< Genesis 10 >
1 Now, these are the generations of the sons of Noah, Shem, Ham, and Japheth, and there were born to them sons after the flood.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 The sons of Japheth: Gomer and Magog, and Madai, and Javan and Tubal, —and Meshech, and Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 And the sons of Gomer: Ashkenaz and Riphath, and Togarmah.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 And the sons of Javan: Elishah, and Tarshish. Kittim, and Rodanim, —
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 From these, were dispersed [the inhabitants] of the coastlands of the nations, in their lands, each man by his tongue, by their families in their nations.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 And, the sons of Ham: Cush and Mizraim and Phut and Canaan.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 And, the sons of Cush: Seba and Havilah, and Sabtah and Raamah, and Sabtechah, —And the sons of Raamah, Sheba and Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 And, Cush begat Nimrod.—he, became a hero in the earth;
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 he, became a hero of hunting before Yahweh, for this cause, it is said. Like Nimrod, a hero of hunting before Yahweh.
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 So the beginning of his kingdom came to be Babel, and Erech, and Accad and Calneh, in the land of Shinar.
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 From that land, went forth Asshur, —and he built Nineveh, and Rehoboth-ir, and Calah:
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 and Resen, between Niveveh and Calah, —the same is the great city.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 And, Mizraim, begat Ludim and Anamim and Lehabim, and Naphtuchim;
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 and Pathrusim and Casluhim whence came forth Philistim and Caphtorim.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 And Canaan begat Zidon his firstborn, and Heth:
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 and the Jebusite, and the Amorite, and the Girgashite;
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 and the Hivite and the Arkite, and the Sinite:
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 and the Arvadite and the Zemarite and the Hamathite, —and after-wards, were spread abroad the families of the Canaanite.
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 And it came to pass that the boundary of the Canaanite was from Zidon, as thou enterest in towards Gerar unto Gaza, —as thou enterest in towards Sodom and Gomorrah and Admah and Zeboim, as far as Lasha.
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 These, are the sons of Ham, by their families by their tongues, in their lands in their nations.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 Now, to Shem, father of all the sons of Eber, elder brother of Japheth, to him also, were children born.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 The sons of Shem, Elam and Asshur, —and Arpachshad and Lud and Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 And, the sons of Aram: Uz and Hul, and Gether and Mash.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 Now Arpachshad, begat Shelah, and Shelah begat Eber.
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 And to Eber, were born two sons, —the name of the one was Peleg, for in his days, was the earth divided, and the name of his brother was Joktan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 Now, Joktan, begat Almodad, and Sheleph, and Hazarmaveth, and Jerah;
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 and Hadoram and Uzal, and Diklah:
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 and Obal and Abimael, and Sheba:
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 and Ophir and Havilah, and Jobab—all these were sons of Joktan.
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 And it came to pass that their dwelling was from Mesha, as thou enterest in towards Sephar, the mountain of the east.
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 These are the sons of Shem, by their families by their tongues, in their lands by their nations.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 These, are the families of the sons of Noah, by their generations in their nations, and from these, were dispersed the nations in the earth after the flood.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.