< Hebrews 10 >
1 For the law, having in a shadow of the destined good things, not the very image of the things, they can never, with the same sacrifices which year by year they offer evermore, make them who approach, perfect;
Kwa vile sheria ni kivuli cha mambo mema yajayo, si yale yaliyo halisi. Sheria kamwe haiwezi kuwakamilisha wale ambao wanaomkaribia Mungu kwa njia ya dhabihu zilezile ambazo makuhani waliendelea kutoa mwaka baada ya mwaka.
2 Else would they not, in that case, have ceased being offered, by reason of those rendering the divine service having no further conscience at all of sins, being once for all purified?
Au vinginevyo dhabihu hizo zisingeweza kukoma kutolewa? Kwa kigezo hicho waabuduo, wakiwa wamesafishwa mara moja, wasingelikuwa na utambuzi zaidi wa dhambi.
3 But, in them, is a recalling to mind of sins, year by year,
Bali katika dhabihu hizo kuna ukumbusho wa dhambi zilizotendwa mwaka baada ya mwaka.
4 For it is impossible for blood of bulls and goats to be taking away sins.
Kwa kuwa haiwezekani kwa damu ya mafahari na mbuzi kuziondoa dhambi.
5 Wherefore, coming into the world, he saith: Sacrifice and offering, thou willedst not, but, a body, hast thou fitted for me, —
Wakati Kristo alipokuja duniani, alisema, “Hamkutamani matoleo au dhabihu, badala yake, mliandaa mwili kwa ajili yangu.
6 In whole-burnt-offerings and sacrifices for sins, thou didst not delight:
Hamkuwa na thamani katika matoleo yote ya kuteketezwa au dhabihu kwa ajili ya dhambi.
7 Then, said I—Lo! I am come, —in the heading of the scroll, it is written concerning me, —to do, O God, thy will.
Kisha nilisema, “Ona, hapa ninayafanya mapenzi yako, Mungu, kama ilivyoandikwa kunihusu mimi katika gombo”.
8 Higher up, saying—Sacrifices, and offerings, and whole-burnt-offerings, and sacrifices for sins, thou willedst not, neither delightedst in, —the which, according to the law, are offered,
Alisema kama ilivyo semwa hapo juu: “Hamkutamani dhabihu, matoleo, au sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya dhambi, wala hukuona furaha ndani yake” dhabihu ambazo zinatolewa kulingana na sheria.
9 Then, hath he said—Lo! I am come! to do, thy will: —he taketh away the first, that, the second, he may establish:
Kisha alisema, “Ona, niko hapa kufanya mapenzi yako”. Ameweka pembeni taratibu zilizo za awali ili kuimarisha zile za pili.
10 By which will, we have been made holy, through the offering of the body of Jesus Christ, once for all.
Katika taratibu za pili, tumekwisha tengwa kwa Mungu kwa mapenzi yake kupitia kujitoa kwa mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa nyakati zote.
11 And, every priest, indeed, standeth daily publicly ministering, and the same sacrifices ofttimes offering, the which never can clear away sins;
Ni kweli, kila kuhani husimama kwa huduma siku kwa siku, akitoa dhabihu ile ile, ambayo, kwa vyovyote, kamwe isingeweza kuziondoa dhambi.
12 But this priest, having offered one sacrifice for sins evermore, sat down on the right hand of God:
Lakini baada ya Kristo kutoa dhabihu mara moja kwa dhambi milele yote, aliketi mkono wa kuume wa Mungu,
13 As for the rest, waiting—until his foes be made his footstool;
akisubiri mpaka maadui zake watiwe chini na kufanywa kiti kwa ajili ya miguu yake.
14 For, by one offering, hath he perfected for evermore, them who are being made holy.
Kwa kuwa kwa njia ya toleo moja amewakamilisha milele wale ambao wametengwa kwa Mungu.
15 But even the Holy Spirit beareth us witness; for, after having said—
Na Roho Mtakatifu pia ashuhudia kwetu. Kwa kuwa kwanza alisema,
16 This is the covenant which I will covenant unto them after these days, saith the Lord, —Giving my laws upon their hearts, upon their understandings also, will I inscribe them,
“Hili ni agano nitakalofanya pamoja nao baada ya siku hizo; asema Bwana: nitaweka sheria zangu ndani ya mioyo yao, na nitaziandika katika akili zao”.
17 [He] also [saith] —of their sins, and of their lawlessnesses, I will in nowise be mindful any more.
Kisha alisema, “Hawatazikumbuka tena dhambi na matendo yao mafu”.
18 But, wherever a remission of these is, there is, no further, offering, for sins.
Sasa mahali palipo na msamaha kwa hawa, hakuna tena dhabihu yoyote kwa ajili ya dhambi.
19 Having therefore, brethren, freedom of speech for the entrance through the Holy place, by the blood of Jesus,
Kwa hiyo, ndugu, tunao ujasiri wa kuingia mahali patakatifu zaidi kwa damu ya Yesu.
20 Which entrance he hath consecrated for us, as a way recent and living, through the veil, that is, his flesh, —
Hiyo ni njia ambayo ameifungua kwa ajili yetu kwa njia ya mwili wake, mpya na hai inayopitia kwenye pazia.
21 And having a great priest over the house of God,
Na kwa sababu tunaye kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu,
22 Let us approach with a genuine heart, in full assurance of faith, having been sprinkled, as to our hearts, from an evil conscience, and bathed, as to our bodies, with pure water;
na tumkaribie na moyo wa kweli katika utimilifu wa uhakika wa imani tukiwa na mioyo iliyonyunyiziwa safi kutoka uovu wa dhamiri na kuwa na miili yetu iliyooshwa kwa maji safi.
23 Let us hold fast the confession of the hope without wavering, —for, faithful, is he that hath promised;
Basi na tushikilie kwa uthabiti katika ungamo la ujasiri wa tumaini letu, bila ya kugeuka, kwa sababu Mungu aliyeahidi ni mwaminifu.
24 And let us attentively consider one another, to provoke unto love and noble works, —
Na tuzidi kutafakari namna ya kumtia moyo kila mmoja kupenda na matendo mema.
25 Not forsaking the assembling of ourselves together, according to the custom of some, but exhorting, and by so much the more as this, by as much as ye behold, the day, drawing near.
Na tusiache kukusanyika pamoja, kama wafanyavyo wengine. Badala yake, kutiana moyo kila mmoja zaidi na zaidi, kama muonavyo siku inakaribia.
26 For, if, by choice, we be sinning, after the receiving of the full-knowledge of the truth, no longer, for sins, is there left over, a sacrifice,
Kama tukifanya makusudi kuendelea kutenda dhambi baada ya kuwa tumepokea elimu ya ukweli, Dhabihu nyingine ya dhambi haisalii tena.
27 But some fearful reception of judgment and fiery jealousy, about to devour the opposers.
Badala yake, kuna tarajio pekee la hukumu ya kutisha, na ukali wa moto ambao utawateketeza maadui wa Mungu.
28 Any one having set aside a law of Moses, apart from compassions, upon [the testimony of] two or three witnesses, dieth:
Yeyote ambaye ameikataa sheria ya Musa hufa bila rehema mbele ya ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.
29 Of how much sorer punishment, suppose ye, shall he be accounted worthy, who hath trampled underfoot the Son of God, and, the blood of the covenant, hath esteemed, a profane thing, by which he had been made holy, and, unto the Spirit of favour, hath offered wanton insult?
kiwango gani zaidi cha adhabu unafikiri kinamstahiri kilammoja ambaye amemdharau mwana wa Mungu, yeyote aliyeitendea damu ya agano kama kitu kisicho kitakatifu, damu ambayo kwayo aliiweka wakfu kwa Mungu - yeyote ambaye amemtukana Roho wa neema?
30 For we know him that hath said—To me, belongeth avenging, I, will recompense; and again—The Lord will judge his people.
Kwakuwa tunajua mmoja ambaye aliyesema, “Kisasi ni changu, nitalipa”. Na tena, “Bwana atawahukumu watu wake”.
31 A fearful thing [it is] to fall into the hands of a Living God!
Ni jambo la kuogofya mtu kuangukia katika mikono ya Mungu aliye hai!
32 But be calling to mind the former days, in which, once ye were illuminated, a great combat of sufferings, ye endured; —
Lakini kumbuka siku zilizopita, baada ya kutiwa kwenu nuru, ni jinsi gani mliweza kuvumilia maumivu makali.
33 Partly, indeed, because, both with reproaches and tribulations, ye were being made a spectacle, but, partly, because, into fellowship with them who were so involved, ye were brought; —
Mlikuwa mmewekwa wazi katika dhihaka ya matukano na mateso, na mlikuwa washiriki pamoja na wale waliopitia mateso kama hayo.
34 For, even with them who were in bonds, ye sympathised, and, unto the seizure of your goods, with joy, ye bade welcome, —knowing that ye have yourselves, for a better possession and an abiding.
Kwa kuwa mlikuwa na moyo wa huruma kwa hao waliokuwa wafungwa, na mlipokea kwa furaha adhabu ya urithi wenu, mkijua kwamba ninyi wenyewe mlikuwa na urithi bora na wa kudumu milele.
35 Do not, then, cast away your freedom of speech, —the which hath a great recompense.
Kwa hiyo msiutupe ujasiri wenu, ulio na zawadi kuu.
36 For, of endurance, ye have need, in order that, the will of God having done, Ye may bear away, the promise.
Kwa kuwa mnahitaji uvumilivu, ili kwamba mpate kupokea ambacho Mungu amekiahidi, baada ya kuwa mmekwisha yatenda mapenzi yake.
37 For, yet a little while, how short! how short! The Coming One will be here, and will not tarry;
Kwa kuwa baada ya kitambo kidogo, mmoja anayekuja, atakuja hakika na hatakawia.
38 But, my righteous one, by faith, shall live, and, if he draw back, my soul delighteth not in him.
Mwenye haki wangu ataishi kwa imani. Kama atarudi nyuma, sitapendezwa naye.”
39 We, however, are not of a drawing back unto destruction, but, of faith, unto an acquisition of life.
Lakini sisi si kama wale warudio nyuma kwa kuangamia. Badala yake, sisi ni baadhi ya wale tulio na imani ya kuzilinda roho zetu.