< Job 40 >

1 And Yahweh responded to Job, and said: —
Bwana akamwambia Ayubu:
2 Shall a reprover contend, with the Almighty? He that disputeth with GOD, let him answer it!
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Then Job responded to Yahweh, and said: —
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Lo! I am of no account, what shall I reply to thee? My hand, have I laid on my mouth:
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Once, have I spoken, but I will not proceed, yea twice, but I will not add.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 So then Yahweh responded to Job, out of a storm, and said: —
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Gird, I pray thee—as a strong man—thy loins, I will ask thee, and inform thou me.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 Wilt thou even frustrate my justice? Wilt thou condemn me, that thou mayest appear right?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 But if, an arm like GOD, thou hast, and, with a voice like his, thou canst thunder,
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 Deck thyself, I pray thee, with majesty and grandeur, Yea, with dignity and splendour, thou shalt clothe thyself;
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Pour out thy transports of anger, and look on every one who is high, and lay him low;
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Look on every one who is high, and humble him, yea tread down the lawless, on the spot:
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Hide them in the dust all together, Their faces, bind thou in darkness;
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 And, even I myself, will praise thee, in that thine own right hand can bring thee salvation.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Behold, I pray thee, the Hippopotamus, which I made with thee, Grass—like the ox, he eateth;
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Behold, I pray thee, his strength in his loins, and his force, in the muscles of his belly;
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 He bendeth down his tail like a cedar, the sinews of his thighs, are twisted together;
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 His bones, are barrels of bronze, his frame, is like hammered bars of iron:
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 He, is the beginning of the ways of GOD, Let his maker, present him his sword:
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Surely the mountains bring, produce, to him, where, all the wild beasts of the field, do play;
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Under the lotus-trees, he lieth down, in a covert of reed and swamp;
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 The lotus-trees cover him with their shade, the willows of the torrent-bed compass him about;
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Lo! the river becometh insolent—he is not alarmed! He is confident, though a Jordan burst forth to his mouth:
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Before his eyes, shall he be caught? With a hook, can one pierce his nose?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< Job 40 >