< Job 37 >

1 Yea, at this, my heart quaketh, and starteth up out of its place.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Hear! oh hear! the raging of his voice, A growling sound also, out of his mouth, goeth forth;
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Under the whole heavens, he letteth it loose, His lightning also, unto the wings of the earth;
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 After it, roareth a voice, He thundereth with his voice of majesty, Nor will he hold them back, when his voice is heard.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 GOD thundereth with his voice, wonderfully, Doing great things, which we cannot know;
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 For, to the snow, he saith, Fall earthwards, —Also to the downpour of rain, yea the downpour of his mighty rains.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 On the hand of every man, he setteth a seal, that all men may take note of his doing.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 So then the wild-beast hath gone into covert, and, in its lairs, doth it remain.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 Out of a chamber cometh a storm-wind, and, out of the north, cold.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 By the breath of GOD, is given—frost, and, the breadth of waters, is congealed;
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Also, with moisture, burdeneth he the thick cloud, He disperseth his lightning-cloud;
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 Yea, the same, in circles, turneth itself to and fro, by his steering them to their work, whithersoever he commandeth them, over the face of the world, towards the earth.
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Whether, as a rod, or for his earth, or in lovingkindness, he causeth it to come.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 Give thou ear unto this, O Job, Stay, and consider well the wonders of GOD: —
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 Canst thou got to know of GOD’S giving charge over them, or of the causing of the lightning of his cloud to shine forth?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 Canst thou get to know concerning the poisings of the thick cloud, the wonders of one who is perfect in knowledge?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 That thy garments should be hot when he quieteth the earth from the south?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 Didst thou spread out, with him, the skies, strong as a molten mirror?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Let us know what we shall say to him, We cannot set in order, by reason of darkness.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 Shall it be declared to him—that I would speak? Were any man to say aught, he might he destroyed?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Yet, now, men see not the light, bright though it is in the skies, when, a wind, hath passed over, and cleansed them.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Out of the north, a golden light cometh, Upon GOD, is fearful splendour:
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 The Almighty, whom we have not fully found out, is great in vigour, —Neither, justice nor abounding righteousness, will he weaken.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Therefore, do men revere him, He will not regard any who are wise in heart.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >