< Job 38 >

1 Then Yahweh responded to Job, out of a storm, and said: —
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 Who is it that darkeneth counsel, by words, without knowledge?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Gird, I pray thee—like a strong man—thy loins, that I may ask thee, and inform thou me:
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 Where wast thou, when I founded the earth? Tell, if thou knowest understanding!
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Who set the measurements thereof, if thou knowest? Or who stretched out over it a line?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 Whereon were the pedestals thereof sunk? Or who laid the corner stone thereof; —
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 When the morning stars sang together, and all the sons of God shouted for joy?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 Or [who] shut in, with double doors, the sea, when, bursting out of the womb, it came forth;
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 When I put a cloud as the garment thereof, and a thick cloud as the swaddling-band thereof;
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 And brake off for it my boundary, and fixed a bar and double doors;
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 And said—Hitherto, shalt thou come, and no further, —and, here, shalt thou set a limit to the majesty of thy waves?
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 Since thy days [began] hast thou commanded the morning? or caused the dawn to know its place;
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 That it might lay hold of the wings of the earth, and the lawless be shaken out of it?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 It transformeth itself like the clay of a seal, so that things stand forth like one arrayed;
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 That their light may be withdrawn from the lawless, and, the lofty arm, be shivered.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 Hast thou entered as far as the springs of the sea? Or, through the secret recesses of the resounding deep, hast thou wandered?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Have the gates of death been disclosed to thee? And, the gates of the death-shade, couldst thou descry?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Hast thou well considered, even the breadths of the earth? Tell—if thou knowest it all!
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 Where then is the way, the light shall abide? And, the darkness, where then is its place?
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 That thou mayest conduct it unto the bound thereof, and that thou mayest perceive the paths to its house.
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Thou knowest, for, then, hadst thou been born! And, in number, thy days are many!
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Hast thou entered into the treasuries of the snow? And, the treasuries of the hail, couldst thou see?
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 Which I have reserved for a time of distress, for the day of conflict and of war?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 Where then is the way the lightning is parted? The east wind spreadeth itself abroad over the earth.
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Who hath cloven—for the torrent—a channel? Or a way for the lightning of thunders;
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 To give rain over the no-man’s land, the desert, where no son of earth is;
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 To satisfy the wild and the wilderness, to cause to spring forth the meadow of young grass?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Hath the rain a father? Or who hath begotten the drops of dew?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 Out of whose womb, came forth the ice? And, the hoar-frost of the heavens, who hath given it birth?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 Like a stone, are the waters congealed, and, the face of the roaring deep, becometh firm!
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 Canst thou bind the fetters of the Pleiades? Or, the bands of Orion, canst thou unloose?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Canst thou bring forth the signs of the Zodiac each in its season? Or, the Bear and her Young, canst thou lead?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Knowest thou, the statutes of the heavens? Or didst thou appoint his dominion over the earth?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 Canst thou lift up, to the thick cloud, thy voice, and the overflow of waters cover thee?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Canst thou send forth the lightnings, so that they go, and say to thee, Behold us?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Who hath put—into cloud-forms—wisdom? Or who hath given—to the meteor—understanding?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Who can count the thin clouds, in wisdom? And, the bottles of the heavens, who can empty out;
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 When the dust is cast into a clod, and the lumps are bound together?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 Wilt thou hunt—for the Lioness—prey? Or, the craving of the Strong Lion, wilt thou satisfy;
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 When they settle down in dens, abide in covert, for lying in wait?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Who prepareth for the Raven his nourishment, —when his young ones—unto GOD—cry out, [when] they wander for lack of food?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >