< John 21 >
1 After these things, Jesus manifested himself again, unto the disciples, by the sea of Tiberias; and manifested himself, thus: —
Baada ya mambo hayo Yesu alijidhihirisha tena kwa wanafunzi katika Bahari ya Tiberia; hivi ndivyo alivyojidhihirisha mwenyewe:
2 There were together, Simon Peter, and Thomas, who was called Didymus, and Nathanael, who was from Cana of Galilee, and the sons of Zebedee, and, two other, of his disciples.
Simon Petro alikuwa pamoja na Thomaso aitwaye Didimas, Nathanaeli wa kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili wa Yesu.
3 Simon Peter saith unto them—I go a fishing! They say unto him—We also, go with thee! They went out, and got up into the boat, and during that night, they caught nothing.
Simon Petro akawaambia, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Sisi, pia tutaenda nawe.” Wakaenda wakaingia kwenye mashua, lakini usiku huo wote hawakupata chochote.
4 But, morning by this time drawing on, Jesus stood upon the beach; nevertheless, the disciples knew not that it was, Jesus.
Na asubuhi kulipokucha, Yesu alisimama ufukweni, nao wanafunzi hawakutambua kuwa alikuwa Yesu.
5 Jesus, therefore, saith unto them—Children! perhaps ye have nothing to eat? They answered him—No.
Kisha Yesu akawambia, “Vijana, mna chochote cha kula?” Nao wakamjibu, “Hapana.”
6 And, he, said unto them—Cast the net, on the right side of the boat, —and ye shall find. They cast, therefore; and, no longer, were they able, to draw, it, for the multitude of the fishes.
Akawambia, “Shusheni wavu upande wa kuume wa mashua, nanyi mtapata kiasi.” Kwa hiyo wakashusha wavu nao hawakuweza kulivuta tena kwa sababu ya wingi wa cha samaki.
7 That disciple, therefore, whom Jesus loved, saith unto Peter—It is, the Lord! Simon Peter, therefore, hearing that it was the Lord, girded about him, his upper garment, —for he was naked; and cast himself into the sea;
Basi yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akamwambia Petro, “Ni Bwana.” Naye Simon Petro aliposikia kuwa ni Bwana, akajifunga vazi lake (maana hakuwa amelivaa vizuri), kisha akajitupa baharini.
8 but, the other disciples, came, by the little boat, —for they were not farther from the land than about two hundred cubits off, —dragging the net of fishes.
Wale wanafunzi wengine wakaja kwenye mashua (kwani hawakuwa mbali na pwani, yapata mita mia moja kutoka ufukweni), nao walikuwa wakivuta zile nyavu zilizokuwa zimejaa samaki.
9 So, when they got out upon the land, they behold a coal fire lying, and fish lying over, and bread.
Walipofika ufukweni, waliona moto wa mkaa pale na juu yake kulikuwa na samaki pamoja na mkate.
10 Jesus saith unto them—Bring of the fish which ye caught just now.
Yesu akawambia, “Leteni baadhi ya samaki mliovua sasa hivi.”
11 Simon Peter, therefore, went on board, and drew the net on to the land, —full of large fishes, a hundred and fifty-three; and, though they were so many, the net was not rent.
Basi Simon Petro akapanda na kuukokota ule wavu uliokuwa umejaa samaki wakubwa, kiasi cha samaki 153; japo walikuwa wengi, ule wavu haukuchanika.
12 Jesus saith unto them—Come! break your fast. Not one, of the disciples was venturing to ask him, Who art, thou? knowing that it was, the Lord.
Yesu akawaambia, “Njoni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanfunzi aliyethubutu kumwuliza, “Wewe ni nani?” Walijua kuwa alikuwa ni Bwana.
13 Jesus cometh, and taketh the bread, and giveth unto them; and the fish, in like manner.
Yesu akaja, akachukua ule mkate, kisha akawapa, akafanya vivyo hivyo na kwa wale samaki.
14 This, already, is the third time Jesus was manifested unto the disciples, after he was raised from among the dead.
Hii ilikuwa mara ya tatu kwa Yesu kujidhihirisha kwa wanafunzi wake baada ya kufufuka toka wafu.
15 When, therefore, they had broken their fast, Jesus saith unto Simon Peter—Simon, son of John! lovest thou me more than these? He saith unto him—Yea, Lord! thou, knowest that I am fond of thee, he saith unto him—Be feeding my lambs.
Baada ya kuwa wamefungua kinywa, Yesu akamwambia Simon Petro, “Simon mwana wa Yohana je, wanipenda mimi kuliko hawa?” Petro akajibu, “Ndiyo, Bwana; “Wewe wajua kuwa mimi nakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wanakondoo wangu.”
16 He saith unto him, again, the second time—Simon, son of John! lovest thou me? He saith unto him—Yea, Lord! thou, knowest that I am fond of thee. He saith unto him—Be shepherding my sheep.
Akamwambia mara ya pili, “Simon mwana wa Yona, je, wanipenda?” Petro akamwambia, “Ndiyo, Bwana; wewe wajua kuwa nakupenda. “Yesu akamwambia, “Chunga kondoo wangu.”
17 He saith unto him, the third time—Simon, son of John! art thou fond of me? Peter was grieved, that he said unto him, the third time, Art thou fond of me? and he said unto him—Lord! all things, thou, knowest: thou perceivest that I am fond of thee. Jesus saith unto him—Be feeding my sheep.
Akamwambia tena mara ya tatu, “Simon, mwana wa Yohana, Je wanipenda?” Naye Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, “Je Wewe wanipenda?” Naye akamwambia, “Bwana, unajua yote; unajua kuwa nakupenda.” Yesu akamwambia, Lisha kondoo wangu.
18 Verily, verily, I say unto thee—When thou wast younger, thou usedst to gird thyself, and to walk whither thou didst choose; but, when thou shalt become aged, thou shalt stretch out thy hands, and, another, shall gird thee, and bear thee, whither thou dost not choose.
Amini, amini, nakuambia, ulipokuwa kijana ulizoea kuvaa nguo mwenyewe na kwenda kokote ulikotaka; lakini utakapokuwa mzee, utanyosha mikono yako, na mwingine atakuvalisha nguo na kukupeleka usikotaka kwenda.”
19 Now, this, he said, signifying, by what manner of death, he should glorify God. And, having said this, he saith unto him—Be following me.
Yesu alisema haya ili kuonesha ni aina gani ya kifo ambacho Petro angemtukuza Mungu. Baada ya kuwa amesema haya, akamwambia Petro, “Nifuate.”
20 Peter, turning about, beholdeth the disciple whom Jesus loved, following, —who also reclined during the supper upon his breast, and said—Lord, who is it that is delivering thee up?
Petro aligeuka na kumwona yule mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda akawafuata- Huyu ndiye aliyekuwa amajiegemeza kwenye kifua cha Yesu wakati wa chakula cha jioni na kumwuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”
21 Peter, therefore, seeing, this one, saith unto Jesus—Lord! and, this one, what?
Petro alimwona na kisha akamwuliza Yesu, “Bwana, Huyu mtu atafanya nini?”
22 Jesus saith unto him—If I will that, he, remain until I come, what is that to thee? Thou, be following me.
Yesu akamjibu, “Kama nataka abaki mpaka nitakapokuja, hilo linakuhusu nini?” Nifuate.”
23 This word, therefore, went forth unto the brethren, that, that disciple, should not die. Howbeit, Jesus did not tell him, he should not die; but, If I will that, he, remain until I come, what is that to thee?
Kwa hiyo habari hii ikaenea miongoni mwa wale ndugu, kwamba mwanafunzi huyo hatakufa. Lakini Yesu hakumwambia Petro kuwa, mwanafunzi huyo hafi, “Kama nataka yeye abaki mpaka nitakapokuja yakuhusu nini?”
24 This, is the disciple who beareth witness concerning these things, and who hath written these things; and we know that, true, is, his witness.
Huyu ndiye mwanafunzi atoaye ushuhuda wa mambo haya, na ndiye aliye andika mambo haya, na tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
25 Now there are many other things also, which Jesus did, which, indeed, if they were to be written one by one, not even the world, itself, I suppose, would contain, the books which must be written.
Kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu aliyafanya. Kama kila moja lingeandikwa, nadhani kwamba ulimwengu wenyewe usingetosha kuviweka vitabu ambavyo vingeandikwa.