< Luke 3 >

1 Now, in the fifteenth year of the supremacy of Tiberius Caesar, —Pontius Pilate being governor of Judaea, and Herod being tetrarch of Galilee, and, Philip his brother, tetrarch of Ituraea and the country of Trachonitis, and Lysanius, tetrarch of Abylene, —
Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 in the High-priesthood of Annas and Caiaphas, came a word of God unto John the son, of Zechariah, in rue desert;
na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
3 and he came into all the country about the Jordan, proclaiming an immersion of repentance into remission of sins:
Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
4 as it is written in the book of the discourses of Isaiah the prophet: A voice of one crying aloud! In the desert, prepare ye the way of the Lord, straight, be making his paths;
Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
5 Every chasm, shall be filled up, and, every mountain and hill, be made low; and the, crooked, places shall become, straight, and the, rugged, places, smooth ways; —
Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
6 And all flesh shall see the salvation of God.
Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu.”
7 He was saying, therefore, unto the multitudes who were going forth to be immersed by him—Broods of vipers! who suggested to you, to flee from the coming wrath?
Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
8 Bring forth, therefore, fruits worthy of repentance, and do not begin to be saying within yourselves, As our father, we have, Abraham; for, I say unto you—God is able, out of these stones, to raise up children unto Abraham.
Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
9 And, already, even the axe, unto the root of the trees is being laid; every tree, therefore, not bringing forth [good] fruit, is to be hewn down, and, into fire, to be cast.
Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
10 And the multitude began to question him saying—What, then, shall we do?
Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?”
11 And, answering, he said unto them—He that hath two tunics, let him share with him that hath none, and, he that hath food, in like manner, let him be doing.
Akawajibu, “Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
12 And there came, even tax-collectors, to be immersed; and they said unto him—Teacher! what, shall we, do?
Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
13 And, he, said unto them, Nothing more than what is appointed you, exact ye.
Naye akawaambia, “Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.”
14 Then were questioning him, soldiers also, saying—What shall, even we, do? And he said unto them—Molest ye, no one, neither accuse falsely; and be content with your supplies.
Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.”
15 Now, as the people were in expectation, and all were deliberating in their hearts, concerning John, —whether by any means, he, might be, the Christ,
Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
16 John answered, saying unto all—I, indeed, in water, am immersing you, but he that is mightier than I, cometh, the thong of whose sandals I am not worthy to unloose, —he, will immerse you in Holy Spirit and fire:
Hapo Yohane akawaambia wote, “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 whose fan is in his hand, to clear out his threshing-floor, and to gather the wheat into his granary; but, the chaff, will he burn up with fire unquenchable.
Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.”
18 So then indeed, as to many things and various, he exhorted, and continued telling his glad-message unto the people.
Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
19 But, Herod the tetrarch, being reproved by him concerning Herodias, the wife of his brother, and concerning all the wicked things Herod had done,
Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
20 added this also unto all, —he locked up John in prison.
Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
21 Now it came to pass, when one and all the people were immersed, Jesus also, having been immersed, and being at prayer, heaven was opened;
Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
22 and the Holy Spirit descended, in bodily appearance, as a dove, upon him, —and, a voice out of heaven, came—Thou, art my Son, the Beloved, in thee, I delight.
na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
23 And, Jesus himself, was, when he began, about thirty years of age, being the son, as was supposed—of Joseph, of Heli:
Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
24 of Matthat, of Levi, of Melchi, —of Jannai, of Joseph:
Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
25 of Mattathias, of Amos, of Nahum, —of Esli, of Naggai:
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
26 of Maath, of Mattathias, of Semein, —of Josech, of Joda:
mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
27 of Joanan, of Rhesa, of Zerubbabel, —of Salathiel, of Neri:
mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 of Melchi, of Addi, of Cosam, —of Elmadam, of Er:
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 of Jesus, of Eliezer, of Jorim, —of Matthat, of Levi:
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
30 of Symeon, of Judas, of Joseph, —of Jonam, of Eliakim:
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
31 of Melea, of Menna, of Mattatha, —of Natham, of David:
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 of Jesse, of Obed, of Boaz, —of Salmon, of Nashon:
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 of Amminadab, of Arni, of Hezron, —of Perez, of Judah:
mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
34 of Jacob, of Isaac, of Abraham, —of Terah, of Nahor:
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 of Serug, of Reu, of Peleg, —of Eber, of Shelah:
mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 of Cainan, of Arphaxad, of Shem, —of Noah, of Lamech:
mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
37 of Methuselah, of Enoch, of Jared, —of Mahalaleel, of Cainan:
mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
38 of Enos, of Seth, —of Adam; of God.
mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.

< Luke 3 >