< Isaiah 63 >
1 Who is this coming in from Edom With bright-red garments, from Bozrah? This made splendid in his raiment, Marching on in the greatness of his strength? I, speaking in righteousness, Mighty to save.
Ni nani huyu anayekuja kutoka Edomu, kutoka Bosra, mwenye mavazi yaliyotiwa madoa mekundu? Ni nani huyu, aliyevikwa joho la kifahari, anayetembea kwa ukuu wa nguvu zake? “Mimi ndimi, nisemaye katika haki, mwenye nguvu wa kuokoa.”
2 Wherefore is there red, on thy raiment, —And thy garments as of one treading in a wine-trough?
Kwa nini mavazi yako ni mekundu, kama ya yule akanyagaye shinikizo la zabibu?
3 A winepress, have I trodden, alone, And of the peoples, there was no man with me. So I trod them down in mine anger, And trampled upon them, in mine indignation, —And their life-blood besprinkled my garments, And all mine apparel, I defiled;
“Nimekanyaga shinikizo la zabibu peke yangu; kutoka mataifa hakuna mtu aliyekuwa pamoja nami. Nimewaponda kwa miguu katika hasira yangu na kuwakanyaga chini katika ghadhabu yangu; damu yao ilitia matone kwenye mavazi yangu, na kutia madoa nguo zangu zote.
4 For, a day of avenging, was in my heart, And the year of my redeemed, had come.
Kwa kuwa siku ya kisasi ilikuwa moyoni mwangu, mwaka wa ukombozi wangu umefika.
5 Therefore looked I around, and there was none to help, —And I was astonished that there was none to uphold, —So, mine own arm brought me salvation, And mine indignation, the same upheld me;
Nilitazama, lakini hakuwepo yeyote wa kunisaidia, nilishangaa kwa kuwa hakuwepo yeyote aliyetoa msaada; hivyo mkono wangu wenyewe ndio ulionifanyia wokovu, na ghadhabu yangu mwenyewe ndiyo iliyonitegemeza.
6 Then trod I down peoples in mine anger, And make them drunk with mine indignation, And brought down to the earth their life-blood.
Nilikanyaga mataifa kwa miguu katika hasira yangu, katika ghadhabu yangu niliwalewesha, na kumwaga damu yao juu ya ardhi.”
7 The lovingkindness of Yahweh, will I recall the praises of Yahweh, According to all that Yahweh hath bestowed upon us, —Even the abundance of goodness to the house of Israel, Which he bestowed upon them—According to his compassions and According to the abundance of his lovingkindness.
Nitasimulia juu ya wema wa Bwana, kwa matendo ambayo apaswa kusifiwa, sawasawa na yote ambayo Bwana ametenda kwa ajili yetu: naam, mambo mengi mema aliyoyatenda kwa ajili ya nyumba ya Israeli, sawasawa na huruma zake na wema wake mwingi.
8 Therefore he said—Surely my people, they are, Sons, they will not act falsely! So he became their saviour.
Alisema, “Hakika wao ni watu wangu, wana ambao hawatanidanganya”; hivyo akawa Mwokozi wao.
9 In all their affliction, he, was afflicted And the messenger of his presence saved them, In his love and in his pity, he, redeemed them, —And then lifted them up and carried them all the days of the age-past time.
Katika taabu zao zote naye alitaabika, na malaika wa uso wake akawaokoa. Katika upendo wake na rehema zake aliwakomboa, akawainua na kuwachukua siku zote zilizopita.
10 But, they, rebelled, and grieved his Holy Spirit, —And so he turned against them as an enemy, he himself, fought against them.
Lakini waliasi, na kumhuzunisha Roho Mtakatifu wake. Hivyo aligeuka na kuwa adui yao, na yeye mwenyewe akapigana dhidi yao.
11 Then were recalled the days of the age-past time Moses—his people: —Where is he that led them up out of the sea with the shepherds of his flock? Where is he that put within him his Holy Spirit?
Ndipo watu wake wakazikumbuka siku zilizopita, siku za Mose na watu wake: yuko wapi yeye aliyewaleta kupitia katikati ya bahari, pamoja na wachungaji wa kundi lake? Yuko wapi yule aliyeweka Roho wake Mtakatifu katikati yao,
12 That caused to go at the right hand of Moses his own majestic arm, —Cleaving the waters from before them, To make himself an age-abiding name:
aliyetuma mkono wake uliotukuka wenye nguvu kuwa katika mkono wa kuume wa Mose, aliyegawa maji ya bahari mbele yao, ili kujipatia jina milele,
13 Causing them to go through the roaring deeps, —Like a horse through the wilderness, That they should not stumble?
aliyewaongoza kupitia kwenye vilindi? Kama farasi katika nchi iliyo wazi, wao hawakujikwaa,
14 As a beast, into the valley, goeth down, The Spirit of Yahweh, causeth him to rest, So, didst thou lead thy people, To make thyself a majestic name!
kama ngʼombe washukao bondeni kwenye malisho, walipewa pumziko na Roho wa Bwana. Hivi ndivyo ulivyowaongoza watu wako ili kujipatia mwenyewe jina tukufu.
15 Look thou down, out of the heavens and see, Out of the high abode of thy holiness and of thy majesty, —Where are thy jealousy, and thy mighty deeds? The resounding of thy yearning affection, and thy compassions towards me, are they restrained?
Tazama chini kutoka mbinguni ukaone kutoka kiti chako cha enzi kilichoinuliwa juu, kitakatifu na kitukufu. Uko wapi wivu wako na uweza wako? Umetuzuilia wema wako na huruma zako.
16 For, thou, art our father, Though, Abraham, knew us not, And Israel could not acknowledge us, —Thou, O Yahweh, art our father, Our Redeemer from the Age-past time, is thy name.
Lakini wewe ni Baba yetu, ingawa Abrahamu hatufahamu sisi wala Israeli hatutambui; wewe, Ee Bwana, ndiwe Baba yetu, Mkombozi wetu tangu zamani za kale ndilo jina lako.
17 Wherefore shouldst thou suffer us to wander O Yahweh, from thy ways? Wherefore shouldst thou let us harden our heart past revering thee? Return thou for the sake of Thy servants, The tribes thou thyself hast inherited.
Ee Bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako, na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu? Rudi kwa ajili ya watumishi wako, yale makabila ambayo ni urithi wako.
18 For a short time only, did thy holy people hold possession, —Our adversaries, trod down thy sanctuary!
Kwa maana kwa muda mfupi watu wako walimiliki mahali pako patakatifu, lakini sasa adui zetu wamepakanyaga mahali patakatifu pako.
19 We have become like those Over whom from age-past times, thou hast not ruled, Who have never been called by thy name!
Sisi tumekuwa kama wale ambao hujawatawala kamwe, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako.