< Micah 3 >

1 Then said I, Hear, I pray you, ye heads of Jacob, and ye judges of the house of Israel, —Is it not yours to know justice?
Nimesema'”Sasa sikilizeni, ninyi viongozi wa Yakobo na kutawala nyumba ya Israeli: Je siyo sahihi kwenu kuielewa haki?
2 Ye haters of right, and lovers of wrong, —tearing away their skin from off them, and their flesh from off their bones;
Ninyi manaochukia mazuri na kupenda uovu, ninyi mnaoambua ngozi yao, miili yao kutoka kwenye mifupa yao-
3 Who indeed have eaten the flesh of my people, and, their skin from off them, have stript, and, their bones, have they broken in pieces, —and will spread them out, as flesh with a fork, and as flesh, in the midst of a pot.
ninyi mnaokula pia miili ya watu wangu, na kuambua ngozi yao, kuvunja mifupa yao, na kuwakatakata katika vipande vipande, kama nyama kwenye chungu, kama nyama kwenye sufuria kubwa.
4 Then, shall they make outcry unto Yahweh, but he will not answer them, —that he may hide his face from them, at that time, even as they have made wicked their doings.
Kisha ninyi watawala mtalia kwa Yahwe, lakini hatawajibu. Atauficha uso wake kutoka kwenu kipindi hicho, kwasababu mmefanya matendo maovu.”
5 Thus, saith Yahweh, concerning the prophets who are leading astray my people, —who bite with their teeth, and then cry—Prosper! and whoso holdeth not to their mouth, they hallow against him a war!
Yahwe asema hivi kuhusu manabii ambao wawafanyao watu wangu kushindwa, “Kwa wale wawalishao wanatangaza, 'Kutakuwa na ustawi.' Lakini kwa wale wasioweka kitu kwenye vinywa vyao, wanaanzisha vita dhidi yake.
6 Therefore, shall it be night to you, for lack of vision, and darkness to you, for lack of divination, —and the sun, shall go in, over the prophets, and the day, shall be overcast because of them;
Kwa hiyo, itakuwa usiku kwenu usiokuwa na maono juu yenu; itakuwa giza ili kwamba msiweze kubashiri. Jua litakwenda chini juu ya manabii, na siku itakuwa giza juu yao.
7 And the men of vision, shall turn pale, and the diviners, shall blush, and shall put a covering upon their lip, all of them, —because there is no answer of God.
Waonaji watawekwa kwenye aibu, waaguzi wa watachanganyikiwa. Wote watafunga midomo yao, kwa kuwa hakuna jibu kutoka kwangu.”
8 But, in very deed, I, am full of vigour, with the spirit of Yahweh, and of justice and of valour, —to declare to Jacob, his transgression, and to Israel, his sin.
Lakini kwangu, nimejazwa nguvu kutoka kwa Roho wa Yahwe, na nimejaa haki na uweza, kumwambia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
9 Hear this, I pray you, ye heads of the house of Jacob, and ye judges of the house of Israel, —who abhor justice, and, all right, do pervert:
Sasa sikieni hii, ninyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, na watawala wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao mnaochukia haki, na kupotosha kila haki.
10 Building Zion, with deeds of blood, —and Jerusalem, with perversity.
Mnaijenga Sayuni kwa damu na Yerusalemu kwa uovu.
11 Her heads, for a bribe, pronounce sentence, and, her priests, for a price, give direction, and, her prophets, for silver, divine, —yet, on Yahweh, they lean, saying, Is not, Yahweh, in our midst? there shall not come upon us, calamity.
Viongozi wenu huhukumu kwa rushwa, makuhani wenu hufundisha kwa hijara, na manabii wenu hufanya utabiri kwa ajili ya pesa. Hata hivyo bado mtamtegemea Yahwe na kusema, “Je hayupo Yahwe pamoja nasi? Hakuna uovu utakaokuja juu yetu.”
12 Wherefore, for your sake, Zion, as a field, shall be ploughed, and, Jerusalem, unto heaps of ruins, shall be turned, —and, the mountain of the house, shall [be] like mounds in a jungle.
Kwa hiyo, kwasababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa rundo la kifusi, na mwinuko wa hekalu utakuwa kama mwinuko wa msituni.

< Micah 3 >