< Genesis 34 >

1 Then went forth Dinah, the daughter of Leah, whom she had borne to Jacob, —to see the daughters of the land.
Basi Dina, Binti wa Lea aliyemzalia Yakobo, akaenda kuwaona wasichana wa nchi.
2 And Shechem, son of Hamor the Hivite, prince of the land, saw her, —so he took her, and lay with her, and humbled her.
Shekemu mwana wa Hamori Mhivi, mwana mfalme wa nchi, akamwona na akamkamata kwa nguvu na kulala naye.
3 And his soul clave unto Dinah, daughter of Jacob, —and he loved the young woman, and spake to the heart of the young woman.
Akavutiwa na Dina, binti Yakobo. Akampenda msichana na kuongea naye kwa upole.
4 Then spake Shechem unto Hamor his father, saying, —Take me this girl to wife!
Shekemu akamwambia Hamori baba yeke, kusema, “Nipe msichana huyu kuwa mke wangu.”
5 Now, Jacob, had heard that he had defiled Dinah his daughter, but, his sons, happened to be with his cattle in the field, —so Jacob kept quiet until they came in.
Basi Yakobo akasikia kwamba alikuwa amemchafua Dina binti yake. Wanawe walikuwa pamoja na wanyama uwandani, hivyo Yakaobo akawangoja hata walipokuja.
6 Then came forth Hamor, father of Shechem, unto Jacob, —to speak with him.
Hamori baba wa Shekemu akaenda kuongea na Yakobo.
7 Now the sons of Jacob came in from the field as soon as they heard, and the men were grieved, and it was vexing to them exceedingly, —for, a disgraceful deed, had he done with Israel in lying with Jacob’s daughter, seeing that so, it should not be done.
Wana wa Yakobo waliposikia neno hili wakaja kutoka uwandani. Watu hawa walichukizwa sana. Walikasirika sana kwa sababu alikuwa amemwaibisha Israeli kwa kumlazimisha binti wa Yakobo, kwa maana jambo kama hilo halikupasa kutendeka.
8 So then Hamor spake with them saying—As for Shechem my son, his soul hath become attached to your daughter, —I pray you give her to him, to wife.
Hamori akaongea nao, akisema, “Shekemu mwanangu anampenda binti yenu. Tafadhari mpeni kuwa mke wake.
9 And exchange ye daughters with us in marriage, —your daughters, shall ye give to us, and our daughters, shall ye take to you.
Mwoane nasi, tupeni binti zenu, na mjichukulie binti zetu kwa ajili yenu wenyewe.
10 And with us, shall ye dwell, —and, the land, shall be before you, tarry, and go through it, and get possessions therein.
Mtaishi nasi, na nchi itakuwa wazi kwa ajili yenu kufanya biashara humo, na kupata mali.”
11 Then said Shechem unto her father and unto her brethren, Let me find favour in your eyes, —and, whatsoever ye may say unto me, will I give:
Shekemu akamwambia baba yake na ndugu zake, “Na nione kibari machoni penu, na chochote mtakachoniambia nitatoa.
12 Heap on me, exceedingly, dowry and gift, and I will give, just as ye may say unto me, —but give me the young woman, to wife.
Niambieni kiasi kikubwa chochote cha mahari na zawadi kama mtakavyo, nami nitatoa chochote msemacho, lakini mnipe msichana kuwa mke wangu.”
13 And the sons of Jacob answered Shechem and Hamor his father deceitfully, and spake (because he had defiled Dinah their sister)—
Wana wa Yakobo wakamjibu Shekemu na Hamori baba yake kwa hila, kwa sababu Shekemu alikuwa amemnajisi Dina dada yao.
14 and said unto them—We cannot do this thing, to give our sister to a man that is uncircumcised, —for a reproach, it would be to us.
Wakawambia, “Hatuwezi kufanya jambo hili, kumpa dada yetu mtu yeyote ambaye hajatailiwa; kwani hiyo ni aibu kwetu.
15 Only herein, can we consent to you, —If ye will become like us, by circumcising to you every male,
Kwa sharti hili peke yake tutakubaliana nanyi: iwapo mtatailiwa kama sisi, ikiwa kila mtu mme miongoni mwenu atatailiwa.
16 then will we give our daughters to you, and your daughters, will we take to us, —and we will dwell with you, and become one people.
Ndipo tutakapowapa binti zetu, nasi tutachukua binti zenu kwetu sisi wenyewe, na tutaishi nanyi na kuwa wamoja.
17 But if ye will not hearken unto us, to be circumcised, then will we take our daughter and be gone.
Lakini kama hamtusikilizi na kutailiwa, ndipo tutakapomchukua dada yetu na kuondoka.
18 And their words looked fair in the eyes of Hamor, —and in the eyes of Shechem, Hamor’s son;
Maneno yao yakawafurahisha Hamori na Shekemu mwanaye.
19 and the young man deferred not to do the thing, because he had delight in Jacob’s daughter, —he, moreover being more honourable than all the house of his father.
Kijana hakukawia kufanya walichokisema, kwa maana alipendezwa na binti Yakobo, na kwa sababu alikuwa mtu aliyeheshimiwa sana katika nyumba ya babaye.
20 So Hamor entered with Shechem his son into the gate of their city, —and they spake unto the men of their city, saying:
Hamori na Shekemu mwanaye wakaenda katika lango la mji wao na kuongea na watu wa mji, kusema,
21 As for these men, in peace, they are with us—let them therefore dwell in the land and go through it, for, the land, lo! it is roomy on both hands before them, —their daughters, let us take to us for wives, and our daughters, let us give to them.
“Watu hawa wanaamani nasi, hivyo na waishi katika nchi na kufanya biashara humo kwa maana, kweli, nchi ni kubwa ya kuwatosha. Haya na tuwachukue binti zao kuwa wake, nasi tuwape binti zetu.
22 Only herein, will the men consent to us, to dwell with us, to become one people, —If we circumcise to us every male, even as they are circumcised.
Kwa shariti hili pekee watu hawa wanakubali kuishi nasi na kuwa wamoja: ikiwa kila mwanamme miongoni mwetu atatailiwa, kama wao.
23 Their herds and their substance, and all their beasts, shall they, not be, ours? Only, we must consent to them, that they may dwell with us.
Je wanyama wao na vitu vyao - wanyama wao wote kuwa wetu? Haya na tukubaliane nao, nao wataishi kati yetu.”
24 And they hearkened unto Hamor, and unto Shechem his son, even all that were going forth out of the gate of his city, —and every male was circumcised, all that were going forth out of the gate of his city.
Watu wote wa mji wakamsikiliza Hamori na Shekemu, mwanaye. Kila mwanamme akatailiwa.
25 And it came to pass on the third day, when they were in pain, that two of the sons of Jacob Simeon and Levi, Dinah’s brothers, took each man his sword, and came in upon the city, boldly, —and slew every, male;
Katika siku ya tatu, walipokuwa katika maumivu bado, wawili wa wana wa Yakobo (Simoni na Lawi, kaka zake Dina), wakachukua kila mmoja upanga wake na kuushambulia mji ambao ulikuwa na uhakika wa ulinzi wake, nao wakauwa wanamme wote.
26 Hamor also, and Shechem his son, slew they with the edge of the sword, —and took Dinah out of the house of Shechem, and came forth,
Wakamwua Hamori na Shekemu kwa makali ya upanga. Wakamchukua Dina kutoka nyumba ya Shekemu na kuondoka.
27 The sons of Jacob, came in upon the slain and plundered the city, —because they had defiled their sister:
Wale wana wengine wa Yakobo wakaja kwa maiti na kuuteka nyara mji, kwa sababu watu wale walikuwa wamemnajisi dada yao.
28 their flocks, and their herds and their asses, —and that which was in the city, and that which was in the field, they took;
Wakachukua makundi yao ya kondoo, mbuzi, punda, na kila kitu ndani ya mji na viunga vyake
29 and all their wealth and all their little ones, and their women, took they captive, and seized as plunder, —even all that was in their houses.
utajiri wote. Watoto na wake zao wote, wakawachukua. Hata wakachukua kila kitu kilichokua katika nyumba.
30 Then said Jacob unto Simeon and unto Levi—Ye have troubled me by making me odious among them that dwell in the land, among the Canaanites, and among the Perizzites, —I, having only men that may be counted, they will gather themselves, together against me and smite me, —and I shall be destroyed both I and my house.
Yakobo akawambia Simoni na Lawi, “Mmeleta shida juu yangu, kunifanya ninuke kwa wenyeji wa nchi, Wakanaani na Waperizi. Mimi nina watu wachache. Ikiwa watajikusanya pamoja kinyume changu na kunishambulia.”
31 And they said, —As with a harlot, was he to deal with our sister.
Lakini Simoni na Lawi wakasema, “Je Shekemu alipaswa kumtendea dada yetu kama kahaba?”

< Genesis 34 >