< Luke 12 >
1 Amongst which things, when the ten thousands of the multitude were gathered together, so that they were treading one upon another, he began to be saying, unto his disciples, first—Be keeping yourselves free from the leaven of the Pharisees, the which is, hypocrisy.
Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
2 But, nothing, hath been, covered up, which shall not be uncovered, and hidden, which shall not be made known.
Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
3 Because, as many things as, in the darkness, ye have said, in the light, shall be heard; and, what to the ear ye spake, in the chambers, shall be proclaimed on the housetops.
Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
4 And I say unto you, my friends—Do not be put in fear of them who kill the body, and, after these things, have nothing more uncommon which they can do.
“Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
5 But I will suggest to you, whom ye should fear—Fear him who, after killing, hath authority to cast into gehenna, —Yea, I say unto you—Him, fear ye. (Geenna )
Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo. (Geenna )
6 Are not, five sparrows, sold for two farthings? and, not one from among them, hath been forgotten before God.
Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
7 But, even the hairs of your head, have all been numbered: Be not afraid: many sparrows, ye excel.
Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
8 And I say unto you—Whosoever shall confess me before men, even the Son of Man, will confess him, before the messengers of God;
“Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
9 But, he who denied me before men, shall be denied before the messengers of God.
Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
10 And, whosoever shall say a word against the Son of Man, it shall be forgiven him; but, unto him who, against the Holy Spirit, speaketh profanely, it shall not be forgiven.
“Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11 But, whensoever they shall be bringing you in before the synagogues, and the rulers, and the authorities, do not be anxious how, [or what] ye shall answer, or what ye shall say;
“Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
12 For, the Holy Spirit, shall teach you, in that very hour, what ye ought to say.
Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema.”
13 And one from amongst the multitude said unto him—Teacher! bid my brother divide with me the inheritance.
Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba.”
14 But, he, said unto him—Man! who hath appointed me a judge or divider over you?
Yesu akamjibu, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?”
15 And he said unto them—Mind and be guarding yourselves from all covetousness; for not, in one’s abundance, doth his life spring out of his possessions.
Basi, akawaambia wote, “Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo.”
16 And he spake a parable unto them, saying—A certain rich man’s estate, bare well.
Kisha akawaambia mfano: “Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
17 And he began to deliberate within himself, saying—What shall I do? because I have not where I can gather my fruits.
Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
18 And he said—This, will I do, —I will pull down my barns, and, greater ones, build, and gather, there, all my wheat and good things;
Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
19 and will say to my soul—Soul! thou hast many good things [lying by for many years: be taking thy rest, eat, drink, ] be making merry!
Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
20 But God said unto him—Simple one! on this very night, they are asking, thy soul, from thee; The things, then, which thou hast prepared, whose shall they be?
Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?”
21 [So, is he that is laying up treasure for himself, and is not rich, towards God.]
Yesu akamaliza kwa kusema “Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu.”
22 And he said unto his disciples—For this cause, I say unto you, —Be not anxious for the life, what ye shall eat, nor yet for [your] body, what ye shall put on;
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
23 For, the life, is more, than the food, and, the body, than, the clothing.
Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
24 Consider well the ravens—That they sow nor, neither do they reap, which have neither chamber nor barn, —and, God, feedeth, them! By how much do, ye, excel, the birds?
Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
25 And, who from among you, though anxious, can, unto his stature, add a cubit?
Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
26 If then, not even the least thing, ye can do, why, concerning the rest, are ye anxious?
Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
27 Consider well the lilies, how they grow: they toil not, neither do they spin, and yet I say unto you—Not even Solomon, in all his glory, was arrayed like one of these.
Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
28 But, if God thus adorneth, the grass, which is, in a field, to-day, and, to-morrow, into an oven, is cast, how much rather you, O little-of-faith?
Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
29 Ye, therefore, be not seeking what ye shall eat and what ye shall drink, and be not held in suspense;
“Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
30 For, after all these things, do, the nations of the world, seek, —but, your Father, knoweth that ye need these things.
Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
31 Notwithstanding, be seeking his kingdom, —and, these things, shall be added unto you.
Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
32 Be not afraid, the dear little flock! for your Father delighteth to give you, the kingdom.
“Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
33 Sell your possessions, and give alms, make for yourselves purses that wax not old, —treasure unfailing, in the heavens, where, thief, doth not draw near, and, moth, doth not spoil.
Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
34 For, where your treasure is, there, will your heart he also.
Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
35 Let your loins be girded, and your lamps burning,
“Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
36 And, ye yourselves, like unto men awaiting their own lord, once he may break up out of the marriage-feast, —that, when he cometh and knocketh, straightway, they may open unto him.
muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
37 Happy those servants, whom the lord, when he cometh, shall find watching! Verily, I say unto you—he will gird himself, and make them recline, and, coming near, will minister unto them.
Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
38 And, if, in the second, or if, in the third, watch, he come and find, thus, happy, are, they!
Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
39 But, of this, be taking note—Had the householder known, in what hour the thief was coming, he would have watched, and not suffered his house, to be digged through.
Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
40 Ye, therefore, be getting ready, because, in what hour ye are not thinking, The Son of Man cometh!
Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”
41 But Peter said—Lord! unto us, this parable, speakest thou? or, even unto all?
Petro akamwambia, “Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?”
42 And the Lord said—Who then is the faithful steward, the prudent one, whom the lord will appoint over his body of attendants, to be giving, in due season, the measured allowance of wheat?
Bwana akajibu, “Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
43 Happy, that servant, whom the lord, when he cometh shall find doing, thus!
Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44 Of a truth, I say unto you—Over all his possessions, will he appoint him.
Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
45 But, if that servant should say in his heart—My lord delayeth to come! and should begin to be striking the youths and the maidens, —to be eating also, and drinking, and making himself drunk,
Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
46 The lord of that servant, will have come—on a day when he is not expecting, and in an hour when he is not taking note, —and will cut him asunder, and, his part, with the unfaithful, will appoint.
bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
47 And, that servant, who had come to know the will of his lord, and neither prepared, nor wrought unto his will, shall be beaten with many stripes;
Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
48 Whereas, he who had not come to know, and did things worthy of stripes, shall be beaten with few stripes. And, every one to whom was given much, much, shall be sought from him; and, he to whom they committed much, for more than common, will they ask him.
Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
49 Fire, came I to cast upon the earth, —and what can I wish, if, already, it hath been, kindled?
“Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
50 But, an immersion, have I, to be immersed with, and how am I distressed, until it be ended!
Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51 Suppose ye, that, peace, I am come to give in the earth? Nay, I tell you, but rather division.
Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
52 For there shall be, henceforth, five in one house, divided, —three against two, and two against three:
Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53 There shall be divided—Father against son, and son against father, mother against daughter, and daughter against the mother, —mother-in-law against her daughter-in-law, and daughter-in-law against the mother-in-law.
Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake.”
54 And he went on to say, even unto the multitudes, —Whensoever ye see a cloud springing up from the west, straightway, ye are saying—A thunderstorm is coming! and it happeneth thus.
Yesu akayaambia tena makundi ya watu, “Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
55 And, whensoever a south wind, blowing, ye say—A scorching heat, will there be! and it cometh to pass.
Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
56 Hypocrites! the face of the earth and of the heaven, ye know how to scan; but, this season, how know ye not to scan;
Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
57 Why, moreover, even from yourselves, judge ye not what is just?
“Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
58 For, as thou art going along with thine adversary unto a ruler, on the way, take pains to get a release from him; lest once he drag thee along unto the judge, and, the judge, deliver thee up to the punisher, —and, the punisher, cast thee into prison:
Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
59 I tell thee—In nowise shalt thou come out from thence, until, even the last fraction, thou pay!
Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho.”