< Jeremiah 30 >

1 The word which came unto Jeremiah, from Yahweh, saying: —
Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Bwana:
2 Thus, speaketh Yahweh, God of Israel, saying, —Write thee all the words which I have spoken unto thee in a scroll;
“Hili ndilo asemalo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Andika katika kitabu maneno yote niliyonena na wewe.
3 For lo! days are coming, Declareth Yahweh, when I will turn the captivity of my people Israel and Judah, Saith Yahweh, —and will bring them back into the land which I gave to their fathers that they might possess it.
Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘nitakapowaleta watu wangu Israeli na Yuda kutoka uhamishoni, na kuwarudisha katika nchi niliyowapa baba zao ili kuimiliki,’ asema Bwana.”
4 Now, these, are the words which Yahweh hath spoken against Israel and against Judah:
Haya ndiyo maneno Bwana aliyoyanena kuhusu Israeli na Yuda:
5 Yea, thus, saith Yahweh, A voice of trembling, have we heard, Dread and not welfare!
“Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Vilio vya woga vinasikika: hofu kuu, wala si amani.
6 Ask, I pray you, and see, whether a male travaileth with child! Why have I seen Every man with his hands upon his loins like a woman in travail, and Every face turned into ghastliness?
Ulizeni na mkaone: Je, mwanaume aweza kuzaa watoto? Kwa nini basi ninaona kila mwanaume mwenye nguvu ameweka mikono yake tumboni kama mwanamke aliye na utungu wa kuzaa, kila uso ukigeuka rangi kabisa?
7 Alas! for, great, is that day, so that none is like it, —Yea, a time of anguish it is for Jacob, But out of it, shall he be saved.
Tazama jinsi ile siku itakavyokuwa ya kutisha! Hakutakuwa na nyingine mfano wake. Utakuwa wakati wa dhiki kwa Yakobo, lakini ataokolewa kutoka hiyo.
8 And it shall come to pass in that day, Declareth Yahweh of hosts, That I will break his yoke from off thy neck, And thy bonds, will I tear off, —And foreigners shall use him as a slave no more;
“‘Katika siku ile,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nitaivunja nira kutoka shingoni mwao na kuvipasua vifungo vyao; wageni hawatawafanya tena watumwa.
9 But they shall serve Yahweh their God, —and David their king, whom I will raise up unto them.
Badala yake, watamtumikia Bwana, Mungu wao na Daudi mfalme wao, nitakayemwinua kwa ajili yao.
10 Thou therefore do not fear O my Servant Jacob Urgeth Yahweh, Neither be thou dismayed, O Israel, For behold me! saving thee from afar And thy seed out of the land of their captivity, —Then shall Jacob return, and rest and be quiet, And there shall be none to make him afraid;
“‘Hivyo usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu, usifadhaike, ee Israeli,’ asema Bwana. ‘Hakika, nitakuokoa kutoka mbali, wazao wako kutoka nchi ya uhamisho wao. Yakobo atakuwa tena na amani na usalama, wala hakuna atakayemtia hofu.
11 For with thee, am, I, Declareth Yahweh To save thee, —Though I make an end of all the nations whither I have scattered thee, Yet will I not of thee, make an end, But will chastise thee in measure, not holding thee, guiltless!
Mimi niko pamoja nawe, nami nitakuokoa,’ asema Bwana. ‘Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote ambamo miongoni mwao nimewatawanya, sitawaangamiza ninyi kabisa. Nitawaadhibu, lakini kwa haki. Sitawaacha kabisa bila adhabu.’
12 For Thus, saith Yahweh—incurable is thine injury, —Grievous is thy wound:
“Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Kidonda chako hakina dawa, jeraha lako haliponyeki.
13 There is none to plead thy cause for binding thee up, —Healing bandages, hast thou none:
Hakuna yeyote wa kukutetea shauri lako, hakuna dawa ya kidonda chako, wewe hutapona.
14 All thy lovers, have forgotten thee, Thyself, do they not seek, —For With the wounding of an enemy, have I wounded thee With the correction of one who is cruel, Because of the abounding of thine iniquity, Because numerous have been thy sins.
Wale walioungana nawe wote wamekusahau, hawajali chochote kukuhusu wewe. Nimekupiga kama vile adui angelifanya, na kukuadhibu kama vile mtu mkatili angelifanya, kwa sababu hatia yako ni kubwa mno na dhambi zako ni nyingi sana.
15 Why shouldst thou make outcry over thine injury, Incurable is thy pain? Because of the abounding of thine iniquity, [Because] numerous have been thy sins Have I done these things unto thee.
Kwa nini unalia kwa ajili ya jeraha lako, yale maumivu yako yasiyoponyeka? Kwa sababu ya uovu wako mkubwa na dhambi zako nyingi nimekufanyia mambo haya.
16 Therefore, all who devour thee, shall be devoured, And, all thine adversaries—all of them, into captivity, shall depart, —So shall they who plundered thee, be plundered, And all who preyed upon thee, will I deliver up as a prey.
“‘Lakini watu wote wakuangamizao wataangamizwa; adui zako wote watakwenda uhamishoni. Wale wote wakutekao nyara watatekwa nyara; wote wakufanyao mateka nitawafanya mateka.
17 For I will put a bandage upon thee, And from thy wounds, will I heal thee Declareth Yahweh, —Because An outcast, they called thee, ‘Tis, Zion! who hath none to ask for her welfare,
Lakini nitakurudishia afya yako na kuyaponya majeraha yako,’ asema Bwana, ‘kwa sababu umeitwa mwenye kutupwa, Sayuni ambaye hakuna yeyote anayekujali.’
18 Thus, saith Yahweh—Behold me! bringing back the captivity of the tents of Jacob, And on his habitations, will I have compassion, —So shall the city be built, upon her own mound, And the citadel, upon its own site, shall remain:
“Hili ndilo asemalo Bwana: “‘Nitarudisha baraka za mahema ya Yakobo, na kuhurumia maskani yake. Mji utajengwa tena juu ya magofu yake, nalo jumba la kifalme litasimama mahali pake halisi.
19 So shall there proceed from them thanksgiving, and The sound of them who make merry, —And I will multiply them, and they shall not become few, And will make them honourable, and they shall not be despised:
Nyimbo za kushukuru zitatoka kwao na sauti ya furaha. Nitaiongeza idadi yao wala hawatapungua, nitawapa heshima na hawatadharauliwa.
20 And, his sons, shall come to be as aforetime, And, his assembly, before me, shall continue, —And I will bring punishment on all his oppressors;
Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa siku za zamani, nayo jumuiya yao itaimarishwa mbele yangu; nitawaadhibu wale wote wawaoneao.
21 And, his illustrious one, shall spring, from himself, And his ruler, from his own midst, shall proceed, And I will bring him near and he shall approach unto me, —For who is there that hath pledged his own heart to approach unto me? Demandeth Yahweh:
Mmoja wao atakuwa kiongozi wao; mtawala wao atainuka miongoni mwao. Nitamleta karibu nami, naye atanikaribia mimi, kwa maana ni nani yule atakayejitolea kuwa karibu nami?’ asema Bwana.
22 So shall ye become my people; And, I, will become your God.
‘Kwa hiyo ninyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.’”
23 Lo! the tempest of Yahweh! Indignation, hath come forth, A tempest rolling itself upward, —Upon the head of the lawless ones, shall it hurl itself down!
Tazama, tufani ya Bwana italipuka kwa ghadhabu, upepo wa kisulisuli uendao kasi utashuka juu ya vichwa vya waovu.
24 The fierceness of the anger of Yahweh will not turn back, Until he hath executed nor Until he hath established The purposes of his heart, —In the afterpart of the days, shall ye understand it.
Hasira kali ya Bwana haitarudi nyuma mpaka atakapotimiza makusudi yote ya moyo wake. Siku zijazo mtayaelewa haya.

< Jeremiah 30 >