< Mark 4 >

1 And, again, began he to be teaching by the sea; and there come together unto him a very great multitude, so that, he, into a boat, entering, was sitting upon the sea, —and, all the multitude, were, near the sea upon the land.
Yesu alianza kufundisha tena akiwa kando ya ziwa. Umati mkubwa wa watu ulimzunguka hata ikambidi aingie katika mashua na kuketi. Watu wakawa wamekaa katika nchi kavu, kando ya ziwa.
2 And he began to teach them, in parables, many things, and was saying unto them, in his teaching—
Aliwafundisha mambo mengi kwa mifano, na katika mafundisho yake aliwaambia,
3 Hearken! Lo! the sower went forth to sow;
“Sikilizeni! Mpanzi alikwenda kupanda mbegu.
4 And it came to pass, as he sowed, some, indeed, fell by the pathway, and the birds came, and devoured it;
Alipokuwa akipanda, nyingine zilianguka njiani, ndege wakaja wakazila.
5 And, some, fell on the rocky places, [even] where it had not much earth, —and, straightway, it sprang forth, by reason of its not having depth of earth;
Nyingine zilianguka penye mawe pasipokuwa na udongo mwingi. Mbegu hizo ziliota mara kwa kuwa udongo haukuwa na kina.
6 and, when the sun arose, it was scorched, —and, by reason of its not having root, it was dried up;
Jua lilipochomoza, zikachomeka; na kwa kuwa mizizi yake haikuwa na nguvu, zikanyauka.
7 And, some, fell among the thorns, and the thorns came up and choked it, and, fruit, it yielded not;
Nyingine zilianguka kwenye miti ya miiba, nayo ikakua na kuzisonga, nazo hazikuzaa nafaka.
8 And, other, fell into the good ground, and was yielding fruit, coming up and growing, —and was bearing, thirtyfold and sixtyfold and a hundredfold,
Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikakua na kuzaa: moja punje thelathini, moja sitini na nyingine mia.”
9 And he was saying—He that hath ears to hear, let him hear!
Kisha akawaambia, “Mwenye masikio na asikie!”
10 And when he was alone they who were about him with the twelve questioned him as to the parables;
Yesu alipokuwa peke yake, baadhi ya wale waliomsikia walimwendea pamoja na wale kumi na wawili, wakamwuliza juu ya hiyo mifano.
11 and he was saying unto them—To you, the sacred secret hath been given of the kingdom of God, whereas, to them who are outside, in parables are all things coming to pass, —that
Naye akawaambia, “Ninyi mmejaliwa kujua siri ya Utawala wa Mungu, lakini wale walio nje wataambiwa kila kitu kwa mifano,
12 They may surely look and yet not see, and surely hear and yet not understand, lest once they should return and it be forgiven them.
ili, Watazame kweli, lakini wasione. Wasikie kweli, lakini wasielewe. La sivyo, wangemgeukia Mungu, naye angewasamehe.”
13 And he saith unto them—Know ye not this parable? How then will ye get to know all the parables?
Basi, Yesu akawauliza, “Je, ninyi hamwelewi mfano huu? Mtawezaje basi, kuelewa mfano wowote?
14 The sower, soweth the word;
Mpanzi hupanda neno la Mungu.
15 And these are they beside the pathway where the word is sown, —and, as soon as they hear, straightway, cometh Satan, and snatcheth away the word which hath been sown into them;
Watu wengine ni kama wale walio njiani ambapo mbegu zilianguka. Hawa hulisikia hilo neno lakini mara Shetani huja na kuliondoa neno hilo lililopandwa ndani yao.
16 And these are likewise they upon the rocky places sown, —who, as soon as they hear the word, straightway, with joy receive it,
Watu wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa penye mawe. Mara tu wanapolisikia hilo neno hulipokea kwa furaha.
17 and have no root in themselves, but, only for a season are, —afterwards, when there ariseth tribulation or persecution by reason of the word, straightway, they find cause of stumbling;
Lakini haliwaingii na kuwa na mizizi ndani yao; huendelea kulizingatia kwa kitambo tu, na wakati taabu au udhalimu vinapotokea kwa sababu ya hilo neno mara wanakata tamaa.
18 And others are they who among thorns are sown, —these are they who hear the word,
Watu wengine ni kama zile mbegu zilizoanguka penye miti ya miiba. Huo ni mfano wa wale wanaolisikia hilo neno,
19 and, the anxieties of the age, and the deceit of wealth, and the covetings about the remaining things, entering in, choke up the word, and, unfruitful, it becometh; (aiōn g165)
lakini wasiwasi wa ulimwengu huu, anasa za mali na tamaa za kila namna huwaingia na kulisonga hilo neno, nao hawazai matunda. (aiōn g165)
20 And those yonder are they who on the good ground are sown, —who, indeed, hear the word, and accept it, and bear fruit—thirtyfold and sixtyfold and a hundredfold.
Lakini wengine ni kama zile mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. Hawa hulisikia hilo neno, wakalipokea, wakazaa matunda: wengine thelathini, wengine sitini na wengine mia moja.”
21 And he was saying unto them—Doth the lamp come that under the measure it should be put, or under the couch? Is it not that upon the lampstand it may be put?
Yesu akaendelea kuwaambia, “Je, watu huwasha taa wakaileta ndani na kuifunika kwa pishi au kuiweka mvunguni? La! Huiweka juu ya kinara.
22 For it is not hidden, save that it may be made visible; neither did it get hidden away, but that it might come into a place where it could be seen.
Basi, kila kilichofichwa kitafichuliwa, na kila kilichofunikwa kitafunuliwa.
23 If any one hath ears to hear, let him hear.
Mwenye masikio na asikie!”
24 And he was saying unto them—Be taking heed what ye are hearing: —with what measure ye mete, it shall be measured unto you, and added unto you;
Akawaambia pia, “Sikilizeni kwa makini mnachosikia! Kipimo kilekile mnachowapimia watu wengine, ndicho mtakachopimiwa; tena mtazidishiwa.
25 For, he that hath, it shall be given, unto him, and, he that hath not, even what he hath, shall be taken from him.
Aliye na kitu atapewa zaidi; asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.”
26 And he was saying—Thus, is the kingdom of God: As a man may cast seed upon the earth,
Yesu akaendelea kusema, “Ufalme wa Mungu ni kama ifuatavyo. Mtu hupanda mbegu shambani.
27 and be sleeping and rising, night and day, —and the seed be sprouting, and lengthening itself, —how, he, knoweth not:
Usiku hulala, mchana yu macho na wakati huo mbegu zinaota na kukua; yeye hajui inavyofanyika.
28 of itself, the earth beareth fruit, —first, a blade, afterwards, an ear, after that, full corn in the ear;
Udongo wenyewe huiwezesha mimea kukua na kuzaa matunda: kwanza huchipua jani changa, kisha suke, na mwishowe nafaka ndani ya suke.
29 but, as soon as the fruit yieldeth itself up, straightway, he sendeth forth the sickle, because standing by is the harvest.—
Nafaka inapoiva, huyo mtu huanza kutumia mundu wake, maana wakati wa mavuno umefika.”
30 And he was saying—How shall we liken the kingdom of God, or, in what parable, shall we put it?
Tena, Yesu akasema, “Tuufananishe Utawala wa Mungu na nini? Tuueleze kwa mifano gani?
31 As a grain of mustard seed, —which, whensoever it may be sown upon the earth, is less than all the seeds that are upon the earth;
Ni kama mbegu ya haradali ambayo ni ndogo kuliko mbegu zote.
32 and, as soon as it is sown, springeth up, and becometh greater than all garden plants, and produceth large branches, so that, under the shade thereof, the birds of heaven can find shelter.
Lakini ikisha pandwa, huota na kuwa mmea mkubwa kuliko mimea yote ya shambani. Matawi yake huwa makubwa hata ndege wa angani huweza kujenga viota vyao katika kivuli chake.”
33 And, with many such parables as these, was he speaking unto them the word, —according as they were able to hear;
Yesu aliwahubiria ujumbe wake kwa mifano mingine mingi ya namna hiyo; aliongea nao kadiri walivyoweza kusikia.
34 but, without a parable, was he not speaking unto them, —privately, however, unto his own disciples, was he explaining all things.
Hakuongea nao chochote bila kutumia mifano; lakini alipokuwa pamoja na wanafunzi wake peke yao alikuwa akiwafafanulia kila kitu.
35 And he saith unto them, on that day, when evening came, Let us cross over unto the other side;
Jioni, siku hiyohiyo, Yesu aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvuke ziwa, twende ng'ambo.”
36 and, dismissing the multitude, they take him with them, as he was, in the boat, and, other boats, were with him.
Basi, wakauacha ule umati wa watu, wakamchukua Yesu katika mashua alimokuwa. Palikuwapo pia mashua nyingine hapo.
37 And there ariseth a great tempest of wind, —and, the waves, were dashing over into the boat, so that, already being filled, was the boat.
Basi, dhoruba kali ikaanza kuvuma, mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikaanza kujaa maji.
38 And he was in the stern, on the cushion, sleeping. And they arouse him, and say unto him, Teacher! carest thou not that we perish?
Yesu alikuwa sehemu ya nyuma ya mashua, amelala juu ya mto. Basi, wanafunzi wakamwamsha na kumwambia, “Mwalimu, je, hujali kwamba sisi tunaangamia?”
39 And, roused up, he rebuked the wind, and said unto the sea—Hush! be still! and the wind lulled, and it became a great calm.
Basi, akaamka, akaukemea ule upepo na kuyaamrisha mawimbi ya ziwa, “Kimya! Tulia!” Hapo upepo ukakoma, kukawa shwari kabisa.
40 And he said unto them—Why, are ye, fearful? Not yet, have ye faith?
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mbona mnaogopa? Je, bado hamna imani?”
41 And they were caused to fear a great fear, and were saying one to another—Who then is, this, that, both the wind and the sea, give ear unto him?
Nao wakaogopa sana, wakawa wanaulizana, “Huyu ni nani basi, hata upepo na mawimbi vinamtii?”

< Mark 4 >