< Jeremiah 44 >
1 The word which came to Jeremiah, against all the Jews who were dwelling in the land of Egypt, —who were dwelling in Migdol and in Tahpanhes, and in Noph, and in the land of Pathros saying:
Neno hili lilimjia Yeremia kuhusu Wayahudi wote waishio Misri, huko Migdoli, Tahpanhesi na Memfisi, katika nchi ya Pathrosi kusema:
2 Thus, saith Yahweh of hosts, God of Israel, Ye yourselves, saw all the calamity which I brought in upon Jerusalem, and upon all the cities of Judah, —and there they are, a desolation this day, and there is not in them an inhabitant:
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Mliona maangamizi makubwa niliyoyaleta juu ya Yerusalemu na juu ya miji yote ya Yuda. Leo imeachwa ukiwa na magofu
3 because of their wickedness which they committed, provoking me to anger, by going to burn incense, to serve other gods, whom they had not known, they, ye nor your fathers;
kwa sababu ya uovu waliokuwa wameufanya. Walinikasirisha kwa kufukiza uvumba na kwa kuabudu miungu mingine ambayo kamwe wao, wala ninyi, wala baba zenu hawakuifahamu.
4 yet I sent unto you all my servants the prophets, betimes sending them, saying, Do not, I pray you, commit this abominable thing, which I hate!
Tena na tena, niliwatuma watumishi wangu manabii ambao walisema, ‘Msifanye jambo hili la kuchukiza ambalo nalichukia!’
5 but they hearkened not neither inclined their ear, by turning from their wickedness, —so as not to burn incense to other gods.
Lakini hawakusikiliza wala hawakujali, hawakugeuka ili kuuacha uovu wao, wala hawakuacha kufukiza uvumba kwa miungu mingine.
6 Therefore were mine indignation and mine anger poured out, and a fire was kindled in the cities of Judah and in the streets of Jerusalem, —and they became waste and desolate, as at this day.
Kwa hiyo hasira yangu kali ilimwagika, ikawaka dhidi ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu, na kuifanya ukiwa na magofu kama ilivyo leo.
7 Now, therefore, Thus, saith Yahweh God of hosts God of Israel—Wherefore, are ye committing a great wickedness against your own lives, that ye should cut off from you man and woman child and suckling, out of the midst of Judah, —so that there should not be left you a remnant:
“Basi hili ndilo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Kwa nini kujiletea maafa makubwa kama haya juu yenu kwa kujikatilia mbali kutoka Yuda wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, hata kujiacha bila mabaki?
8 in that ye provoke me to anger by the works of your own hands, burning incense to other gods, in the land of Egypt, which ye have been entering to sojourn, —that ye should cut them off from you, and that ye should become a contempt and a reproach among all the nations of the earth?
Kwa nini kuichochea hasira yangu kwa kile ambacho mikono yenu imekitengeneza, mkaifukizia uvumba miungu mingine huko Misri, mahali mlipokuja kuishi? Mtajiangamiza wenyewe na kujifanya kitu cha kulaania na shutumu miongoni mwa mataifa yote duniani.
9 Have ye forgotten the wicked ways of your fathers and the wicked ways of the kings of Judah, and the wicked ways of his wives, and your own wicked ways, and the wicked ways of your own wives, —which they committed in the land of Judah, and in the streets of Jerusalem?
Je, mmesahau uovu uliotendwa na baba zenu, na wafalme na malkia wa Yuda, na uovu uliofanywa na ninyi na wake zenu katika nchi ya Yuda na barabara za Yerusalemu?
10 They have not been crushed, unto this day; neither have they been afraid, neither have they walked in my law, and in my statutes, which I set before you and before your fathers,
Mpaka leo hawajajinyenyekeza au kuonyesha heshima, wala hawajafuata sheria yangu na amri nilizoweka mbele yenu na baba zenu.
11 Therefore, Thus, saith Yahweh of hosts God of Israel, Behold me! setting my face against you for calamity, —even to cut off all Judah;
“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: Mimi nimekusudia kuleta maafa juu yenu, na kuiangamiza Yuda yote.
12 and I will take the remnant of Judah who did set their faces to enter the land of Egypt to sojourn there, and they shall all be consumed, in the land of Egypt, shall they fall by the sword, by famine, shall they be consumed, from the least even unto the greatest, by sword and by famine, shall they die, —so shall they become a curse, and an astonishment, and a contempt and a reproach;
Nitawaondoa mabaki ya Yuda waliokusudia kwenda Misri kukaa humo. Wote wataangamia huko Misri, wataanguka kwa upanga au kufa kwa njaa. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkuu sana, watakufa kwa upanga au njaa. Watakuwa kitu cha kulaania na cha kutisha, cha laumu na shutumu.
13 and I will bring punishment upon them who are dwelling in the land of Egypt, just as I brought punishment upon Jerusalem, —by sword, by famine and by pestilence;
Nitawaadhibu wale waishio Misri kwa upanga, njaa na tauni kama nilivyoiadhibu Yerusalemu.
14 and there shall be neither escape nor survival, unto the remnant of Judah who have been entering, to sojourn there into the land of Egypt, —that they should return to the land of Judah even when they are lifting up their soul to return to dwell there, for none shall return, saving fugitives.
Hakuna hata mmoja wa mabaki ya Yuda ambaye amekwenda kuishi Misri atakayeepuka au kunusurika ili kurudi katika nchi ya Yuda, ambayo wanaitamani sana kurudi na kuishi ndani yake, hakuna hata mmoja atakayerudi isipokuwa wakimbizi wachache.”
15 Then all the men who knew that their wives were burning incense to other gods, and all the women standing by, a great convocation, —with all the people who were dwelling in the land of Egypt in Pathros, made answer unto Jeremiah, saying:
Kisha wanaume wote ambao walijua kwamba wake zao walikuwa wakifukiza uvumba kwa miungu mingine, pamoja na wanawake wote waliokuwako, yaani, kusanyiko kubwa na watu wote walioishi nchi ya Misri na Pathrosi, wakamwambia Yeremia,
16 As touching the word which thou hast spoken unto us, in the name of Yahweh we are not going to hearken unto thee;
“Hatutausikiliza ujumbe uliotuambia katika jina la Bwana!
17 but, we will certainly do, the whole thing that hath gone forth out of our own mouth, by burning incense to the queen of the heavens, and pouring out to her drink-offerings, just as we and our fathers, and our kings and our princes, did, in the cities of Judah and in the streets of Jerusalem, then were we filled with bread and became prosperous, and calamity, saw we none;
Hakika tutafanya kila kitu tulichosema tutakifanya: Tutafukiza uvumba kwa Malkia wa Mbinguni na tutammiminia sadaka zetu za kinywaji kama vile sisi na baba zetu, wafalme wetu na maafisa wetu tulivyofanya katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu. Wakati ule tulikuwa na chakula tele, tulikuwa matajiri wala hatukupata dhara lolote.
18 whereas, from the very time we ceased burning incense to the queen of the heavens and pouring out to her drink-offerings, we have lacked everything, —and by sword and by famine, have we been consumed.
Lakini tangu tulipoacha kumfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka za kinywaji, hatupati chochote, na tumekuwa tukiangamizwa kwa upanga na njaa.”
19 And, though we are burning incense to the queen of the heavens and pouring out to her drink-offerings, is it, without our men that we have made to her sacrificial cakes as images of her and poured out to her, drink-offerings?
Wanawake wakaongeza kusema, “Wakati tulipomfukizia uvumba Malkia wa Mbinguni na kummiminia sadaka zetu za kinywaji, je, waume zetu hawakujua kwamba tulikuwa tukitengeneza maandazi kwa mfano wake, na kummiminia yeye sadaka za kinywaji?”
20 Then spake Jeremiah unto all the people, —against the men and against the women, and against all the people who had been making any answer unto him, saying:
Ndipo Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wanawake waliokuwa wakimjibu,
21 Was it not, the very incense which ye burned in the cities of Judah, and in the streets of Jerusalem, ye and your fathers your kings and your princes and the people of the land, was it not those very things, that Yahweh did remember, and that came up on his heart;
“Je, Bwana hakukumbuka na kufikiri juu ya uvumba uliofukizwa katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu na ninyi pamoja na baba zenu, wafalme wenu, maafisa wenu na watu wa nchi?
22 so that Yahweh could no longer forbear because of the wickedness of your doings, because of the abominations which ye committed, —and your land became a desolation, and an astonishment, and a contempt without inhabitant—as at this day?
Bwana alipokuwa hawezi kuendelea kuvumilia matendo yenu maovu na mambo ya machukizo mliyoyafanya, nchi yenu ilikuwa kitu cha kulaania na kuachwa ukiwa pasipo wakazi, kama ilivyo leo.
23 Because that ye burned incense, and that ye sinned against Yahweh and hearkened not unto the voice of Yahweh, and, in his law and in his statutes and in his testimonies, did not walk, for this cause, did this calamity befall you—as at this day.
Kwa sababu mmefukiza uvumba na kufanya dhambi dhidi ya Bwana, nanyi hamkumtii wala kufuata sheria yake au amri zake au maagizo yake, maafa haya yamekuja juu yenu, kama mnavyoona sasa.”
24 And Jeremiah said unto all the people, and unto all the women, —Hear ye the word of Yahweh, all Judah, who are in the land of Egypt, —
Kisha Yeremia akawaambia watu wote, pamoja na wanawake, “Sikieni neno la Bwana, enyi watu wote wa Yuda mlioko Misri.
25 Thus, saith Yahweh of hosts, God of Israel, saying, Ye and your wives, have both spoken with your mouth and with your hands, have ye fulfilled saying, We will, certainly perform, our vows which we have vowed, to burn incense to the queen of the heavens, and to pour out to her drink-offerings: the women will certainly confirm, your vows, and, certainly perform, your vows.
Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Ninyi na wake zenu mmeonyesha kwa matendo yenu kile mlichoahidi mliposema, ‘Hakika tutatimiza nadhiri tulizoziweka za kumfukizia uvumba na kummiminia sadaka za kinywaji Malkia wa Mbinguni.’ “Endeleeni basi, fanyeni yale mliyoahidi! Timizeni nadhiri zenu!
26 Therefore, hear ye the word of Yahweh, all Judah, who are dwelling in the land of Egypt, —Behold me! I have sworn by my great Name, Saith Yahweh, That my Name shall no more be invoked by the mouth of any man of Judah saying—By the life of My Lord, Yahweh in all the land of Egypt.
Lakini sikieni neno la Bwana, enyi Wayahudi wote mnaoishi Misri: ‘Ninaapa kwa Jina langu lililo kuu,’ asema Bwana, ‘kwamba hakuna hata mmoja atokaye Yuda anayeishi popote Misri ambaye kamwe ataomba tena kwa Jina langu au kuapa, akisema, “Hakika kama Bwana Mwenyezi aishivyo.”
27 Behold me! watching over them for calamity, and not for blessing, —so shall all the men of Judah who are in the land of Egypt, be consumed, by sword and by famine until there be an end of them.
Kwa maana ninawaangalia kwa ajili ya madhara, wala sio kwa mema. Wayahudi walioko Misri wataangamia kwa upanga na njaa, hadi wote watakapoangamizwa.
28 Yet, the fugitives of the sword, shall certainly return out of the land of Egypt into the land of Judah men easily counted, —that all the remnant of Judah who are entering Egypt to sojourn there, may know, whose word, shall stand, mine or theirs!
Wale watakaonusurika upanga na kurudi katika nchi ya Yuda kutoka Misri watakuwa wachache sana. Ndipo mabaki wote wa Yuda waliokuja kuishi Misri watakapojua ni neno la nani litakalosimama, kwamba ni langu au lao.
29 And, this, to you, shall be the sign, Declareth Yahweh, that I am about to bring punishment upon you in this place, —that ye may know that my words shall, certainly stand against you, for calamity:
“‘Hii itakuwa ndiyo ishara kwenu kwamba nitawaadhibu mahali hapa, asema Bwana, ili mpate kujua kuwa onyo langu la madhara dhidi yenu hakika litatimizwa.’
30 Thus, saith Yahweh, Behold me! delivering up Pharaoh-hophra king of Egypt into the hand of his enemies, yea into the hand of them who are seeking his life, —just as I delivered Zedekiah king of Judah into the hand of Nebuchadrezzar king of Babylon his enemy, and one seeking his life.
Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Nitamtia Farao Hofra mfalme wa Misri mikononi mwa adui zake wanaoutafuta uhai wake, kama vile nilivyomtia Sedekia mfalme wa Yuda mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, adui aliyekuwa akiutafuta uhai wake.’”