< Luke 6 >

1 And it came to pass, on a Sabbath, that he was passing along through cornfields, and his disciples were plucking and eating the ears of corn, rubbing them with their hands.
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 But, certain of the Pharisees, said—Why are ye doing what is not allowed on the Sabbath?
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 And, making answer unto them, Jesus said—Have ye never read, even this, what David did when he hungered, he, and they who were with him—
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 How he entered into the house of God, and, the presence-bread, receiving, did eat, and gave to them who were with him, which it is not allowable to eat, save alone, to the priests?
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 And he was saying to them—The Son of Man is, Lord of the Sabbath.
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 And it came to pass, on another Sabbath, that he entered into the synagogue, and was teaching, and there was a man there, and, his right hand, was withered.
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 Now the Scribes and the Pharisees were narrowly watching him, whether, on the Sabbath, he healeth, —that they might find whereof to accuse him.
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 But, he, knew their reasonings, and said to the man who had the, withered, hand—Arise, and stand forward in the midst! And, arising, he stood forward.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 And Jesus said unto them—I ask you, whether it is allowed, on the Sabbath, to do good or to do harm, —life, to save, or, to destroy.
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 And, looking round upon them all, he said unto him—Stretch forth thy hand! and, he, did so, and his hand was restored.
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 But, they, were filled with folly, and began conversing one with another, as to, what they might do with Jesus.
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 And it came to pass, in these days, that he went forth into the mountain to pray, and was spending the night in the prayer-house of God.
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 And, when it became day, he called his disciples, and chose from them, twelve, whom also he named, Apostles, —
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 Simon, whom also he named Peter, and Andrew his brother; and James and John; and Philip and Bartholomew;
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 and Matthew and Thomas; and James, son of Alphaeus, and Simon, who was called Zealot; and Judas, [son] of James,
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 and Judas Iscariot, who became betrayer; —
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 and, coming down with them, he stood upon a level place, also a great multitude of his disciples, —and a great throng of the people, from all Judaea and Jerusalem and the sea-coast of Tyre and Zidon, who had come to hearken unto him and to be healed from their diseases;
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 and, they who were molested by impure spirits, were being cured;
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 and, all the multitude, were seeking to touch him, because, power, from him, was coming forth, and healing all.
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 And, he, lifting up his eyes towards his disciples, was saying: —Happy, ye destitute, for, yours, is the kingdom of God.
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Happy, ye that hunger now, for ye shall be filled. Happy, ye that weep now, for ye shall laugh.
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 Happy, are ye, whensoever men shall hate you, and whensoever they shall separate you, and reproach you, and cast out your name as evil, for the sake of the Son of Man:
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 be rejoiced in that day, and leap, for lo! your reward, is great in heaven; for, according to the same things, were their fathers doing unto the prophets.
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 But alas! for you, ye wealthy, for ye are duly receiving you consolation.
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 Alas! for you, ye who are filled full now, for ye shall hunger. Alas! ye that laugh now, for ye shall mourn and weep.
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 Alas! whensoever all men shall, speak well of you, for, according to the same things, were their fathers doing unto the false prophets.
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 But, unto you, I say, who are hearkening: Be loving your enemies; be doing, good, unto them that hate you;
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 Be blessing them that curse you; be praying for them that wantonly insult you.
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 To him who is smiting thee upon the one cheek, be offering, the other also; and, from him who is taking away thy mantle, thy tunic also, do not forbid:
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 To every one asking thee, give, and, from him that taketh away thy possessions, ask them not back.
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 And, according as ye desire that men be doing unto you, be ye doing unto them, in like manner.
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 And, if ye love them that love you, what sort of thanks are there for you? for, even sinners, love, such as love them.
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 [For], if ye even do good unto them that do good unto you, what sort of thanks are there for you? Even sinners, the same, are doing.
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 And, if ye lend to them from whom ye are hoping to receive, what sort of thanks are there for you? Even sinners, unto sinners, do lend, that they may receive back, as much.
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 But love your enemies, and do good and lend, hoping for, nothing, back; and your reward shall be, great, and ye shall be sons of the Most High, —for, he, is, gracious, unto the ungrateful and wicked.
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 Become ye compassionate, according as, your Father, is, compassionate;
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 And do not judge, and in nowise shall ye be judged; and do not condemn, and in nowise shall ye be condemned; release, and ye shall be released;
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 Give, and it shall be given unto you: good measure, pressed down, shaken together, running over, will they give into your lap; for, with what measure ye mete, shall it be measured back unto you.
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 He spake, moreover, a parable also, unto them: Can, the blind, guide, the blind? will not, both, fall into, a ditch?
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 A disciple is not above the teacher; but, when trained, every one shall be as his teacher.
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 But why beholdest thou the mote that is in the eye of thy brother, while, the beam that is in thine own eye, thou dost not consider?
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 How canst thou say to thy brother—Brother! let me cast out the mote that is in thine eye, —thyself, the beam in thine own eye, not beholding? Hypocrite! cast out, first, the beam out of thine own eye, and, then, shalt thou see clearly, to cast out, the mote that is in the eye of thy brother.
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 For a good tree doth not produce worthless fruit, neither again doth, a worthless tree, produce good fruit.
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 For, every tree, by its own fruit, becometh known. For not, of thorns, do they gather figs, neither, of a bramble-bush, do they gather, a bunch of grapes.
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 The good man, out of the good treasure of the heart, bringeth forth that which is good; and, the wicked man, out of the wicked heart, bringeth forth that which is wicked; for, out of an overflowing of heart, speaketh, his mouth.
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 And why call ye me, Lord! Lord! and not do the things that I say?
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 Every one coming unto me, and hearkening unto my words, and doing them, I will suggest to you, whom he is like:
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 He is like unto a man building a house, who digged, and deepened, and laid a foundation upon the rock, —and, a flood, coming, the stream burst against that house, and was not strong enough to shake it, because it had been, well, built.
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 But, he that hath heard and not done, is like unto a man having built a house upon the earth, without a foundation, —against which the stream burst, and, straightway, it fell in; and it came to pass, that, the crash of that house, was, great.
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< Luke 6 >