< Malachi 2 >
1 Now, therefore, for you, is this charge, O ye priests: —
“Sasa onyo hili ni kwa ajili yenu, enyi makuhani.
2 If ye will not hear, and if ye will not lay it to heart, to give glory to my Name, saith Yahweh of hosts, then will I send among you the curse, and will curse your blessings, —and indeed I have cursed them, because ye are not at all laying it to heart.
Kama hamtasikiliza, na kama hamtaki kuielekeza mioyo yenu kuheshimu Jina langu, nitatuma laana juu yenu, nami nitalaani baraka zenu. Naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamkuielekeza mioyo yenu kuniheshimu mimi,” Asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
3 Behold me! threatening, on your account, the seed, and I will scatter refuse upon your faces, the refuse of your festivals, —and one shall carry you away unto it;
“Kwa sababu yenu nitawakatilia mbali wazao wenu. Nitazipaka nyuso zenu mavi, mavi ya dhabihu zenu. Nanyi mtafukuzwa pamoja nazo mtoke mbele zangu.
4 So shall ye know that I sent unto you this charge, —as being my covenant with Levi, saith Yahweh of hosts.
Nanyi mtajua kuwa nimewapelekea onyo hili ili kwamba Agano langu na Lawi lipate kuendelea,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
5 My covenant, was with him, Life and Well-being, so I gave them to him—[I] as One to be revered— and he did revere me, — and, before my Name, dismayed, was he.
“Agano langu lilikuwa pamoja naye, agano la uhai na amani, nami nilimpa yote, ili aniche na kuniheshimu, naye akaniheshimu na kusimama akilicha Jina langu.
6 The deliverance of truth, was in his mouth, and, perverseness, was not found in his lips, — In well-doing and in uprightness, walked he with me, and, multitudes, did he turn from iniquity.
Fundisho la kweli lilikuwa kinywani mwake, wala hakuna uongo wowote uliopatikana katika midomo yake. Alitembea nami katika amani na unyofu, naye akawageuza wengi kutoka dhambini.
7 For, the lips of a priest, should keep knowledge, and, a deliverance, should men seek at his mouth, — for, the messenger of Yahweh of hosts, he is.
“Kwa maana yapasa midomo ya kuhani kuhifadhi maarifa. Tena kutoka kinywani mwake watu wangepaswa kutafuta mafundisho, kwa sababu yeye ni mjumbe wa Bwana Mwenye Nguvu Zote.
8 But, ye, have departed out of the way, ye have caused multitudes to stumble at the deliverance, — ye have violated the covenant of Levi, saith Yahweh of hosts.
Lakini mmegeuka mkaiacha njia, na kwa mafundisho yenu mmesababisha wengi kujikwaa. Mmevunja agano na Lawi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
9 Therefore, I also, will suffer you to be despised and of no account unto all the people, —in proportion as none of you have been keeping my ways, but have had respect to persons, in giving your deliverance.
“Kwa hiyo nimewasababisha ninyi kudharauliwa na kufedheheshwa mbele ya watu wote, kwa sababu hamkufuata njia zangu, bali mmeonyesha upendeleo katika mambo ya sheria.”
10 Is there not, one Father, to us all? Did not, one GOD, create us? Wherefore should we deal treacherously one with another, profaning the covenant of our fathers?
Je, sote hatuna Baba mmoja? Hatukuumbwa na Mungu mmoja? Kwa nini basi tunalinajisi Agano la baba zetu kwa kukosa uaminifu kila mmoja kwa mwenzake?
11 Judah, hath dealt treacherously, and, an abomination, hath been wrought in Israel, and in Jerusalem, — for Judah, had profaned, the holy place of Yahweh, which he had loved, and hath taken to himself the daughter of a foreign GOD.
Yuda amevunja uaminifu. Jambo la kuchukiza limetendeka katika Israeli na katika Yerusalemu: Yuda amepanajisi mahali patakatifu apendapo Bwana, kwa kuoa binti wa mungu mgeni.
12 May Yahweh, cut off, from the man that doeth it—him that crieth out and him that answereth, out of the tents of Jacob, — him also that bringeth near a present to Yahweh of hosts.
Kwa maana kwa mtu yeyote atendaye jambo hili, Bwana na amkatilie mbali kutoka hema za Yakobo, hata kama huwa anamletea Bwana Mwenye Nguvu Zote sadaka.
13 And, this, a second time, will ye do, covering with tears, the altar of Yahweh, weeping and making outcry, —because he will not again turn unto the gift, and receive [it] with acceptance, at your hands?
Kitu kingine mnachokifanya: Mnaifurikisha madhabahu ya Bwana kwa machozi. Mnalia na kuugua kwa sababu yeye haziangalii tena sadaka zenu wala hazikubali kwa furaha kutoka mikononi mwenu.
14 Yet ye say, For what cause? Because, Yahweh, hath been witness between thee and the wife of thy youth, with whom, thou, hast dealt treacherously, though, she, was thy consort, and thy covenant wife.
Mnauliza, “Kwa nini?” Ni kwa sababu Bwana ni shahidi kati yako na mke wa ujana wako, kwa sababu umevunja uaminifu naye, ingawa yeye ni mwenzako, mke wa agano lako la ndoa.
15 Now was it not, One, [who] made [you] who had, the residue of the spirit? What, then, of that One? He was seeking a godly seed. Therefore should ye take heed to your spirit, and, with the wife of thy youth, do not thou deal treacherously.
Je, Bwana hakuwafanya wao kuwa mmoja? Katika mwili na katika roho wao ni wa Mungu. Kwa nini wawe mmoja? Kwa sababu Mungu alikuwa akitafuta mzao mwenye kumcha Mungu. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, mtu asivunje uaminifu kwa mke wa ujana wake.
16 For he hateth divorce, saith Yahweh, God of Israel, him also who covereth with violence his own clothing, saith Yahweh of hosts, —therefore should ye take heed to your spirit, and not deal treacherously.
“Ninachukia kuachana,” asema Bwana, Mungu wa Israeli, “pia nachukia mtu anayejivika jeuri kama vazi,” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. Kwa hiyo jihadharini wenyewe katika roho zenu, wala msije mkavunja uaminifu.
17 Ye have wearied Yahweh with your words, and yet ye say, Wherein have we been wearisome? When ye have said, Everyone who doeth wrong, is right in the eyes of Yahweh, and, in them, he hath taken delight, or, Where is the God of justice?
Mmemchosha Bwana kwa maneno yenu. Nanyi mnauliza, “Tumemchosha kwa namna gani?” Mmemchosha kwa kusema, “Wote watendao mabaya ni wema machoni pa Bwana, naye anapendezwa nao” au “Mungu wa haki yuko wapi?”