< Ezra 9 >
1 Now, when these things were ended, the rulers drew near unto me, saying, The people of Israel and the priests and the Levites have not kept themselves separate from the peoples of the lands, —in view of their abominations-even of the Canaanites, the Hittites, the Perizzites, the Jebusites, the Ammonites, the Moabites, the Egyptians, and the Amorites;
Kipindi mambo hayo yanatendeka, wakuu wakaja kwangu na kuniambia,”Watu wa Israel, Makuhani na walawi hawakuweza kujitenga wenyewe kutoka kwa watu wa nchi zingine na maovu yao: Wakanaani, Wahiti, Waperuzi, wayebusi, Waamoni, Wamoabu, Wamisri na Waamori.
2 for they have taken of their daughters, for themselves and for their sons, so that the holy seed have intermingled themselves among the peoples of the lands, —and, the hand of the rulers and the deputies, hath, in this unfaithfulness, been, foremost.
Kwa kuwa wamewachukua baadhi ya binti na watoto wa kiume, wamejichanganya watu watakatifu na watu wa nchi nyingine na wakuu na viongozi wamekuwa wa kwanza katika imani hii potofu.
3 When I heard this thing, I rent my garment, and my robe, —and tore out of the hair of my head and my beard, and sat stunned.
Niliposikia haya, nikachana nguo zangu na kanzu na kunyoa nywele kichwani na ndevu na nikakaa chini kutafakari.
4 Then, unto me, were gathered, all who trembled at the words of the God of Israel, concerning the unfaithfulness of them who had been exiled, —but, I, sat stunned, until the evening gift.
Na wale wote waliotetemeka kwa neno la Mungu wa Israel kuhusu imani potofu walikusanyika kwangu wakati nimakaa chini nikiwa na aibu hadi kufikia kipindi cha sadaka za jioni.
5 And, at the evening gift, I arose from mine affliction, which had been accompanied by the rending of my garment and my robe, —and I bowed upon my knees, and spread forth my hands unto Yahweh my God;
Lakini katika sadaka ya jioni nikasimama kwenye nafasi yangu nikiwa mnyenyekevu na nguo ilichanika na kanzu, na nikapiga magoti na kunyoosha mikono yangu kwa Yahwe Mungu wangu. Nikasema
6 and said, O my God, I turn pale and am ashamed, to lift up, O my God, my face unto thee, —for, our iniquities, have multiplied above the head, and our guilt hath magnified itself unto the heavens.
“Mungu wangu, nina aibu na sistahili kuinua uso wangu kwako, makosa yetu yamekuwa hadi kuvuka kichwani na maovu yetu yameongezeka kufika mbinguni.
7 Since the days of our fathers, we, have been in great guilt, until this day, —and, for our iniquities, have we been given up—we, our kings, our priests, —into the hand of the kings of the lands, by sword and by captivity and by spoiling and by a turning pale of face, as at this day.
Kuanzia siku ya watangulizi wetu mpaka sasa tumekuwa katika maovu makuu. Makosa yetu, viongozi, makuhani, walikuwa katika mikono ya mfalme wa dunia hii, katika upanga, matekani na kunyanyaswa na tuna aibu ya uso hata leo.
8 And, now, for a very little moment, hath come favour from Yahweh our God, in leaving to us a remnant to escape, and in giving to us a nail in his holy place, —that our God may enlighten our eyes, and give us a little reviving in our bondage.
sasa kwa kipindi kifupi, neema kutoka kwa Yahwe Mungu wetu imekuja kutuacha mabaki wachache na kutupa kuhimmili sehemu takatifu. Hii ilikuwa ni kwa ajili ya Mungu wetu kututia nuru macho yetu na kutupa unafuuu sisi tulio watumwa.
9 For, bondmen, we are, but, in our bondage, hath our God not forsaken us, —but extended unto us lovingkindness before the kings of Persia, to give us a reviving, to set up on high the house of our God, to raise up the desolations thereof, and to give us a wall in Judah and in Jerusalem.
Kwa kuwa sisi tu watumwa, lakini Mungu bado hajatusahau lakini ameongeza agano la uaminifu kwetu, ameyatenda haya mbele ya macho ya mfalme wa Uajemi ili kwamba haweze kutupatia nguvu mpya. Ili kwamba tuweze kujenga nyumba ya Mungu na tuweze kuondoa majuto. Alitenda hayo ili kwamba aweze kutupatia msingi wa usalama katika Yuda na Yerusalem.
10 But, now, what can we say, O our God, after this? for we have forsaken thy commandments,
Lakini sasa Mungu wetu, tuseme nini baaada ya haya? Tumesahau amri zako.
11 which thou didst command by the hand of thy servants the prophets, saying, As for the land which, ye, are entering to possess, an impure land, it is, with the impurity of the peoples of the lands, —with their abominations, which have filled it from one end to the other, with their uncleanness.
amri ambazo uliwapa manabii watumishi wako, pale uliposema, “Nchi hii mnayoingia kuimiliki ni nchi chafu. Imechanganyikana na watu wasio na utaratibu. ameenea kutoka sehemu moja hadi nyingine kwa uchafu wao.
12 Now, therefore, your daughters, do not ye give to their sons, and, their daughters, do not ye take for your sons, neither shall ye seek their prosperity nor their pleasure unto times age-abiding, —to the end ye may become strong, and may eat the good of the land, and may suffer your children to possess it, unto times age-abiding.
Hivyo sasa, msiwape binti zenu kwa watoto wao, msichukue binti zao kwa ajili ya watoto wenu, msitafute amani kwao na fadhili, ili kwamba muweze kuwa imara na kula vizuri vya nchi, hivyo utasababisha watoto wenu kumiliki kwa wakati wote.”
13 And, after all that hath come upon us, for our wicked doings, and for our great guilt—For, thou, O our God, hast spared us, punishing us less than our iniquities deserved, and hast given us a deliverance such as this,
Baada ya yote kutokea kwetu kwa sababu ya uovu wetu na makosa yetu makuu, tokea hapo, Mungu wetu, hukutazama makosa yetu na kutuadhibu tulivyostahili na ukatuacha kama mabaki.
14 should we again break thy commandments and join ourselves by affinity of marriage with the peoples of these abominations, —wouldst thou not be angry with us, unto a full end, that there should be neither remainder nor deliverance?
Tunaweza kuvunja tena amri zako na kuingiliana katika ndoa, na hawa watu wasiofuata utaratibu? Je hautachukia na kututowesha sote hakuna wa kubaki, hakuna wa kutoroka?
15 O Yahweh, God of Israel, righteous thou art, for we have had left us a deliverance as at this day, —here we are, before thee, in our guilty deeds, for there is no standing before thee, because of this thing!
Yahwe, Mungu wa Israel, wewe ni mwenye haki, kwa kuwa tumebaki wachache mabaki hadi siku ya leo. Tazama, tuko mbele yako na makosa yetu, kwa kuwa hakuna hata mmoja anayeweza kusimama mbele kwa sababu ya hili.