< Job 34 >
1 Furthermore Elihu responded, and said: —
Zaidi ya hayo, Elihu aliendelea kusema:
2 Hear, ye wise men, my words, and, ye who know, give ear unto me;
“Sikilizeni maneno yangu, ninyi watu wenye hekima; nisikieni, ninyi mlio na maarifa.
3 For, the ear, trieth words, as, the palate, tasteth in eating.
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.
4 What is right, let us choose for ourselves, Let us know, among ourselves, what is good;
Na tujichagulie sisi wenyewe yale yenye adili: na tujigundulie miongoni mwetu yale yaliyo mazuri.
5 For Job hath said—I am righteous, But, GOD, hath turned away my right;
Kwa kuwa Ayubu amesema, 'mimi ni mwenye haki, lakini Mungu ameondoa haki zangu.
6 Concerning mine own right, shall I tell a falsehood? Incurable is my disease—not for any transgression.
Pamoja na haki zangu, ninaangaliwa kama mwongo. Kidonda changu hakiponyeki, ingawa mimi sina dhambi.'
7 What man is like Job? He drinketh in scoffing like water;
Ni mtu gani aliye kama Ayubu ambaye hunywa dharau kama maji,
8 And is on the way to keep company, with the workers of iniquity, and to walk with lawless men.
ambaye huzunguka katika ushirika wa watu ambao ni waovu, na ambaye hutembea pamoja na watu waovu?
9 For he hath said, It profiteth not a man, when, his good pleasure, is with God.
Kwa kuwa anasema, ' Hakuna faida kwa mtu kujifurahisha kwa kufanya mambo ambayo Mungu anayataka.'
10 Wherefore, ye men of mind, hearken unto me, —Far be it, that, GOD, should be lawless, or, the Almighty, be perverse!
Basi nisikilizeni mimi, enyi watu wenye ufahamu: na iwe mbali na Mungu kwamba atatenda uovu;
11 For, what any son of earth doeth, he repayeth him, and, according to every man’s course, he causeth him to find.
na iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi. Kwa kuwa humlipa mtu kutokana na kazi yake; na humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe.
12 Nay, verily, GOD, will not condemn unjustly, —nor, the Almighty, pervert justice.
Kwa hakika, Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.
13 Who set him in charge of the earth? Or who appointed [him] the whole world?
Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?
14 If he should set against him his heart, His spirit and his inspiration, unto himself he should withdraw.
Ikiwa aliweka makusudio yake juu yake mwenyewe, na kama amejikusanyia mwenyewe nafsi yake na pumzi yake,
15 All flesh together, would cease to breathe, and, the earth-born, unto dust, would return.
basi miili yote itateketea pamoja; mwanadamu angerudi mavumbini tena.
16 If then [thou hast] understanding, hear this, Give thou ear to the teaching of my words: —
Kama sasa mna ufahamu, sikilizeni haya; sikilizeni sauti ya maneno yangu.
17 Shall, the very hater of right, control? Or, the just—the mighty one, wilt thou condemn?
Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?
18 Doth one say to a king, Abandoned one! Or, Lawless one! unto nobles?
Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?
19 For he hath shewn no respect of persons unto princes, neither hath he recognised the rich rather than the poor? For, the work of his hands, are they all.
Mungu ambaye haoneshi upendeleo kwa viongozi na ambaye hawakubali zaidi watu matajiri kuliko masikini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake.
20 In a moment, they die, even in the middle of the night, —A people are convulsed when they pass away, A mighty one is removed, without hand;
Watakufa kwa muda mfupi; wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita; watu wenye nguvu watatwaliwa mbali, lakini si kwa mikono ya wanadamu.
21 For, his eyes, are on the ways of a man, and, all his footsteps, he beholdeth, —
Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu; anaziona hatua zake zote.
22 No darkness, and no death-shade, where the workers of iniquity may hide.
Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito ambao watenda mabaya wanaweza kujificha wao wenyewe.
23 For, unto no man, doth he appoint a repetition, —in going unto GOD in judgment;
Kwa kuwa Mungu hahitaji kumchunguza mtu zaidi; wala hakuna haja kwa mtu yeyote kwenda mbele zake kwa hukumu.
24 He shattereth mighty ones unsearchably, and setteth up others in their stead:
Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi; huwaweka watu wengine katika nafasi zao.
25 Therefore, he observeth their works, —and overturneth [them] in a night, and they are crushed;
Kwa namna hii ana maarifa juu ya matendo yao; huwatupa watu hawa wakati wa usiku; nao wameangamizwa.
26 In the place of lawless men, hath he chastised them, in presence of beholders.
Huwaua kwa matendo yao mabaya kama wakosaji dhahiri mbele za watu wengine
27 Forasmuch, as they turned from following him, and, none of his ways, did they teach;
kwasababu wamegeuka na kuacha kumfuata yeye na wamekataa kuzisadiki njia zake zozote.
28 Causing to reach him the outcry of the poor, Yea, the outcry of the oppressed, he heareth.
Na kwa namna hii, wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie; amekisikia kilio cha watu walioteswa.
29 When, he, giveth quiet, who then shall condemn? And, when he hideth [his] face, who then shall sing of him? whether unto a nation or unto mankind altogether,
Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua? Anatawala sawa sawa juu ya taifa na mtu pia,
30 That impious men may not reign, nor be ensnarers of the people.
ili kwamba watu wasiomjua Mungu wasije wakatawala, ili kwamba asiwepo mtu wa kuwanasa watu.
31 For, unto GOD, hath one [ever] said—I have borne punishment, I will not be perverse;
Fikiria mtu akimwambia Mungu, ' Mimi ni mwenye hatia kabisa, lakini sitatenda dhambi tena;
32 What I see not, do, thou, shew me, If, perverseness, I have wrought, I will do it no more?
nifunze kile ambacho siwezi kukiona; nimetenda dhambi, lakini sitafanya tena.'
33 According to thy mind, must he requite it, that thou hast refused? For, thou, must choose, and not, I, What then thou knowest, speak!
Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda? Ni lazima uchague, siyo mimi. Basi sema yale ambayo unayajua.
34 The men of mind, will say to me, yea any wise man hearkening unto me: —
Watu wenye ufahamu wataniambia, kwa kweli, kila mtu mwenye hekima ambaye hunisikia atasema,
35 Job, without knowledge, doth speak, and, his words, are not with discretion.
Ayubu anazungumza bila maarifa; maneno yake hayana hekima.'
36 Would that Job might be tested to the uttermost, for replying with the men of iniquity:
Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake kwasababu ya kuongea kwake kama watu waovu.
37 For he addeth—unto his sin—rebellion, In our midst, he clappeth his hands, and multiplieth his sayings against GOD.
Kwa kuwa anaongeza uasi juu ya dhambi yake; anapiga makofi ya dharau kati yetu; anaweka maneno kinyume na Mungu.”