< Jeremiah 16 >
1 And the word of Yahweh came unto me saying:
Kisha neno la Bwana likanijia:
2 Thou shall not take to thee a wife, —Neither shalt thou have sons or daughters, in this place.
“Kamwe usioe na kuwa na wana wala binti mahali hapa.”
3 For, Thus, saith Yahweh, Concerning the sons and concerning the daughters that are being born in this place, —and concerning their mothers who do bear them, and concerning their fathers who do beget them, in this land,
Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana kuhusu wana na binti wazaliwao katika nchi hii, na kuhusu wale wanawake ambao ni mama zao, na wale wanaume ambao ni baba zao:
4 Of deaths from diseases, shall they die, They shall not be lamented, Neither shall they be buried, As heaps of dung on the face of the ground, shall they serve, —Yea by sword and by famine, shall they be consumed, And, their dead bodies shall become, food—To the bird of the heavens, and To the beast of the earth.
“Watakufa kwa magonjwa ya kufisha. Hawataombolezewa wala kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyosambaa juu ya ardhi. Watakufa kwa upanga na kwa njaa, nazo maiti zao zitakuwa chakula cha ndege wa angani, na cha wanyama wa nchi.”
5 For, Thus, saith Yahweh—Do not thou enter into the house of crying, Neither do thou go to lament, nor do thou bemoan for them, —For I have withdrawn my blessing from this people, Declareth Yahweh, Both lovingkindness and compassion.
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Usiingie katika nyumba ambayo kuna chakula cha matanga, usiende kuwaombolezea wala kuwahurumia, kwa sababu nimeziondoa baraka zangu, upendo wangu na huruma zangu kutoka kwa watu hawa,” asema Bwana.
6 So shall great and small die in this land, They shall not be buried, —Neither shall men lament for them Nor cut themselves, Nor make themselves bald for them;
“Wakubwa na wadogo watakufa katika nchi hii. Hawatazikwa wala kuombolezewa, na hakuna atakayejikatakata au kunyoa nywele za kichwa chake kwa ajili yao.
7 Neither shall they break bread to them in mourning To console one over his dead, —Nor cause them to drink the cup of consolation, Over one’s father Or over one’s mother;
Hakuna yeyote atakayewapa chakula ili kuwafariji wale waombolezao kwa ajili ya wale waliokufa, hata akiwa amefiwa na baba au mama, wala hakuna yeyote atakayewapa kinywaji ili kuwafariji.
8 And the house of banqueting, shall thou not enter To sit with them, To eat and to drink.
“Usiingie katika nyumba ambayo kuna karamu, na kuketi humo ili kula na kunywa.
9 For, Thus, saith Yahweh of hosts, God of Israel, Behold me! causing to cease out of this place, Before your eyes, And in your days, The voice of joy, and the voice of gladness, The voice of the bridegroom and the voice of the bride,
Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote, aliye Mungu wa Israeli: ‘Mbele ya macho yako na katika siku zako, nitakomesha sauti zote za shangwe na za furaha, na pia sauti za bibi arusi na bwana arusi mahali hapa.’
10 And it shall be when thou shalt declare to this people, all these words, —and they shall say unto thee—For what reason, hath Yahweh pronounced against us all this great calamity? Or what is our iniquity, or what our sin, which we have sinned against Yahweh our God?
“Utakapowaambia watu hawa mambo haya yote na wakakuuliza, ‘Kwa nini Bwana ameamuru maafa makubwa kama haya dhidi yetu? Tumefanya kosa gani? Tumetenda dhambi gani dhidi ya Bwana, Mungu wetu?’
11 Then shalt thou say unto them, —For that your fathers forsook, me, Declareth Yahweh, And walked after other gods, and served them, and bowed down to them, —Whereas me, they forsook And my law, kept they not;
Basi waambie, ‘Ni kwa sababu baba zenu waliniacha mimi, wakafuata miungu mingine ili kuitumikia na kuiabudu. Waliniacha mimi na hawakuishika sheria yangu,’ asema Bwana.
12 And, ye, have done more wickedly than your fathers, —for look at you! walking every man after the stubbornness of his wicked heart, so as not to hearken unto me,
‘Lakini ninyi mmetenda uovu zaidi kuliko baba zenu. Tazama jinsi ambavyo kila mmoja wenu anafuata ukaidi wa moyo wake mbaya, badala ya kunitii mimi.
13 Therefore will I hurl you forth, from off this land, unto a land which ye have not known, ye, nor your fathers, —and ye can serve there other gods day and night, in that I will grant you no favour.
Kwa hiyo nitawaondoa katika nchi hii na kuwatupa katika nchi ambayo ninyi wala baba zenu hamkuijua, nako huko mtaitumikia miungu mingine usiku na mchana, kwa maana sitawapa fadhili zangu huko.’
14 Therefore lo! days are coming, Declareth Yahweh, When it shall be said no more By the life of Yahweh, who brought up the sons of Israel out of the land of Egypt; but—
“Hata hivyo, siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
15 By the life of Yahweh, who hath brought up the sons of Israel out of the land of the North, and out of all the lands whither he had driven them, —So will I bring them back upon their own soil, which I gave to their fathers.
bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wana wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia.’ Maana nitawarudisha katika nchi niliyowapa baba zao.
16 Behold me! sending for many fishers Declareth Yahweh, And they shall catch them, —and thereafter will I send for many hunters, and they shall hunt them from off every mountain and from off every hill, and out of the clefts of the crags.
“Lakini sasa nitawaagiza wavuvi wengi,” asema Bwana, “nao watawavua. Baada ya hilo, nitawaagizia wawindaji wengi, nao watawawinda kwenye kila mlima na kilima, na katika nyufa za miamba.
17 For mine own eyes are upon all their ways, they have not been hid from my face—neither hath their iniquity been concealed from being straight before mine eyes.
Macho yangu yanaziona njia zao zote, hazikufichika kwangu, wala dhambi yao haikusitirika.
18 Thus will I recompense, first, twofold, their iniquity and their sin, because of their profaning my land, —with the carcase of their disgusting and detestable things, have they filled mine inheritance.
Nitawalipiza maradufu kwa ajili ya uovu wao na dhambi yao, kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa maumbo yasiyo na uhai ya vinyago vyao vibaya, na kuujaza urithi wangu na sanamu za kuchukiza.”
19 O Yahweh, my strength, and my refuge, and my place to fly to, in the day of distress, —Unto thee, shall nations come in, out of the ends of the earth, that they may say—Surely! Falsehood, did our fathers inherit, Vanity, among whom is none that can profit:
Ee Bwana, nguvu zangu na ngome yangu, kimbilio langu wakati wa taabu, kwako mataifa yatakujia kutoka miisho ya dunia na kusema, “Baba zetu hawakuwa na chochote zaidi ya miungu ya uongo, sanamu zisizofaa kitu ambazo hazikuwafaidia lolote.
20 Shall a son of earth, make for himself gods, Seeing that, they, are no-gods?
Je, watu hujitengenezea miungu yao wenyewe? Naam, lakini hao si miungu!”
21 Therefore behold me! causing them to know, by this stroke, I will cause them to know my hand and my might, —That they may know that my name, is Yahweh!
“Kwa hiyo nitawafundisha: wakati huu nitawafundisha nguvu zangu na uwezo wangu. Ndipo watakapojua kuwa Jina langu ndimi Bwana.