< Hebrews 2 >
1 For this cause, it behoveth us, with unwonted firmness, to be holding fast unto the things that have been heard, lest, at any time, we drift away.
Kwa hiyo ni lazima tuweke kipaumbele zaidi kwa yale tuliyosikia, ili kwamba tusije tukatengwa mbali nayo.
2 For, if the word through messengers spoken became firm, and, every transgression and disobedience received a just recompense,
Kwa maana ikiwa ujumbe uliozungumzwa na malaika ni halali, na kila kosa na uasi hupokea adhabu tu,
3 how shall, we, escape, if, so great a salvation as this, we have neglected, —which, indeed, having received, a beginning, of being spoken through the Lord, by them who heard, unto us was confirmed,
tutapataje kuepuka kama tusipojali wokovu huu mkuu? —wokuvu ambao kwanza ulitangazwa na Bwana na kuthibitishwa kwetu na wale waliousikia.
4 God, jointly witnessing also, both with signs and wonders and manifold mighty works, and with distributions of Holy Spirit, according to his own will?
Mungu pia aliuthibitisha kwa ishara, maajabu, na kwa matendo makuu mbalimbali, na kwa zawadi za Roho Mtakatifu alizozigawa kulingana na mapenzi yake mwenyewe.
5 For, not unto messengers, hath he subjected the coming habitable earth of which we are speaking;
Mungu hakuuweka ulimwengu ujao, ambao tunaongelea habari zake, chini ya malaika.
6 But one somewhere hath borne witness, saying—What is man, that thou shouldst make mention of him? Or the son of man, that thou shouldst put him in charge?
Badala yake, mtu fulani ameshuhudia mahali fulani akisema, “Mtu ni nani, hata uweze kumkumbuka? Au mwana wa mtu, hata umtunze?
7 Thou hast made him less, some little, than messengers, With glory and honour, hast thou crowned him, —[And hast set him over the works of thy hands];
mtu kuwa mdogo kuliko malaika; umemvika taji ya utukufu na heshima. (Zingatia: Katika nakala halisi za kwanza, mstari huu haupo. “Na umemuweka juu ya kazi ya mikono yako.)
8 All things, hast thou subjected beneath his feet. For, in subjecting, [to him] the all things, nothing, left he, to him unsubjected; But now, not yet, do we see, to him, the all things subjected; —
Umeweka kila kitu chini ya miguu yake.” Kwa hiyo Mungu ameweka kila kitu chini ya mtu. Hakuacha kitu chochote ambacho hakiko chini yake. Lakini sasa hivi hatuoni bado kila kitu kikiwa chini yake.
9 But, Jesus, made some little less than messengers, we do behold: by reason of the suffering of death, crowned with glory and honour, to the end that, by favour of God, in behalf of every one, he might taste of death.
Hata hivyo, tunaona ambaye alikuwa amefanywa kwa muda, chini kuliko malaika—Yesu, ambaye, kwa sababu ya mateso yake na kifo chake, amevikwa taji ya utukufu na heshima. Hivyo sasa kwa neema ya Mungu, Yesu ameonja kifo kwa ajili ya kila mtu.
10 For it was becoming in him—For the sake of whom are the all things, and by means of whom are the all things, —when, many sons, unto glory, he would lead, The Princely Leader of their salvation, through sufferings, to make perfect.
Ilikuwa sahihi kwamba Mungu, kwa sababu kila kitu kipo kwa ajili yake na kupitia yeye, alipaswa kuwaleta watoto wengi katika utukufu, na kwamba alipaswa kumfanya kiongozi katika wokovu wao kuwa mkamilifu kupitia mateso yake.
11 For, both he that maketh holy, and they who are being made holy, are, all, of One; For which cause, he is not ashamed to be calling them, brethren,
Kwa maana wote wawili yule anayeweka wakfu na wale ambao wanawekwa wakfu, wote wanatoka kwenye asili moja, Mungu. Kwa sababu hii yule anayewaweka wakfu kwa Mungu haoni aibu kuwaita ndugu.
12 saying—I will declare thy name unto my brethren, in the midst of an assembly, will I sing praise unto thee;
Anasema, “Nitatangaza jina lako kwa ndugu zangu, nitaimba kuhusu wewe kutoka ndani ya kusanyiko.”
13 and again—I, will be confident upon him; and again—Lo! I, and the children which, unto me, God, hath given.
Tena asema, “Nitaamini katika yeye.” Na tena, “Tazama, hapa nipo na watoto ambao Mungu amenipa.”
14 Seeing therefore the children have received a fellowship of blood and flesh, he also, in like manner, took partnership in the same, —in order that, through death, —he might paralyse him that held the dominion of death, that is, the Adversary, —
Kwa hiyo, kwa kuwa watoto wa Mungu wote hushiriki mwili na damu, kadhalika Yesu alishiriki vitu vilevile, ili kwamba kupitia kifo apate kumdhohofisha yule ambaye ana mamlaka juu ya mauti, ambaye ni ibilisi.
15 And might release these—as many as, by fear of death, were all their lifetime liable, to bondage.
Hii ilikuwa hivyo ili awaweke huru wale wote ambao kupitia hofu ya kifo waliishi maisha yao yote katika utumwa.
16 For, not surely of messengers, is he laying hold, but, of Abraham’s seed, he is laying hold.
Kwa hakika siyo malaika anaowasaidia. Badala yake, anawasaidia wazao wa Abraham.
17 Whence he was obliged, in every way, unto the brethren, to be made like, that he might become a merciful and faithful high-priest, in the things pertaining unto God, —for the making of propitiation for the sins of the people.
Kwa hiyo, ilikuwa lazima yeye awe kama ndugu zake katika njia zote, ili aweze kuwa kuhani mkuu mwenye huruma na mwaminifu kwa vitu vya Mungu, na ili kwamba awe na uwezo wa kutoa msamaha kwa dhambi za watu.
18 For, in that, he, suffered when tested, he is able, unto them who are being tested, to give succour.
Kwa sababu Yesu mwenyewe ameteseka, na kujaribiwa, ana uwezo wa kuwasaidia wale wanaojaribiwa.