< Leviticus 5 >

1 Any person, moreover, whensoever he shall sin in that, when he heareth a voice of swearing, he himself, being a witness either seeing or knowing, —if he do not tell and so hath to bear his iniquity: —
“‘Ikiwa mtu atakuwa ametenda dhambi kwa sababu hakusema alipotakiwa kutoa ushahidi hadharani kuhusu jambo aliloona au kujua habari zake, yeye anastahili adhabu.
2 Or, any person, who toucheth anything unclean, whether the carcase of an unclean wild-beast or the carcase of an unclean tame-beast, or the carcase of an unclean creeping thing, —and it is hidden from him, he himself being unclean, and he becometh aware of his guilt: —
“‘Au kama mtu akigusa kitu chochote ambacho ni najisi, iwe ni mizoga ya wanyama pori walio najisi, au ya wanyama wafugwao walio najisi, au ya viumbe vitambaavyo ardhini, hata akiwa hana habari, amekuwa najisi na mwenye hatia.
3 Or whensoever one shall touch the uncleanness of man, as regardeth any uncleanness of his, wherewith one may become unclean, —and it be hidden from him, and then he himself, getting to know it becometh aware of his guilt: —
“‘Au kama akigusa kitu kilicho kichafu kinachotokana na binadamu, kitu chochote kile kinachoweza kumfanya awe najisi, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
4 Or, any person, whensoever he shall swear, speaking unadvisedly with the lips, to harm or to help, as regardeth anything wherein the son of earth may speak unadvisedly by way of oath, and it be hidden from him, —and then, he himself, getting to know it, becometh aware of his guilt as regardeth any one of these things.
“‘Au kama mtu ameapa kufanya kitu chochote bila kufikiri, kiwe chema au kibaya, kwa vyovyote mtu aweza kuapa bila kujali, hata akiwa hana habari, atakapofahamu atakuwa na hatia.
5 Then shall it be, when he becometh aware of his guilt, as regardeth any one of these things, that he shall confess that wherein he hath sinned;
“‘Wakati mtu yeyote atakapokuwa na hatia katika mojawapo ya haya, lazima akiri ni kwa njia gani ametenda dhambi,
6 and shall bring in as his guilt-bearer unto Yahweh for his sin which he hath committed, a female from the flock—a lamb or a kid of the goats—as a sin-bearer, —so shall the priest put propitiatory-covering over him, because of his sin.
na kama adhabu ya dhambi aliyoitenda, lazima alete kwa Bwana kondoo jike au mbuzi jike kutoka kwenye kundi lake kama sadaka ya dhambi; naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yake.
7 And, if his hand cannot reach sufficient for a lamb, then shall he bring in to bear his guilt—for that he hath sinned—two turtle-doves, or two young pigeons unto Yahweh, —one for a sin-bearer, and one for an ascending-sacrifice.
“‘Lakini huyo mtu kama hataweza kumtoa mwana-kondoo, ataleta hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa Bwana kuwa adhabu kwa ajili ya dhambi yake, mmoja wa hao ndege kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na wa pili kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.
8 And he shall take them in unto the priest, who shall bring near that which is for a sin-bearer first, —and shall nip through the neck close to the head but shall not divide it asunder.
Atawaleta kwa kuhani, ambaye atamtoa kwanza ndege mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Atamvunja shingo na kuacha kichwa chake kikiningʼinia,
9 And he shall sprinkle of the blood of the sin-bearer upon the wall of the altar, and the remainder of the blood, shall he drain out at the base of the altar, —a, sin-bearer, it is.
naye atanyunyiza sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi kwenye pembe za madhabahu. Damu iliyobaki lazima ichuruzwe chini ya madhabahu. Hii ni sadaka ya dhambi.
10 And of the second, shall he make an ascending-sacrifice according to the regulation, —so shall the priest put a propitiatory-covering over him, because of his sin which he hath committed and it shall be forgiven him.
Kisha kuhani atamtoa yule ndege wa pili kama sadaka ya kuteketezwa kwa kufuata utaratibu uliowekwa, na hivyo kufanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoitenda, naye atasamehewa.
11 But if his hand cannot lay hold of two turtledove, or two young pigeons, then shall he bring in as his oblation—because he hath sinned—the tenth of an ephah of fine meal for bearing sin, —he shall not put thereon oil, neither shall he lay thereon frankincense, for a sin-bearer, it is.
“‘Ikiwa basi, hawezi kupata hua wawili au makinda mawili ya njiwa, ataleta sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa ajili ya sadaka ya dhambi. Kamwe asiweke mafuta wala uvumba juu yake, kwa sababu ni sadaka ya dhambi.
12 And he shall bring it in unto the priest, and the priest shall take therefrom a handful, as the memorial thereof, and shall make a perfume at the altar, upon the altar-flames of Yahweh, —a sin-bearer, it is.
Atauleta unga kwa kuhani, ambaye atachukua konzi moja kama sehemu ya kumbukumbu na atauteketeza kwenye madhabahu juu ya sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto. Hii ni sadaka ya dhambi.
13 So shall the priest put a propitiatory-covering over him, on account of his sin which he hath committed, departing from some one of these things, and it shall be forgiven him, —then shall it be the priest’s, like the meal-offering.
Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi yoyote ya hizo alizotenda, naye atasamehewa. Sadaka iliyobaki itakuwa ya kuhani, kama ilivyokuwa ile sadaka ya nafaka.’”
14 And Yahweh spake unto Moses, saying—
Bwana akamwambia Mose:
15 Whensoever, any person, shall commit a trespass, and shall take away by mistake, from the holy things of Yahweh, then shall he bring in as his guilt-bearer unto Yahweh, a ram without defect out of the flock, with thine estimate in silver by shekels, after the shekel of the sanctuary, for a guilt-bearer:
“Mtu anapokiuka na kutenda dhambi pasipo kukusudia kuhusu mojawapo ya mambo matakatifu ya Bwana, huyo mtu ataleta kwa Bwana kama adhabu kondoo dume mmoja kutoka kundi lake, asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Hii ni sadaka ya hatia.
16 that, moreover, which he took away from the sanctuary, shall he make good and the fifth part thereof, shall he add thereunto, and shall give it to the priest, —and, the priest, shall put a propitiatory-covering over him with the guilt-bearing ram and it shall be forgiven him.
Ni lazima alipe kwa yale aliyoshindwa kufanya kuhusu vitu vitakatifu, kwa kuongeza sehemu ya tano ya thamani ile na kuitoa yote kwa kuhani, ambaye atamfanyia upatanisho kwa huyo kondoo dume kama sadaka ya dhambi, naye atasamehewa.
17 And if any person when he shall sin, and do something, departing from any of the commandments of Yahweh, as to things which should not be done, —though he knew it not, shall so become guilty, and shall bear his iniquity,
“Kama mtu akifanya dhambi na kufanya yale yaliyokatazwa katika mojawapo ya amri za Bwana, hata ikiwa hajui, yeye ana hatia na anastahili adhabu.
18 then shall he bring in a ram without defect out of the flock by thine estimate as a guilt-bearer unto the priest, —and the priest shall put a propitiatory-covering over him, on account of his mistake which he made though he knew it not and it shall be forgiven him:
Atamletea kuhani kama sadaka ya hatia kondoo dume kutoka kundi lake, kondoo asiye na dosari na mwenye thamani halisi kifedha. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa kosa alilotenda bila kukusudia, naye atasamehewa.
19 a guilt-bearer, it is, —he was, verily guilty against Yahweh.
Hii ni sadaka ya hatia; amekuwa na hatia kwa kufanya kosa dhidi ya Bwana.”

< Leviticus 5 >