levites, —for, the joy of Judah, was over the priests and over the Levites, who were remaining.
Siku hiyo watu waliteuliwa juu ya nyumba ya hazina kwa ajili ya michango, matunda ya kwanza, na zaka, ili kuzikusanya ndani yao sehemu zinazohitajika katika sheria za makuhani na Walawi. Kila mmoja aliteuliwa kufanya kazi mashambani karibu na miji. Kwa maana Yuda alifurahi juu ya makuhani na Walawi waliokuwa wamesimama mbele yao.
45 So they kept the charge of their God, and the charge of the purification, and [so did] the singers and the doorkeepers, —according to the commandment of David and of Solomon his son.
Walifanya utumishi wa Mungu wao, na huduma ya utakaso, kwa mujibu wa amri ya Daudi na ya mwanawe Sulemani, na hivyo
46 For, in the days of David and Asaph, of old, there were chiefs of the singers, and songs of praise and thanksgiving, unto God.
Zamani za kale, katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa na wasimamizi wa waimbaji, na kulikuwa na nyimbo za sifa na shukrani kwa Mungu.
47 Now, all Israel—in the days of Zerubbabel, and in the days of Nehemiah, used to give the portions of the singers and the doorkeepers, the need of a day upon its day, —and they hallowed them unto the Levites, and, the Levites, hallowed them unto the sons of Aaron.
Katika siku za Zerubabeli na katika siku za Nehemia, Israeli wote walitoa sehemu za kila siku kwa waimbaji na walinzi wa mlango. Wakaweka pembeni sehemu ya Walawi, na Walawi waliweka sehemu ya wana wa Haruni.

< Nehemiah 12 >