< Micah 4 >

1 But it shall come to pass, in the afterpart of the days, that the mountain of the house of Yahweh shall be, set up, as the head of the mountains, and, exalted, shall it be, above the hills, —and peoples, shall stream thereunto;
Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote; utainuliwa juu ya vilima, na watu wa mataifa watamiminika humo.
2 Yea many nations, shall go, and say—come ye, and let us ascend unto the mountain of Yahweh, and unto the house of the God of Jacob, that he may teach us of his ways, and we may walk in his paths, —for, out of Zion, shall go forth a law, and, the word of Yahweh, out of Jerusalem;
Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
3 And he will judge between many peoples, and be umpire to strong nations far and wide, —and they will beat their swords into ploughshares, and their spears into pruning-hooks, Nation—against nation—shall not lift up sword, neither shall they learn—any more—to make war.
Atahukumu kati ya mataifa mengi, na ataamua migogoro ya mataifa yenye nguvu na yaliyo mbali. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
4 And they shall dwell—every man—under his own vine and under his own fig-tree, with none to make them afraid, —for, the mouth of Yahweh of hosts, hath spoken.
Kila mtu ataketi chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, wala hakuna mtu atakayewaogopesha, kwa kuwa Bwana Mwenye Nguvu Zote amesema.
5 For, all the peoples, walk, every man in the name of his god, —we, therefore, will walk in the name of Yahweh our God, to times age-abiding and beyond.
Mataifa yote yanaweza kutembea katika jina la miungu yao; sisi tutatembea katika jina la Bwana Mungu wetu milele na milele.
6 In that day, Declareth Yahweh, will I take up her teat is lame, and, her that hath been an outcast, will I carry, —even whomsoever I have afflicted;
“Katika siku hiyo,” asema Bwana, “nitawakusanya walemavu; nitawakusanya walio uhamishoni na wale niliowahuzunisha.
7 And will make of her that was lame a residue, and of her that was removed far away a strong nation, —and Yahweh, shall be king, over them, in Mount Zion, from henceforth, even unto times age-abiding.
Nitawafanya walemavu kuwa mabaki, wale waliofukuzwa kuwa taifa lenye nguvu. Bwana atatawala juu yao katika Mlima Sayuni kuanzia siku hiyo na hata milele.
8 Thou, therefore, O Migdal-eder, mound of the daughter of Zion, as far as thee, shall it come, —so shall arrive the chief dominion, the kingdom of the daughter of Jerusalem.
Lakini kuhusu wewe, ee mnara wa ulinzi wa kundi, ee ngome ya Binti Sayuni, milki ya awali itarudishwa kwako, ufalme utakuja kwa Binti Yerusalemu.”
9 Meanwhile, wherefore shouldst thou cry out aloud? King, is there none within thee? or hath, thy counselor, perished? for labour, hath seized thee, as a woman in child-birth: —
Kwa nini sasa unalia kwa nguvu: kwani huna mfalme? Je, mshauri wako amekufa, hata maumivu yakukamate kama ya mwanamke aliye na utungu wa kuzaa?
10 Be in labour, and bear, O daughter of Zion, as a woman in child-birth, —for, meanwhile, shalt thou go forth out of the city, and dwell in the field, and shalt come as far as Babylon, there, shalt thou be delivered, there, will Yahweh, redeem thee, out of the grasp of thine enemies.
Gaagaa kwa utungu, ee Binti Sayuni, kama mwanamke mwenye utungu wa kuzaa, kwa kuwa sasa ni lazima uuache mji ukapige kambi uwanjani. Utakwenda Babeli; huko utaokolewa. Huko Bwana atakukomboa kutoka mikononi mwa adui zako.
11 Meanwhile, therefore, shall be gathered against thee many nations, —who are saying—Let her be defiled, and let our eyes gaze upon Zion.
Lakini sasa mataifa mengi yamekusanyika dhidi yako. Wanasema, “Mwache anajisiwe, macho yetu na yatazame Sayuni kwa furaha!”
12 But, they, know not the purposes of Yahweh, neither have they discerned his counsel, —for he hath gathered them, as sheaves, to a threshing-floor.
Lakini hawayajui mawazo ya Bwana; hawauelewi mpango wake, yeye awakusanyaye kama miganda kwenye sakafu ya kupuria.
13 Arise and thresh, O daughter of Zion, for, thy horn, will I make to be iron, and, thy hoofs, will I make to he bronze, so shalt thou beat in pieces many peoples, —and shalt devote to Yahweh their unrighteous gain, and their substance, to the Lord of all the earth.
“Inuka upure, ee Binti Sayuni, kwa kuwa nitakupa pembe za chuma; nitakupa kwato za shaba na utavunja vipande vipande mataifa mengi.” Utatoa mapato yao waliopata kwa udanganyifu kwa Bwana, utajiri wao kwa Bwana wa dunia yote.

< Micah 4 >