< Job 11 >
1 Then responded Zophar the Naamathite, and said: —
Ndipo Sofari Mnaamathi alijibu na kusema,
2 Should, the multitude of words, not be answered? Or should, a man full of talk, be justified?
“Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa? Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?
3 Shall, thy pratings, cause men to hold their peace? When thou hast mocked, shall there be none to put thee to shame?
Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?
4 Since thou hast said, Right is my doctrine, and pure am I in his eyes.
Kwa kuwa wewe unasema kwa Mungu, 'Imani yangu ni safi, Mimi sina waa lolote machoni pako.'
5 But, in very deed, oh that GOD would speak, that he would open his lips with thee:
Lakini, laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;
6 That he would declare to thee the secrets of wisdom, for they are double to that which actually is, —Know then that GOD could bring into forgetfulness for thee, a portion of thine iniquity.
hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima! Kwa kuwa yeye ni mkuu katika ufahamu. Tena tambua huyo Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.
7 The hidden depth of GOD canst thou discover? Or, unto the furthest limit of the Almighty, canst thou attain?
Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?
8 The heights of the heavens, what canst thou do? Depths deeper than hades, what canst thou know? (Sheol )
Upeo uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu; waweza kufahamu nini wewe? (Sheol )
9 Longer than the earth, is the measure thereof, and broader than the sea.
Vipimo vyake ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.
10 If he sweep on, or shut up, or call together, Who then shall hinder him?
kama yeye akipita kati na kumyamazisha mtu yeyote, kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni, tena ni nani anayeweza kumzuia yeye?
11 For, he, knoweth men of falsity, and seeth iniquity, and him that doth not diligently consider.
Kwa maana anawajua watu waongo; wakati anapoona uovu, hawezi yeye kuukumbuka?
12 But, an empty person, will get sense, when, a wild ass’s colt, is born a man!
Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu; wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.
13 If, thou, hast prepared thy heart, and wilt spread forth, unto him, thy hands—
Lakini ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;
14 If, iniquity, be in thy hand, Put it far away, and let there not dwell in thy tents perversity,
ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako, lakini hivyo tena unauweka mbali nawe, na haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.
15 Surely, then, shalt thou lift up thy face free from blemish, and shalt be established, and not fear.
Ndipo kwa hakika ungeinua juu uso wako bila ishara ya aibu; Ni dhahiri, ungethibitika na usingeogopa.
16 For, now, shalt thou forget, sorrow, Like waters passed away, shalt thou remember it.
Wewe ungesahau mateso yako; ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.
17 Above high noon, shall rise life’s continuance, Darkness, like a morning, shall appear,
Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri; japokuwa kulikuwa na giza, litakuwa kama asubuhi.
18 And thou shalt he confident, that there is hope, and, when thou hast searched, securely shalt thou lie down;
Ungekuwa salama kwa sababu kuna tumaini; ni dhahiri, wewe utapata usalama juu yako na utachukua pumziko lako katika usalama.
19 And shalt rest, with none to put thee in terror, —and many shall entreat thy favour.
Pia ungelala chini katika pumziko, na hakuna ambaye angekufanya wewe uogope; hakika wengi wangetafuta upendeleo wako.
20 But, the eyes of the lawless, shall fail, —and, place of refuge, shall have vanished from them, and, their hope, be a breathing out of life.
Lakini macho ya watu waovu yatashindwa; hawatakuwa na njia ya kukimbia; tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.