< Ezra 3 >
1 But, when the seventh month was come, and the sons of Israel were in cities, then did the people gather themselves together as one man, unto Jerusalem.
Mwezi wa saba ulipowadia baada ya Waisraeli kukaa katika miji yao, watu wote walikusanyika huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
2 Then arose—Jeshua son of Jozadak and his brethren the priests, and Zerubbabel son of Shealtiel and his brethren, and built the altar of the God of Israel, —to offer thereon ascending-sacrifices, as it was written in the law of Moses, the man of God.
Yeshua mwana wa Yosadaki na makuhani wenzake, Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na wenzake walianza kujenga madhabahu ya Mungu wa Israeli ili kumtolea dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake, kulingana na ilivyoandikwa katika Sheria ya Mose mtu wa Mungu.
3 So they settled the altar upon its stands, for, dread, was upon them, because of the peoples of the countries, —therefore caused they to go up thereon, ascending-sacrifices unto Yahweh, ascending-sacrifices for the morning and for the evening.
Ingawa waliwaogopa watu waliowazunguka, walijenga madhabahu juu ya ule msingi wake, wakamtolea Bwana dhabihu za sadaka za kuteketezwa kwa moto juu yake za asubuhi na za jioni.
4 And they kept the festival of booths, as it was written, —and the ascending-offering of each day upon its own day, by number, according to regulation, the matter of a day upon its day;
Kisha kulingana na kile kilichoandikwa, wakaiadhimisha Sikukuu ya Vibanda wakitoa idadi ya sadaka za kuteketezwa kama ilivyohitajika kila siku sawasawa na ilivyoagizwa.
5 and, afterwards, the continual ascending-sacrifice, and, on the new moons, and on all the appointed seasons of Yahweh, the hallowed things, —also for every one that volunteered a voluntary offering unto Yahweh.
Baada ya hayo, walitoa sadaka za kuteketezwa za kawaida, sadaka za Mwezi Mwandamo na dhabihu zote za sikukuu takatifu za Bwana zilizoamriwa, pamoja na zile sadaka za hiari zilizotolewa kwa Bwana.
6 From the first day of the seventh month, began they to offer up ascending-sacrifices unto Yahweh, —but, the temple of Yahweh, had not had its foundation laid.
Ingawa bado msingi wa Hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa, watu walianza kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Bwana tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
7 And they gave silver, unto the masons and carpenters, —and food and drink and oil, unto them of Zidon and unto them of Tyre, to bring in cedar-trees out of the Lebanon, unto the sea of Joppa, according to the grant of Cyrus king of Persia unto them.
Kisha watu wakawapa mafundi wa uashi na useremala fedha, wakawapa watu wa Sidoni na Tiro vyakula, vinywaji na mafuta ili waweze kuleta magogo ya mierezi kwa njia ya bahari kutoka Lebanoni hadi Yafa, kama alivyoagiza Koreshi mfalme wa Uajemi.
8 Now, in the second year of their coming in unto the house of God, to Jerusalem, in the second month, began Zerubbabel son of Shealtiel and Jeshua son of Jozadak and the rest of their brethren—the priests and the Levites, and all that were come out of the captivity to Jerusalem, and stationed the Levites, of twenty years old and upwards, to preside over the work of the house of Yahweh.
Katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kufika kwenye nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zao wengine (makuhani, Walawi na wote waliorejea Yerusalemu kutoka uhamishoni) walianza kazi, wakiteua Walawi wenye umri kuanzia miaka ishirini au zaidi kusimamia ujenzi wa nyumba ya Bwana.
9 So they took their station—even Jeshua, his sons and his brethren, Kadmiel and his sons, sons of Judah, as one man to preside over the doer of the work in the house of God, the sons of Henadad, their sons and their brethren, the Levites.
Yeshua na wanawe, pamoja na ndugu zake, Kadmieli na wanawe (wazao wa Hodavia), wana wa Henadadi na wana wao na ndugu zao, Walawi wote walijiunga pamoja kusimamia wale waliofanya kazi katika nyumba ya Mungu.
10 And, when the builders laid the foundation of the temple of Yahweh, then the priests, enrobed, took their stand with trumpets, and the Levites the sons of Asaph with cymbals, to offer praise unto Yahweh, after the instructions of David king of Israel.
Wajenzi walipoweka msingi wa Hekalu la Bwana, makuhani wakiwa wamevalia mavazi yao wakiwa na tarumbeta na Walawi (wana wa Asafu) wakiwa na matoazi, walishika nafasi zao za kumtukuza Bwana, kama ilivyoagizwa na Daudi mfalme wa Israeli.
11 And, when they made responses in offering praise and in giving thanks unto Yahweh—For he is good, for, age-abiding, is his lovingkindness, upon Israel, then, all the people, shouted with a great shout, in offering praise unto Yahweh, over the laying of the foundation of the house of Yahweh.
Waliimba nyimbo za sifa na za shukrani kwa Bwana hivi: “Yeye ni mwema; upendo wake kwa Israeli wadumu milele.” Watu wote wakapaza sauti kubwa za sifa kwa Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana ulikuwa umewekwa.
12 But, many of the priests and the Levites and the ancestral chiefs, who were old men, that had seen the first house, when the foundation of this house was laid before their eyes, were weeping with a loud voice, —many, however, shouting and rejoicing, with voice raised on high;
Lakini wengi wa makuhani wazee, Walawi na viongozi wa jamaa waliokuwa wameona Hekalu la mwanzoni, walilia kwa sauti walipoona msingi wa Hekalu hili ukiwekwa, huku wengine wengi wakipiga kelele kwa furaha.
13 so that the people could not distinguish the noise of the shout of joy, from the noise of the weeping of the people, —for, the people, did shout with a great shout, and, the noise, was heard afar off.
Hakuna mtu ambaye angeweza kutofautisha sauti hizo za furaha na za kilio, kwa sababu watu walipiga kelele sana. Nayo hiyo sauti ikasikika mbali.