< Job 6 >

1 Then responded Job, and said: —
Kisha Ayubu akajibu:
2 Oh that, weighed, were my vexation, and, my engulfing ruin—into the balances, they would lift up all at once!
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 For, now, beyond the sand of the seas, would it be heavy, On this account, my words, have wandered.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For, the arrows of the Almighty, are in me, The heat whereof, my spirit is drinking up, The, terrors of GOD, array themselves against me.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Doth the wild ass bray over grass? Or loweth the ox over his fodder?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 Can that which hath no savour be eaten without salt? Or is there any taste in the white of an egg?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 My soul hath refused to touch, Those things, are like disease in my food.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Oh that my request would come! and, my hope, oh that GOD would grant!
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 That it would please GOD to crush me, That he would set free his hand, and cut me off!
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 So might it still be my comfort, And I might exult in the anguish he would not spare, —That I had not concealed the sayings of the Holy One.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 What is my strength, that I should hope? Or what mine end, that I should prolong my desire?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 Is my strength, the strength of stones? Or is, my flesh, of bronze?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Is there any help at all in me? Is not, abiding success, driven from me?
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 The despairing, from his friend, should have lovingkindness, or, the reverence of the Almighty, he may forsake.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 Mine own brethren, have proved treacherous like a torrent, like a channel of torrents which disappear:
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 Which darken by reason of the cold, over them, is a covering made by the snow:
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 By the time they begin to thaw, they are dried up, as soon as it is warm, they have vanished out of their place.
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 Caravans turn aside by their course, they go up into a waste, and are lost:
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 The caravans of Tema looked about, the travelling companies of Sheba, hoped for them:
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 They are ashamed that they had trusted, They have come up to one of them, and are confounded.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 For, now, ye have come to him, ye see something fearful, and fear.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Is it that I said, Make me a gift, or, out of your abundance, offer a bribe on my behalf;
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 And deliver me from the hand of the adversary? And, out of the hand of tyrants, ransom me?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Show me, and, I, will hold my peace, And, wherein I have erred, cause me to understand.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 How pleasant are the sayings that are right! But what can a decision from you, decide?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 To decide words, do ye intend, When, to the wind, are spoken the sayings of one in despair?
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Surely, the fatherless, ye would assail, and make merchandise of your friend!
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 But, now, be pleased to turn to me, that it may be, to your faces, if I speak falsehood,
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Reply, I pray you, let there be no perversity, Yea reply even yet, my vindication is in it!
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 Is there, in my tongue, perversity? Or can, my sense, not discern, engulfing ruin?
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< Job 6 >