< Nahum 2 >
1 He that breaketh in pieces hath come up over thy face, Keep the keeps, —watch the way, brace the loins, make vigour very firm.
Yule ambaye atakuharibu vipande vipande anakuja dhidi yako. Linda kuta za mji, linda barabara, jitieni nguvu ninyi wenyewe, yakusanyeni majeshi yenu.
2 For Yahweh hath restored the excellency of Jacob, like the excellency of Israel, —for the plunderers have plundered them, and, their vine branches, have they marred.
Maana Yehova anarejesha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli, ingawa wateka nyara waliwaharibu na kuharibu matawi ya zabibu zao.
3 The shield of his heroes, is made red, the men of war, are clad in crimson, on fire, are the chariot-steels, on the day he maketh ready, —and, the lances, are put in motion.
Ngao za mashujaa wake ni nyekundu, na watu hodari wamevaa nguo nyekundu; magari ya vita yameandaliwa yanang'ara kwenye vyuma vyake wakati wa mchana, na mikuki ya mivinje inarushwa hewani.
4 In the streets, madly go the chariots, they rush along in the broadways, —their appearance, is like torches, as lightnings, hither and thither do they run.
Magari ya vita yapo kasi kwenye mitaa; yanakimbia mbele na nyuma katika mitaa. Yapo kama kurunzi, na yanakimbia kama radi.
5 Let him call to mind his nobles, they shall stumble as they go—let them hasten to her wall, yet the storming cover, is prepared.
Yule ambaye atakuvunja vipande vipande anawaita maafisa wake; wanajikwaa kila mmoja kwa mwingine katika kutembea kwao; wanaharakisha kuushambulia ukuta wa mji. Ngao kubwa imetayarishwa kujikinga na hawa washambuliaji.
6 The gates of the rivers, have been opened, —and, the palace, doth quake.
Malango kwenye mito yamelazishwa kufunguka, na jumba la mfalme linaanguka kwenye uharibifu.
7 And, Huzzab, hath been taken captive—hath been led up, —and, her handmaids, are making a moan like the sound of doves, as they taber upon their heart.
Husabu amevuliwa mavazi yake na amachukuliwa; watumishi wake wa kike wanaomboleza kama njiwa, wanavipiga vifua vyao.
8 Yet, as for Nineveh, like a reservoir of waters, are her waters, —but, those men, are in flight! Stand! stand! but no one is turning.
Ninawi ni kama bwawa la maji linalovuja, watu wake kwa pamoja wanakimbia kama maji yanayotiririka. Wengine wanasema, “Simama, simama,” lakini hakuna anayegeuka nyuma.
9 Plunder silver, plunder gold, —and there is no end to the costly furnishing, rich with every article of delight.
Chukua nyara ya fedha, kuchua nyara ya dhahabu, maana hakuna mwisho wake, kwa fahari ya vitu vyote vizuri vya Ninawi.
10 Emptiness, yea turned to emptiness, aye deserted [is she]! with, heart, unnerved, and, a tottering, of knees, and, anguish, in all loins, and, the faces of them all, have withdrawn their colour.
Ninawi ipo tupu na imeharibiwa. Moyo wa kila mtu unayeyuka, magoti ya kila mmoja yanagongana pamoja, na uchungu upo kwa kila mmoja; sura zao wote zimepauka.
11 Where is the lair of the lions? Yea the very feeding-place of the young lions, —where walked the lion, the lioness, the lion’s whelp, with none to make them afraid?
Sasa liko wapi pango la simba, sehemu ambapo simba wadogo hula chakula, sehemu ambapo simba dume na simba jike walitembea, pamoja wana-simba, ambapo hawakuogopa kitu chochote?
12 The lion, used to tear in pieces enough for his whelps, and to strangle for his lionesses, —and then fill with prey his holes, and his lairs with what he had torn.
Simba alirarua mawindo yake vipande vipande kwa ajili ya watoto wake; aliwanyonga mawindo wake kwa ajili ya wake zake, na kulijaza pango lake mawindo, makao yake kwa mizoga iliyoraruliwa.
13 Behold me! against thee, Declareth Yahweh of hosts, Therefore will I burn up in smoke her chariots, and, thy young lions, shall be devoured by the sword, —so will I cut off, out of the earth, thy prey, nor shall be heard any more, the voice of thine envoy.
“Tazama, mimi nipo kinyume na wewe- hili ni neno la Yehova wa majeshi. Nitayachoma magari yenu ya vita katika moshi, na upanga utateketeza simba wenu vijana. Nitazuia nyara zenu kutoka kwenye nchi yangu, na sauti za wajumbe wenu hazitasikika tena.”