< Joshua 17 >

1 And the lot for the tribe of Manasseh was, for, he, was the firstborn of Joseph, —as for Machir, the firstborn of Manasseh, the father of Gilead, because, he, was a man of war, therefore had he Gilead and Bashan.
Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
2 So the lot pertained to the rest of the sons of Manasseh, by their families, to the sons of Abiezer, and to the sons of Helek, and to the sons of Asriel, and to the sons of Shechem, and to the sons of Hepher, and to the sons of Shemida, —these, were the sons of Manasseh, son of Joseph, even the male descendants, by their families.
Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
3 But, Zelophehad, son of Hepher, son of Gilead, son of Machir, son of Manasseh, had no sons, but only daughters, —and, these, are the names of his daughters, Mahlah and Noah, Hoglah, Milcah, and Tirzah.
Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
4 And they had come near, before Eleazar the priest, and before Joshua son of Nun, and before the princes, saying, Yahweh, commanded Moses, to give us an inheritance in the midst of our brethren, —And he had given them, according to the bidding of Yahweh, an inheritance, in the midst of the brethren of their father.
Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
5 Thus there fell ten portions to Manasseh, —besides the land of Gilead, and Bashan, which is beyond the Jordan;
Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
6 because, the daughters of Manasseh, received an inheritance in the midst of his sons, —and, the land of Gilead, became the possession of the sons of Manasseh that remained.
kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
7 So then the boundary of Manasseh was from Asher, Michmethath, which faceth Shechem, —and the boundary goeth along unto the right hand, unto the inhabitants of En-tappuah.
Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
8 Manasseh, had the land of Tappuah, —but, Tappuah itself, towards the boundary of Manasseh, pertained unto the sons of Ephraim;
(Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
9 and the boundary goeth down to the ravine of Kanah, southward of the ravine, these cities, belong to Ephraim, in the midst of the cities of Manasseh, —but, the boundary of Manasseh, was on the north side of the ravine, and the extensions thereof were to the sea;
Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
10 southward, pertaineth to Ephraim, and, northward, to Manasseh, and the sea was the boundary thereof, —and they touch, Asher, on the north, and Issachar on the east.
Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
11 And Manasseh had—in Issachar and in Asher—Bethshean and her towns, and Ibleam and her towns, and the inhabitants of Dor and her towns, and the inhabitants of En-dor and her towns, and the inhabitants of Taanach and her towns, and the inhabitants of Megiddo, and her towns—the three heights,
Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
12 The sons of Manasseh, however, could not dispossess these cities, —but the Canaanites were determined to remain in this land;
Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
13 but, when the sons of Israel had waxed strong, they put the Canaanites under tribute, —though they, dispossessed, them not.
Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
14 Then spake the sons of Joseph unto Joshua, saying, —Why hast thou given me, as an inheritance, but one lot and one portion, seeing that, I, am a numerous people, because hitherto hath Yahweh blessed me.
Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
15 And Joshua said unto them: If, a numerous people, thou art, get thee up to the forest, and cut down for thyself there, in the land of the Perizzites and of the Rephaim, —seeing that, too narrow for thee, is the hill country of Ephraim.
Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
16 And the sons of Joseph said, The hill country is not enough for us, —and there are, chariots of iron, among all the Canaanites that dwell in the land of the valley, belonging both to them in Bethshean, and her towns, and to them in the valley of Jezreel.
Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
17 And Joshua made answer unto the house of Joseph, to Ephraim and to Manasseh, saying, —A numerous people, thou art, and, great vigour, thou hast, thou shalt not have one lot only;
Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
18 for, the hill country, shall be thine, in that, a forest, it is, therefore canst thou cut it down, and thine shall be the extensions thereof, —for thou shalt dispossess the Canaanites, though, chariots of iron, they have, and though, strong, they are.
bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”

< Joshua 17 >