< Luke 20 >

1 And it came to pass, on one of the days, as he was teaching the people in the temple, and telling the good tidings, that the High-priests and the Scribes, with the Elders, came upon him, —
Ikawa siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuhubiri injili, makuhani wakuu na walimu wa Sheria walimwendea pamoja na wazee.
2 and spake, saying, unto him—Tell us, by what authority, these things, thou art doing, and, who, is it, that gave thee this authority.
Walizungumza, wakimwambia, 'Tuambie ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya? Au ni nani huyo ambaye amekupa mamlaka haya? “
3 And answering, he said unto them—I too, will question, you, as to a matter, —and tell me!
Naye akajibu, akawaambia, 'Nami pia nitawauliza swali. Niambieni
4 The immersion of John, Of heaven, was it, or of men?
ubatizo wa Yohana. Je, ulitoka mbinguni ama kwa watu? '
5 And they deliberated together by themselves, saying—If we say, Of heaven, he will say, Wherefore did ye not believe him?
Lakini wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, 'Tukisema, `litoka mbinguni, atatuuliza, ` Basi, mbona hamkumwamini?'
6 But, if we say, Of men, the people, one and all, will stone us, for, persuaded, they are, that, John, was, a prophet.
Na tukisema; ilitoka kwa wanadamu; watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii. '
7 And they answered, that they knew not whence.
Basi, wakamjibu ya kwamba hawakujua ilikotoka.
8 And, Jesus, said unto them—Neither do, I, tell, you, by what authority, these things, I am doing.
Yesu akawaambia, '“Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”
9 And he began, unto the people, to be speaking this parable: —A man, planted a vineyard, and let it out to husbandmen, and went from home for a long time.
Aliwaambia watu mfano huu, “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima wa mizabibu, na akaenda nchi nyingine kwa muda mrefu.
10 And, in due season, he sent unto the husbandmen, a servant, that, of the fruit of the vineyard, they might give him; but, the husbandmen, having beaten him, sent him away empty.
Kwa muda uliopangwa, alimtuma mtumishi kwa wakulima mizabibu, kwamba wampe sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wakulima wa mzabibu wakampiga, wakamrudisha mikono- mitupu.
11 And he, further, sent another servant; but, they, beating, that one also, and dishonouring him, sent him away, empty.
Kisha akamtuma tena mtumishi mwingine na nao wakampiga, kumtendea vibaya, na wakamrudisha mikono- mitupu.
12 And he, further, sent, a third; but, they, bruising, this one also, thrust him out.
Alimtuma tena wa tatu na nao wakamjeruhi na kumtupa nje.
13 And the lord of the vineyard said—What shall I do? I will send my son, the beloved, —It may be, that, him, they will respect.
Hivyo bwana wa shamba akasema, 'Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa. Labda watamheshimu. '
14 But he husbandmen, seeing him, began to deliberate one with another, saying—This, is, the heir: Let us slay him, that, ours, may be, the inheritance.
Lakini wakulima wa mzabibu walipomwona, walijadili wao kwa wao wakisema, `Huyu ndiye mrithi. Tumuue, ili urithi wake uwe wetu. '
15 And, thrusting him forth outside the vineyard, they slew him. What, then, will the lord of the vineyard do unto them?
Wakamtoa nje ya shamba la mizabibu na kumuua. Je bwana shamba atawafanya nini?
16 He will come, and destroy these husbandmen, and give the vineyard unto others. But, when they heard it, they said—Far be it!
Atakuja kuwaangamiza wakulima wa mzabibu, na atawapa shamba hilo wengine”. 'Nao waliposikia hayo, wakasema, 'Mungu amekataa'
17 But, he, looking at them, said—What, then, is this that is written, —A stone which the builders’ rejected, The same, hath become, head of the corner?
Lakini Yesu akawatazama, akasema, “Je andiko hili lina maana gani? 'Jiwe walilolikataa wajenzi, limekuwa jiwe la pembeni'?
18 Every one who falleth on that stone, will be sorely bruised, but, on whomsoever it shall fall, it will utterly destroy him.
Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo, atavunjika vipande vipande. Lakini yule ambaye litamwangukia, litamponda. '
19 And the Scribes and the High-priests sought to thrust on him their hands, in that very hour; and feared the people; for they perceived that, against them, spake he this parable.
Hivyo waandishi na wakuu wa makuhani walitafuta njia ya kumkamata wakati huohuo, walijua kwamba alikuwa amesema mfano huu dhidi yao. Lakini waliwaogopa watu.
20 And, watching narrowly, they sent forth suborned men, feigning themselves to be, righteous, that they might lay hold of a word of his, so as to deliver him up unto the rule and the authority of the governor.
Walimuangalia kwa makini, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wapate kupata kosa kwa hotuba yake, ili kumpelekakwa watawala na wenye mamlaka.
21 And they questioned him, saying—Teacher! we know that, rightly, thou speakest and teachest, and respectest no person, but, in truth, the way of God, dost teach:
Nao wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli na si kushawishiwa na mtu yeyote, lakini wewe hufundisha ukweli kuhusu njia ya Mungu.
22 Is it allowable for us to give, unto Caesar, tribute, or not?
Je, ni halali kwetu kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
23 But, observing their villainy, he said unto them—
Lakini Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24 Shew me a denary. Of whom, hath it an image and inscription? And, they, said—Of Caesar.
“Nionyesheni dinari. Sura na chapa ya nani ipo juu yake?” Walisema, '“Ya Kaisari.”
25 And, he, said unto them—Well then! render the things of Caesar, unto Caesar, and the things of God, unto God.
Naye akawaambia, 'Basi, mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari, na Mungu yaliyo yake Mungu.'
26 And they could not lay hold of the saying, before the people; and, marvelling at his answer, they held their peace.
Waandishi na wakuu wa makuhani hawakuwa na uwezo wa kukosoa kile alichosema mbele ya watu. Wakastaajabia majibu yake na hawakusema chochote.
27 But there came near certain of the Sadducees, they who say, Resurrection, there is none! and questioned him,
Baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale ambao wanasema kwamba hakuna ufufuo,
28 saying—Teacher! Moses, wrote for us, If one’s brother die, having a wife, and, he, be, childless, that his brother shall take the wife, and raise up seed unto his brother.
wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, Musa alituandikia kwamba kama mtu akifiwa na ndugu mwenye mke ambaye hana mtoto basi anapaswa kumchukuna mke wa ndugu yake na kuzaa nae kwa ajili ya kaka yake.
29 Seven brethren, therefore, there were, —and, the first, taking a wife, died childless,
Kulikuwa na ndugu saba Wa kwanza alioa, akafa bila kuacha mtoto,
30 And, the second,
na wa pili pia.
31 and the third, took her, —yea, likewise, even the seven; They left no children, and died:
Wa tatu akamchukua vilevile, vivyo hivyo wa saba hakuacha watoto na akafa.
32 Later on, the woman also, died.
Baadaye yule mwanamke pia akafa.
33 The woman, therefore, in the resurrection, Of which of them, doth she become wife? for, the seven, had her to wife.
Katika ufufuo atakuwa mke wa nani? Maana wote saba walikuwa wamemwoa. '
34 And Jesus said unto them—The sons of this age, marry, and are given in marriage, — (aiōn g165)
Yesu akawaambia, “Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa. (aiōn g165)
35 But, they who have been accounted worthy, that age, to obtain, and the resurrection that is from among the dead, neither marry, nor are given in marriage; (aiōn g165)
Lakini wale wanastaohili kupokea ufufuo wa wafu na kuingia uzima wa milele hawaoi wala hawaolewi. (aiōn g165)
36 For they cannot, even die any more, —for, equal unto messengers, are they, and are, sons of God, Of the resurrection, being, sons.
Wala hawawezi kufa tena, kwa sababu huwa sawasawa na malaika na ni watoto wa Mungu, wana wa ufufuo.
37 But, that the dead do rise, even Moses, disclosed at the bush, when he calleth the Lord—The God of Abraham and God of Isaac and God of Jacob:
Lakini hiyo wafu wanafufuliwa, hata Musa alionyesha mahali katika habari za kichaka, pale alimwita Bwana kama Mungu wa Ibrahimu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.
38 Now, God, he is not, of the dead, but, of the living, —for, all, unto him, do live.
Sasa, yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa sababu wote huishi kwake. “
39 And certain of the Scribes, answering, said—Teacher! Well, hast thou spoken.
Baadhi ya walimu wa Sheria wakamjibu, 'Mwalimu, umejibu vema. '
40 For, no longer, were they daring to ask him any questions.
Hawakuthubutu kumwuliza maswali mengine zaidi.
41 And he said unto them—How say they, that, the Christ, is, David’s Son?
Yesu akawaambia, “Ki vipi watu wanasema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42 For, David himself, saith, in [the] book of Psalms: Said the Lord, unto my Lord, Sit thou at my right hand,
Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti mkono wa kulia,
43 Until I make thy foes thy footstool.
mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako. '
44 David, therefore, calleth, him Lord: How, then, his son, is he?
Daudi anamwita Kristo 'Bwana', basi atakuwaje mwana wa Daudi?”
45 And, all the people hearing, he said unto the disciples:
Watu wote walipokuwa wakimsikiliza akawaambia wanafunzi wake,
46 Be taking heed of the Scribes—Who desire to walk about in long robes, and are fond of salutations in the markets, and first seats in the synagogues, and first couches in the chief meals, —
'Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na wapenda salamu maalum sokoni na viti vya heshima katika masinagogi, na maeneo ya heshima karamuni.
47 Who devour the houses of widows, and, for a show, are a long time at prayer. These, shall receive, a heavier sentence.
Wao pia hula nyumba za wajane, na wanajifanya wanasali sala ndefu. Hawa watapokea hukumu kubwa zaidi. '

< Luke 20 >