< Luke 2 >
1 Now it came to pass, in those days, that there went forth a decree from Caesar Augustus, for all the inhabited earth to be enrolled:
Sasa katika siku hizo, ikatokea kwamba Kaisari Agusto alitoa agizo akielekeza kwamba ichukuliwe sensa ya watu wote wanaoishi duniani.
2 this enrolment, first was made while Cyrenius was governor of Syria:
Hii ilikuwa ni sensa ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio akiwa gavana wa Siria.
3 and all were journeying to be enrolled, each one unto his own city.
Hivyo kila mmoja akaenda mjini kwake kuandikishwa sensa.
4 And Joseph also went up from Galilee, out of a city Nazareth, into Judaea, into the city of David which is called Bethlehem; because he was of the house and family of David:
Naye Yusufu aliondoka pia katika mji wa Nazareti huko Galilaya na akasafiri Yudea katika mji wa Bethlehemu, ujulikanao kama mji wa Daudi, kwa sababu alitokea katika ukoo ya Daudi.
5 to enrol himself with Mary who was betrothed to him, she being with child.
Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Mariamu, ambaye alikuwa amemposa na alikuwa akitazamia mtoto.
6 And it came to pass, while they were there, that the days were fulfilled for her to give birth;
Sasa ilitokea kwamba, wakiwa kule wakati wake wa kujifungua mtoto ukawadia.
7 and she gave birth to her firstborn son, and wrapped him in swaddling clothes, and laid him in a manger, because there was no room for them in the inn.
Akajifungua mtoto wa kiume, mzaliwa wake wa kwanza, akamzungushia nguo mwilini kumkinga na baridi mtoto. Ndipo akamweka kwenye kihori cha kulishia wanyama, kwa sababu haikuwepo nafasi kwenye nyumba za wageni.
8 And there were, shepherds, in the same country, dwelling in the fields, and keeping the watches of the night over their flock.
Katika eneo hilo, walikuwapo wachungaji walioishi mashambani wakilinda makundi ya Kondoo wao usiku.
9 And, a messenger of the Lord, stood over them, and, a glory of the Lord, shone round about them; and they feared, a great fear.
Ghafla, malaika wa Bwana akawatokea, na utukufu wa Bwana ukang'aa kuwazunguka, na wakawa na hofu sana.
10 And the messenger said unto them—Be not afraid! For lo! I bring you good tidings of a great joy, the which shall be for all the people:
Ndipo malaika akwaambia, “Msiogope, kwasababu nawaletea habari njema ambayo italeta furaha kuu kwa watu wote.
11 That there hath been born unto you, this day, a saviour, —Who is Christ the Lord—in the city of David!
Leo Mwokozi kazaliwa kwaajili yenu mjini mwa Daudi! Yeye ndiye Kristo Bwana!
12 And, this, to you is, a sign: Ye shall find a babe, wrapped in swaddling clothes, and lying in a manger.
Hii ndiyo ishara ambayo mtapewa, mtamkuta mtoto amefungwa nguo na amelala kwenye hori la kulishia wanyama.”
13 And, suddenly, there came to be, with the messenger, the throng of the heavenly host, praising God, and saying—
Ghafla kukawa na jeshi kubwa la mbinguni likaungana na malaika huyo wakamsifu Mungu, wakisema,
14 Glory, in the highest, unto God! And, on earth, peace, among men of goodwill.
“Utukufu kwa Mungu aliye juu sana, na amani iwe duniani kwa wote ambao anapendezwa nao.”
15 And it came to pass, when the messengers had departed from them into heaven, that, the shepherds, began to say one to another—Let us go through forthwith as far as to Bethlehem, and see this thing which hath come to pass, which the Lord hath made known to us.
Ikawa kwamba malaika walipokwisha kuondoka kwenda mbinguni, wachungaji wakasemezena wao kwa wao, “Twendeni sasa kule Bethlehemu, na tukaone hiki kitu ambacho kimetokea, ambacho Bwana ametufahamisha.”
16 And they came, with haste, and found both Mary and Joseph, and the babe lying in the manger.
Wakaharakisha kule, na wakamkuta Mariamu na Yusufu, na wakamuona mtoto amelala kwenye hori la kulishia wanyama.
17 Now, when they beheld, they made known concerning the thing which had been told them as to this child.
Na walipoona hivi, wakawajulisha watu kile walichokuwa wameambiwa kumhusu mtoto.
18 And, all who heard, marvelled concerning the things which had been told by the shepherds unto them;
Wote waliosikia habari hii wakashangazwa na kile kilichosemwa na wachungaji.
19 but, Mary, was closely observing, all, these things, putting them together in her heart.
Lakini Mariamu akaendelea kufikiri kuhusu yote aliyokwisha kuyasikia, akiyatunza moyoni mwake.
20 And the shepherds returned, giving glory and singing praise unto God, over all things which they had heard and seen, according as it had been told unto them.
Wachungaji wakarudi wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa ajili ya kila kitu walichokwisha sikia na kuona, kama tu ilivyokuwa imenenwa kwao.
21 And, when eight days were fulfilled for circumcising him, then was his name called, Jesus, —which it was called by the messenger, before he was conceived in the womb.
Ilipofika siku ya nane na ilikuwa ni wakati wa kumtahiri mtoto, wakamwita jina Yesu, jina alilokwishapewa na yule malaika kabla mimba haijatungwa tumboni.
22 And, when the days of their purification, according to the law of Moses, were fulfilled, they took him up into Jerusalem, to present [him] unto the Lord, —
zao zilizotakiwa za utakaso zilipopita, kulingana na sheria ya Musa, Yusufu na Mariamu wakampeleka hekaluni kule Yerusalemu kumweka mbele za Bwana.
23 according as it is written in the law of the Lord—Every male that is a firstborn, Holy unto the Lord, shall be called,
Kama ilivyoandikwa katika sheria ya Bwana, “Kila mwanaume anayefungua tumbo ataitwa aliyetolewa wakfu kwa Bwana.”
24 and to give a sacrifice, according to that which is said in the law of the Lord—A pair of turtle-doves, or two young pigeons.
Wao vilevile walikuja kutoa sadaka kulingana na kile kinachosemwa katika sheria ya Bwana, “Jozi ya njiwa au makinda mawili ya njiwa.”
25 And lo! there was, a man, in Jerusalem, whose name, was Symeon; and, this man, was righteous and devout, awaiting the consolation of Israel, and Holy Spirit was upon him;
Tazama, palikuwa na mtu katika Yerusalemu ambaye jina lake alikuwa akiitwa Simeoni. mtu huyu alikuwa mwenye haki na mcha Mungu. Yeye alikuwa akisubiri kwa ajili ya mfariji wa Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 and it had been intimated to him by the Holy Spirit, that he should not see death, before he had seen the Christ of the Lord.
Ilikuwa imekwisha funuliwa kwake kupitia Roho Mtakatifu kwamba yeye hangelikufa kabla ya kuwomwona Kristo wa Bwana.
27 And he came, in the Spirit, into the temple; and, when the parents brought in the child Jesus, that they might do according to that which was customary by the law concerning it,
Siku moja alikuja ndani ya hekalu, akiongozwa na Roho Mtakatifu. Ambapo wazazi walimleta mtoto, Yesu, kumfanyia yale yaliyopasa kawaida ya sheria,
28 even he, welcomed it into his arms, and blessed God, and said—
ndipo Simeoni alimpokea mikononi mwake, na akamsifu Mungu na kusema,
29 Now, dost thou dismiss thy servant, O Sovereign, according to thy declaration—in peace;
“Sasa ruhusu mtumishi wako aende kwa amani Bwana, kulingana na Neno lako.
30 Because mine eyes have seen thy salvation,
Kwa kuwa macho yangu yameuona wakovu wako,
31 Which thou hast prepared in face of all the peoples:
ambao umeonekana kwa macho ya watu wote.
32 A light for the unveiling of nations, and the glory of thy people Israel.
Yeye ni nuru kwa ajili ya ufunuo kwa Wamataifa na utukufu wa watu Israeli.”
33 And his father and mother were marvelling over the things which were being spoken concerning him.
Baba na Mama wa mtoto walishangazwa kwa mambo ambayo yalizungumzwa juu yake.
34 And Symeon blessed them, and said unto Mary his mother—Lo! this one, is being set for the falling and rising of many in Israel, and for a sign to be spoken against;
Ndipo Simeoni akawabariki na akasema kwa Mariamu mama yake, “Sikiliza kwa makini! Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli na ni ishara ambayo watu wengi wataipinga.
35 And, thou! through thy very soul, shall pass a sword, that, reasonings, may be revealed, out of many hearts.
Pia ni upanga utakaochoma nafsi yako mwenyewe, ili kwamba mawazo ya mioyo ya wengi yadhihirike”.
36 And there was one Anna, a prophetess, daughter of Phanuel, of the tribe of Asher; —the same, advanced in many days; having lived with a husband seven years from her virginity,
Nabii mwanamke aliyeitwa Ana pia alikuwako hekaluni. Yeye alikuwa binti wa Fanueli kutoka kabila la Asheri. Alikuwa na miaka mingi sana. Naye aliishi na mume wake kwa miaka saba baada ya kuoana,
37 and, she, had been a widow for as long as eighty-four years, —who left not the temple, with fastings and supplications, rendering divine service night and day; —
na ndipo akawa mjane kwa miaka themanini na minne. Naye hakuwahi kuondoka hekaluni na alikuwa akiendelea kumwabudu Mungu pamoja na kufunga na kuomba, usiku na mchana.
38 and, in that very hour, coming near, she began to give thanks unto God, and to speak concerning him unto all who were waiting for the redemption of Jerusalem.
Na kwa wakati huo, alikuja pale walipo akaanza kumshukuru Mungu. Aliongea kumhusu mtoto kwa kila mtu ambaye alikuwa akisubiri ukombozi wa Yerusalemu.
39 And, when they had finished all things that were according to the law of the Lord, they returned into Galilee, into their own city, Nazareth.
Walipomaliza kila kitu walichotakiwa kufanya kuligana na na sheria ya Bwana, walirudi Galilaya, mjini kwao, Nazareti.
40 And, the child, went on growing, and waxing strong, becoming filled with wisdom; and, the favour of God, was upon it.
Mtoto alikua, na akawa na nguvu, akiongezeka katika hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
41 And his parents used to journey yearly into Jerusalem, at the feast of the passover.
Wazazi wake kila mwaka walikwenda Yerusalemu kwaajili ya sikukuu ya Pasaka.
42 And, when he became twelve years, and they went up, according to the custom of the feast,
Alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walikwenda tena wakati mwafaka kidesturi kwa ajili ya sikukuu.
43 and completed the days, and then were returning, the boy Jesus remained behind in Jerusalem, —and his parents noticed it not;
Baada ya kubaki siku zote kwa ajili ya sikukuu, walianza kurudi nyumbani. Lakini mvulana Yesu alibaki nyuma mle Yerusalemu na wazazi wake hawakujua hili.
44 but, supposing him to be in the company, went a day’s journey, and then began to seek for him among their kinsfolk and acquaintances,
Walidhani kwamba yumo kwenye kundi walilokuwa wakisafiri nalo, hivyo walisafiri safari ya siku. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni wa ndugu na marafiki zao.
45 and, not finding him, returned unto Jerusalem, seeking him.
Waliposhindwa kumpata, walirudi Yerusalemu na wakaanza kumtafuta humo.
46 And it came to pass, that, after three days, they found him in the temple, sitting amidst the teachers, —both hearkening unto them, and questioning them.
Ikatokea kwamba baada ya siku tatu, wakampata hekaluni, akiwa ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 Now all who heard him were beside themselves, because of his understanding and his answers.
Wote waliomsikia walishangazwa na ufahamu wake na majibu yake.
48 And, when they behold him, they were astounded, and his mother said unto him—Child! why, hast thou dealt with us, thus? Lo! thy father and I, in anguish, were seeking thee.
Walipomwona, walistaajabu. Mama yake akamwambia, “Mwanangu, kwa nini umetutendea hivi? Sikiliza, baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa.”
49 And he said unto them—Why was it that ye were seeking me? Perceived ye not, that, in the courts of my Father, I must needs be?
Akawaambia, “Kwa nini mmekuwa mkinitafuta? Hamkujua kwamba lazima niwe kwenye nyumba ya Baba yangu?
50 And, they, understood not the thing which he spake to them.
Lakini hawakuelewa nini alichomaanisha kwa maneno hayo.
51 And he went down with them, and came to Nazareth, and was submitting himself unto them. And, his mother, was closely observing all these things in her heart.
Ndipo akaenda pamoja nao mpaka nyumbani Nazareti na alikuwa mtii kwao. Mama yake alihifadhi mambo yote moyoni mwake.
52 And, Jesus, went on advancing in wisdom, and in stature, and in favour with God and men.
Lakini Yesu aliendelea kukua katika hekima na kimo, na akazidi kupendwa na Mungu na watu.