< Genesis 18 >
1 And Yahweh appeared unto him among the oaks of Mamre, —as, he, was sitting at the opening of the tent in the heat of the day.
Bwana akamtokea Abrahamu karibu na mialoni ya Mamre wakati alipokuwa ameketi kwenye ingilio la hema lake wakati wa adhuhuri.
2 And he lifted up his eyes and looked, and lo! three men, standing over against him, —so he looked and ran to meet them from the opening of the tent, and bowed himself to the earth;
Abrahamu akainua macho akaona watu watatu wamesimama karibu naye. Alipowaona, aliharakisha kutoka kwenye ingilio la hema lake kuwalaki na kuwasujudia hadi nchi.
3 and said, —O My Lord! if, I pray thee, I have found favour in thine eyes, do not I pray thee pass on from thy servant.
Akasema, “Kama nimepata kibali machoni penu, ee bwana wangu, usimpite mtumishi wako.
4 Let there be fetched, I pray thee a little water, and bathe ye your feet, —and rest yourselves under the tree.
Acha yaletwe maji kidogo, kisha ninyi nyote mnawe miguu yenu na mpumzike chini ya mti huu.
5 And let me fetch a morsel of bread, and stay ye your heart, Afterwards, ye may pass on, For on this account, have ye passed by, over against your servant. And they said, Thus, shalt thou do as thou hast spoken.
Niruhusuni niwapatie chakula kidogo mle, ili mpate nguvu mwendelee na safari yenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.” Nao wakamjibu, “Vema sana, fanya kama unavyosema.”
6 So Abraham hastened towards the tent unto Sarah, —and said, Hasten thou three measures of fine meal, knead it, and make hearth-cakes.
Hivyo Abrahamu akaharakisha akaingia hemani kwa Sara, akamwambia, “Chukua vipimo vitatu vya unga laini haraka, ukande na uoke mikate.”
7 And unto the herd, ran Abraham, —and took a calf tender and good and gave unto the young man, and he hastened to make it ready.
Kisha Abrahamu akakimbia kwenda kwenye kundi, akachagua ndama mzuri, laini na akampa mtumishi, ambaye aliharakisha kumtayarisha.
8 And he took butter and milk and the calf that he had made ready, and set before them, —while, he, was standing near them under the tree, they did eat.
Kisha akaleta jibini, maziwa na nyama ya yule ndama iliyoandaliwa, akaviweka mbele ya wageni. Walipokuwa wakila, alisimama karibu nao chini ya mti.
9 And they said unto him, As to Sarah thy wife… And he said Lo! [she is] in the tent.
Wakamuuliza, “Yuko wapi Sara mkeo?” Akasema, “Yuko huko, ndani ya hema.”
10 And he said, I will, surely return, unto thee at the quickening season, —and lo! a son for Sarah thy wife. Now Sarah, was hearkening at the opening of the tent, it, being behind him.
Kisha Bwana akasema, “Hakika nitakurudia tena majira kama haya mwakani na Sara mkeo atakuwa ana mwana.” Sara alikuwa akiwasikiliza kwenye ingilio la hema, lililokuwa nyuma yake.
11 But Abraham and Sarah, were old, far gone in days, —it had ceased to be with Sarah after the manner of women.
Abrahamu na Sara walikuwa wazee tena waliosogea miaka, naye Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake.
12 So then Sarah laughed within herself, saying: After I am past age, hath there come to me pleasure, my lord, also being old?
Hivyo Sara akacheka kimoyomoyo alipokuwa akiwaza, “Baada ya mimi kuwa mkongwe hivi na bwana wangu amezeeka, je, nitaweza kufurahia jambo hili?”
13 And Yahweh said unto Abraham, —Wherefore now did Sarah laugh saying. Can it really and truly be that I should bear, seeing that I have become old?
Ndipo Bwana akamwambia Abrahamu, “Kwa nini Sara amecheka na kusema, ‘Kweli nitazaa mtoto nami sasa ni mzee?’
14 Is anything, too wonderful for Yahweh? At the appointed time, I will return unto thee, at the quickening season and Sarah, shall have a son.
Je, kuna jambo lolote gumu lisilowezekana kwa Bwana? Nitakurudia mwakani majira kama haya, naye Sara atakuwa na mwana.”
15 And Sarah denied, saying, I laughed not, For she was afraid. And he said—Nay! but thou didst laugh!
Sara akaogopa kwa kuwa alidanganya na kusema, “Mimi sikucheka.” Lakini Bwana akasema, “Ndiyo, ulicheka!”
16 And the men rose up from thence, and looked out over the face of Sodom, —Abraham also going with them to set them on their way.
Wakati watu hao waliposimama ili waondoke, walielekeza nyuso zao Sodoma, Abrahamu akawatoa kitambo kidogo ili awasindikize.
17 Now, Yahweh, had said, —Am I going to hide from Abraham what I do,
Ndipo Bwana akasema, “Je, nimfiche Abrahamu jambo ninalokusudia kufanya?
18 when, Abraham, shall surely become, a great and mighty nation, —and all the nations of the earth, shall be blessed in him?
Hakika Abrahamu atakuwa taifa kubwa na lenye nguvu, kupitia kwake mataifa yote ya dunia yatabarikiwa.
19 For I have become his intimate friend, To the end that he may command his sons and his house after him, so shall they keep the way of Yahweh, by doing righteousness and justice. To the end that Yahweh may bring in for Abraham, what he hath spoken concerning him.
Kwa maana nimemchagua yeye, ili awaongoze watoto wake na jamaa yake kufuata njia ya Bwana, kwa kuwa waadilifu na kutenda haki, ili Bwana atimize ahadi yake kwa Abrahamu.”
20 So Yahweh said, The outcry of Sodom and Gomorrah, because it hath become great, —And their sin, because it hath become exceeding grievous,
Basi Bwana akasema, “Kilio dhidi ya Sodoma na Gomora ni kikubwa sana na dhambi yao inasikitisha sana,
21 Let me go down, pray, and let me behold, whether according to their outcry which hath come in unto me, they have done altogether, And if not. I must know!
kwamba nitashuka nione kama waliyoyatenda ni mabaya kiasi cha kilio kilichonifikia. Kama sivyo, nitajua.”
22 And the men turned from thence, and went their way, towards Sodom, —but, Yahweh was yet standing before Abraham.
Basi wale watu wakageuka wakaenda kuelekea Sodoma, lakini Abrahamu akabaki amesimama mbele za Bwana.
23 So then Abraham drew near and said, Wilt thou really sweep away, the righteous with the lawless?
Ndipo Abrahamu akamsogelea akasema: “Je, utawaangamiza wenye haki na waovu?
24 Peradventure there are fifty righteous, in the midst of the city, Wilt thou really sweep away, and not spare the place, for the sake of the fifty righteous which are therein?
Je, ikiwa watakuwepo watu wenye haki hamsini katika mji huo, hivi kweli utauangamiza na wala hutauacha kwa ajili ya hao watu hamsini wenye haki waliomo ndani yake?
25 Far be it from thee! to do after this manner. to put to death the righteous with the lawless! Then should righteous and lawless be alike, Far be it from thee! Shall, the Judge of all the earth not do justice?
Hilo na liwe mbali nawe, kufanya jambo kama hilo, kuwaua wenye haki pamoja na waovu, kuwatendea wenye haki sawasawa na waovu. Iwe mbali nawe! Je, Mwamuzi wa dunia yote hatafanya lililo sawa?”
26 And Yahweh said, If I find in Sodom fifty righteous in the midst of the city, then will I spare all the place for their sake.
Bwana akasema, “Kama nikipata watu hamsini wenye haki katika mji wa Sodoma, nitausamehe huo mji wote kwa ajili yao.”
27 And Abraham responded and said, —Behold I pray thee I have ventured to speak unto My Lord, though I am dust and ashes:
Kisha Abrahamu akasema tena: “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri wa kuzungumza na Bwana, ingawa mimi si kitu bali ni mavumbi na majivu;
28 Peradventure there may lack, of the fifty righteous, five, Wilt thou destroy for five all the city? And he said, I will not destroy, if I find there forty and five.
je, kama hesabu ya wenye haki imepungua watano katika hamsini, utauangamiza huo mji wote kwa ajili ya hao watano waliopungua?” Bwana akamwambia, “Kama nikiwakuta huko watu arobaini na watano, sitauangamiza.”
29 And he added, yet once more, to speak unto him, and said, Peradventure there may be found there—forty. And he said—I will not do it, for the sake of the forty.
Abrahamu akazungumza naye kwa mara nyingine, “Je, kama huko watapatikana watu arobaini tu?” Akamjibu, “Kwa ajili ya hao arobaini, sitauangamiza.”
30 And he said Let it not, I pray thee, be vexing to My Lord, but let me speak, Peradventure there may be found there—thirty And he said, I will not to it, if I find there—thirty.
Ndipo akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze. Je, kama huko watakuwepo thelathini tu?” Akajibu, “Sitapaangamiza ikiwa nitawakuta huko watu thelathini.”
31 And he said Behold, I pray thee, I have ventured to speak unto My Lord, Peradventure there may be found there—twenty. And he said I will not destroy it, for the sake of the twenty.
Abrahamu akasema, “Sasa kwa kuwa nimekuwa na ujasiri sana kuzungumza na Bwana, je, kama wakipatikana huko watu ishirini tu?” Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao ishirini, sitauangamiza.”
32 And he said, Let it not, I pray thee, be vexing to My Lord, but let me speak only this once, Peradventure there may be found there—ten. And he said, I will not destroy [it], for the sake of the ten!
Abrahamu akasema, “Bwana na asikasirike, lakini niruhusu nizungumze tena mara moja tu. Itakuwaje kama watapatikana huko watu kumi tu?” Bwana akajibu, “Kwa ajili ya hao kumi, sitauangamiza.”
33 And Yahweh went his way, when he had made an end. of speaking unto Abraham, —Abraham, also returned to his place.
Bwana alipomaliza kuzungumza na Abrahamu, akaondoka, naye Abrahamu akarudi nyumbani kwake.