< Judges 10 >

1 And there arose, after Abimelech, to save Israel—Tola son of Puah son of Dodo, a man of Issachar, —and, he, used to sit in Shamir, in the hill country of Ephraim;
Baada ya Abimeleki, Tola, mwana wa Pua, mwana wa Dodo, mtu wa Isakari, aliyekaa Shamiri, katika mlima wa Efraimu, akaondoka ili kuwaokoa Israeli.
2 and he judged Israel, twenty-three years, —and died, and was buried in Shamir.
Akawa mwamuzi wa Israeli miaka ishirini na mitatu. Alikufa na kuzikwa Shamiri.
3 And there arose, after him, Jair the Gileadite, —and judged Israel twenty-two years.
Alifuatiwa na Yairi Mgileadi. Akawa mwamuzi wa Israeli miaka ishirini na miwili.
4 Now he had thirty sons, that rode on thirty ass colts, and they had, thirty cities, —they are called Havvoth-jair, until this day, which are in the land of Gilead.
Alikuwa na wana thelathini waliokuwa wakipanda kwenye punda thelathini, na walikuwa na miji thelathini, ambayo inaitwa Hawoth Yairi hata leo, iliyo katika nchi ya Gileadi.
5 And Jair died, and was buried in Kamon.
Yairi alikufa na kuzikwa Kamoni.
6 And the sons of Israel again did the thing that was wicked in the sight of Yahweh, and served the Baals and the Ashtoreths, and the gods of Syria, and the gods of Zidon, and the gods of Moab, and the gods of the sons of Ammon, and the gods of the Philistines, —and forsook Yahweh, and served him not.
Watu wa Israeli waliendelea kutenda maovu mbele za Bwana, wakaabudu Mabaali, Maashtoreti, miungu ya Aramu, miungu ya Sidoni, miungu ya Moabu, miungu ya wana wa Amoni, na miungu ya Wafilisti. Wakamsahau Bwana na hawakamsujudia tena.
7 So the anger of Yahweh kindled upon Israel, —and he sold them into the hand of the Philistines, and into the hand of the sons of Ammon;
Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawauza mikononi mwa Wafilisti na katika mikono ya wana wa Amoni.
8 and they enfeebled and oppressed the sons of Israel in that year, —eighteen years, did they this unto all the sons of Israel who were beyond the Jordan, in the land of the Amorites, that was in Gilead.
Wakawaangamiza na kuwadhulumu watu wa Israeli mwaka huo, na kwa muda wa miaka kumi na nane waliwafukuza watu wote wa Israeli waliokuwa ng'ambo ya Yordani katika nchi ya Waamori, iliyoko Gileadi.
9 And the sons of Ammon crossed the Jordan, to fight, even against Judah and against Benjamin, and against the house of Ephraim, —so that Israel was sore distressed.
Nao wana wa Amoni wakavuka Yordani, wakapigana na Yuda, na Benyamini, na nyumba ya Efraimu; Israeli akasumbuliwa sana.
10 Then did the sons of Israel make outcry unto Yahweh, saying, —We have sinned against thee, because we have forsaken our God, and have served the Baals.
Ndipo wana wa Israeli wakamwita Bwana, wakisema, “Tumekukosea, kwa sababu tumemwacha Mungu wetu, tukaabudu Mabaali.”
11 Then said Yahweh unto the sons of Israel, —Was it not, from the Egyptians, and from the Amorites, and from the sons of Ammon, and from the Philistines, [that I saved you]?
Bwana akawaambia wana wa Israeli, “Je, sikuwatoa ninyi kutoka kwa Wamisri, na Waamori, na Waamoni, na Wafilisti,
12 The Zidonians also, and the Amalekites, and the Maonites, oppressed you, —and ye made outcry unto me, and I saved you out of their hand.
na pia kwa Wasidoni? Waamaleki na Wamaoni walipowakandamiza; mliniita, nami nikawaokoa kutoka katika nguvu zao.
13 Yet have, ye, forsaken me, and served other gods, —therefore will I not again save you.
Lakini ninyi mliniacha tena na kuabudu miungu mingine. Kwa hiyo, sitawaokoa tena.
14 Go and make outcry unto the gods whom ye have chosen, —they, must save you, in the time of your tribulation.
Nendeni mkaiite miungu mnayoiabudu. Ili iwaokoe wakati wa shida.
15 And the sons of Israel said unto Yahweh—We have sinned, do, thou, with us, according to all that is fitting in thine eyes, —only rescue us, we beseech thee this day.
Wana wa Israeli wakamwambia Bwana, Tumefanya dhambi. Tufanyie chochote kinachoonekana kuwa kizuri kwako. Tafadhali, tuokoe leo.
16 And they put away the gods of the stranger out of their midst, and served Yahweh, —and his soul was impatient of the misery of Israel.
Wakaiacha miungu ya kigeni waliyokuwa nayo, nao wakamwabudu Bwana. Naye akawa na subira juu ya taabu ya Israeli.
17 Now the sons of Ammon were called out, and they encamped in Gilead, —and the sons of Israel assembled themselves together, and encamped in Mizpah.
Ndipo Waamoni wakakusanyika, wakaweka kambi Gileadi. Waisraeli walikutana na kuweka kambi yao huko Mispa.
18 Then said the people, the princes of Gilead, one to another, Who is the man that will begin to fight against the sons of Ammon? he shall become head to all the inhabitants of Gilead.
Viongozi wa watu wa Gileadi wakaambiana, 'Ni nani atakayeanza kupigana na Waamoni? Yeye atakuwa kiongozi juu ya wote wanaoishi Gileadi.

< Judges 10 >