< Job 23 >

1 Then responded Job, and said: —
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Even to-day, is my complaint rebellion? His hand, is heavier than my groaning.
“Hata leo malalamiko yangu ni machungu; maumivu yangu ni mazito kuliko manung'uniko yangu.
3 Oh that I knew where I might find him! I would come even unto his dwelling-place;
Ee, ningejua niwezapokumwona! Ee, kwamba ningeweza kwenda alipo!
4 I would set out, before him, a plea, and, my mouth, would I fill with arguments;
Ningeweka shitaka langu mbele yake na kukijaza kinywa changu hoja.
5 I would note the words wherewith he would respond to me, and would mark what he would say to me.
Ningejua ambavyo angenijibu na kufahamu ambavyo angesema juu yangu.
6 Would he, with fulness of might, contend with me? Nay, surely, he, would give heed to me!
Je angehojiana nami katika ukuu wa nguvu zake? Hapana, angenisikiliza.
7 There an upright man, might reason with him, so should I deliver myself completely from my judge.
Pale mwenye haki angehojiana nami. Kwa njia hii ningeonekana bila hatia kwa mwamzi wangu.
8 Behold! eastward, I go, but he is not there, and, westward, but I perceive him not;
Tazama, naelekea mashariki, lakini hayupo pale, na upande wa magharibi, lakini siwezi kumwona.
9 On the north, where he worketh, but I get no vision, He hideth himself on the south that I cannot see him.
Kaskazini, anapofanya kazi, lakini siwezi kumwona, na kusini, anapojificha hata nisimwone.
10 But, he, knoweth the way that I choose, Having tried me, as gold, I shall come forth.
Lakini anaijua njia ninayoichukua; atakapokuwa amenipima, nitatoka kama dhahabu.
11 Of his steps, my foot taketh hold, His way, have I kept, and not swerved;
Mguu wangu umeunganishwa na hatua zake; nimezitunza njia zake na sijageuka.
12 The command of his lips, and would not go back, and, in my bosom, have I treasured the words of his lips.
Sijaiacha amri ya midomo yake; nimeyatii maneno ya kinywa chake.
13 But, he, is one, and who can turn him? What his soul desired, he hath done.
Lakini yeye ni wa pekee, naniawezaye kumgeuza? Analolitaka, hulitenda.
14 Surely he will accomplish what is decreed for me, and, many such things, hath he in store.
Kwa maana hulitimiza agizo lake kinyume changu; anamipango mingi kwa ajili yangu; ipo mingi kama hiyo.
15 For this cause, from his presence, am I driven in fear, I diligently consider and am kept back from him in dread:
Kwa hiyo, nimetishwa mbele zake; ninapofikiri kumhusu, ninamwogopa.
16 Yea, GOD, hath made timid my heart, and, the Almighty, hath put me in terror.
Kwani Mungu ameudhoofisha moyo wangu; Mwenyezi amenitisha.
17 Because I was not cut off before the darkness, nor, before my face, did the gloom form a shroud.
Si kwa sababu nimeondolewa na giza, wala siyo kwamba giza nene limeufunika uso wangu.

< Job 23 >