< Jeremiah 33 >

1 And the word of Yahweh came unto Jeremiah, the second time, when he was yet imprisoned in the guard-court, saying:
Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema:
2 Thus, saith Yahweh, who doeth it, —Yahweh, who fashioneth it to establish it, Yahweh, is his name:
“Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake:
3 Call unto me that I may answer thee, —and tell thee things great and inaccessible, which thou hast not known.
‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’
4 For, Thus, saith Yahweh God of Israel, Concerning the houses of this city, and concerning the houses of the kings of Judah, —which are thrown down against the earthworks and against the sword:
Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga
5 In entering to fight with the Chaldeans, it is to fill them with the dead bodies of men, whom I have smitten in mine anger and in mine indignation, —and because of whom I have hidden my face from this city, —by reason of all their wickedness.
katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.
6 Behold me! laying upon her a bandage of healing, so will I heal them, —And will reveal to them abundance of prosperity and truth;
“‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama.
7 And I will bring back Them of the captivity of Judah, and Them of the captivity of Israel, —And I will build them, as at the first;
Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali.
8 And I will purify them, from all their iniquity wherewith they have sinned against me, —And I will grant pardon for all their iniquities Wherewith they have sinned against me, and Wherewith they have transgressed against me;
Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu.
9 So shall she become to me—A name of joy, A praise and An adorning, To all the nations of the earth, —Who will hear all the good which I am doing them, And will dread and be deeply moved over all the good and over all the prosperity which I am causing her.
Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’
10 Thus, saith Yahweh—Again, shall be heard in this place, as to which ye are saying, Deserted, it is without man or beast, In the cities of Judah and in the streets of Jerusalem, Which are desolate without man or inhabitant or beast
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine
11 The voice of joy, and the voice of gladness The voice of the bridegroom and the voice of the bride, The voice of them who are saying, Praise ye Yahweh of hosts, For good is Yahweh For age-abiding is his lovingkindness, The voice of them who are bringing a thank-offering into the house of Yahweh, —For I will bring back the captives of the land, as at the first, Saith Yahweh.
sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema, “‘“Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote, kwa maana Bwana ni mwema; upendo wake wadumu milele.” Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.
12 Thus, saith Yahweh of hosts, Again, shall there be in this place—Which is deserted without man or even beast—And all the cities thereof, —The home of shepherds, causing flocks to lie down.
“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo.
13 In the cities of the hill country, In the cities of the lowland, and In the cities of the South, and In the land of Benjamin, and In the places round about Jerusalem, and In the cities of Judah, Again shall the flock pass over the hands of the numberer, Saith Yahweh.
Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.
14 Lo! days are coming, Declareth Yahweh, —when I will establish my good word, which I have spoken—As to the house of Israel And concerning the house of Judah:
“‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.
15 In those days and at that time, will I cause to bud unto David A Bud of righteousness, —And he shall execute justice and righteousness in the land:
“‘Katika siku hizo na wakati huo nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi, naye atafanya lile lililo haki na sawa katika nchi.
16 In those days, Judah shall be saved, and, Jerusalem abide, securely, —And, this, is that which shall be proclaimed to her—Yahweh, our righteousness!
Katika siku hizo, Yuda ataokolewa na Yerusalemu ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.’
17 For, Thus, saith Yahweh, —There shall not be wanting to David—A man to sit upon the throne of the house of Israel;
Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli,
18 Nor to the priests the Levites, shall there be wanting—A man, before me, To offer an ascending-sacrifice, or To make a perfume with a gift, or To offer a [peace-] offering, all the days!
wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’”
19 And the word of Yahweh came unto Jeremiah saying:
Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
20 Thus, saith Yahweh, If ye can break, My covenant of the day, and My covenant of the night, That there be not day and night in their season,
“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake,
21 My covenant also, may be broken With David my servant, that he shall not have a son, to reign upon his throne, —And with the Levites the priests, mine attendants:
basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi.
22 As, the host of the heavens, cannot be recorded, Nor the sand of the sea, be measured, So, will I multiply, The seed of David my servant, And the Levites who attend upon me.
Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’”
23 And the word of Yahweh came unto Jeremiah, saying:
Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema:
24 Hast thou not observed what, this people, have spoken saying, The two families which Yahweh did choose, he hath even cast them off? And so, my people, they despise, as though they could not again become a nation in their sight!
“Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa.
25 Thus, saith Yahweh, If my covenant of day and night, the ordinances of the heavens and the earth, I did not appoint,
Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi,
26 The seed of Jacob also and of David my servant, might I cast off so as not to take of his seed as rulers unto the seed of Abraham, Isaac and Jacob, —For I will bring back them of their captivity, and will have compassion upon them.
basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’”

< Jeremiah 33 >