< Ezra 2 >

1 Now, these, are the sons of the province, who came up from among the captives of the exile, whom Nebuchadnezzar the king of Babylon exiled to Babylon, —who came back unto Jerusalem and Judah, every one unto his own city;
Basi hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka hadi Babeli (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,
2 who came in with Zerubbabel, Jeshua, Nehemiah, Seraiah, Reelaiah, Mordecai, Bilshan, Mispar, Bigvai Rehum, Baanah, —the number of the men of the people of Israel: —
wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana): Orodha ya wanaume kati ya watu wa Israeli ilikuwa:
3 The sons of Parosh, two thousand one hundred and seventy-two;
wazao wa Paroshi 2,172
4 The sons of Shephatiah, three hundred and seventy-two;
wazao wa Shefatia 372
5 The sons of Arah, seven hundred and seventy-five;
wazao wa Ara 775
6 The sons of Pahath-moab, belonging to the sons of Jeshua, Joab, two thousand eight hundred and twelve;
wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,812
7 The sons of Elam, a thousand two hundred and fifty-four;
wazao wa Elamu 1,254
8 The sons of Zattu, nine hundred and forty-five;
wazao wa Zatu 945
9 The sons of Zaccai, seven hundred and sixty;
wazao wa Zakai 760
10 The sons of Bani, six hundred and forty-two;
wazao wa Bani 642
11 The sons of Bebai, six hundred and twenty-three;
wazao wa Bebai 623
12 The sons of Azgad, a thousand two hundred and twenty-two;
wazao wa Azgadi 1,222
13 The sons of Adonikam, six hundred and sixty-six;
wazao wa Adonikamu 666
14 The sons of Bigvai, two thousand and fifty-six;
wazao wa Bigwai 2,056
15 The sons of Adin, four hundred and fifty-four;
wazao wa Adini 454
16 The sons of Ater pertaining to Hezekiah, ninety-eight;
wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98
17 The sons of Bezai, three hundred and twenty-three;
wazao wa Besai 323
18 The sons of Jorah, a hundred and twelve;
wazao wa Yora 112
19 The sons of Hashum, two hundred and twenty-three:
wazao wa Hashumu 223
20 The sons of Gibbar, ninety-five;
wazao wa Gibari 95
21 The sons of Bethlehem, a hundred and twenty-three;
watu wa Bethlehemu 123
22 The men of Netophah, fifty-six;
watu wa Netofa 56
23 The men of Anathoth, a hundred and twenty-eight;
watu wa Anathothi 128
24 The sons of Azmaveth, forty-two;
watu wa Azmawethi 42
25 The sons of Kiriath-arim, Chephirah and Beeroth, seven hundred and forty-three;
wazao wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743
26 The sons of Ramah and Geba, six hundred and twenty-one;
wazao wa Rama na Geba 621
27 The men of Michmas, a hundred and twenty-two:
watu wa Mikmashi 122
28 The men of Bethel and Ai, two hundred and twenty-three;
watu wa Betheli na Ai 223
29 The sons of Nebo, fifty-two;
wazao wa Nebo 52
30 The sons of Magbish, a hundred and fifty-six;
wazao wa Magbishi 156
31 The sons of the other Elam, a thousand two hundred and fifty-four;
wazao wa Elamu ile ingine 1,254
32 The sons of Harim, three hundred and twenty;
wazao wa Harimu 320
33 The sons of Lod, Hadid and Ono, seven hundred and twenty-five;
wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 725
34 The sons of Jericho, three hundred and forty-five;
wazao wa Yeriko 345
35 The sons of Senaah, three thousand and six hundred and thirty!
wazao wa Senaa 3,630
36 The priests, The sons of Jedaiah of the house of Jeshua, nine hundred and seventy-three;
Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973
37 The sons of Immer, a thousand and fifty-two;
wazao wa Imeri 1,052
38 The sons of Pashhur, a thousand two hundred and forty-seven;
wazao wa Pashuri 1,247
39 The sons of Harim, a thousand and seventeen,
wazao wa Harimu 1,017
40 The Levites, The sons of Jeshua, and Kadmiel of the sons of Hodaviah, seventy-four.
Walawi: wazao wa Yeshua na Kadmieli (kupitia jamaa ya Hodavia) 74
41 The singers, The sons of Asaph, a hundred and twenty-eight.
Waimbaji: wazao wa Asafu 128
42 The sons of the door-keepers, The sons of Shallum, the sons of Ater, the sons of Talmon, the sons of Akkub, the sons of Hatita, the sons of Shobai, —in all, a hundred and thirty-nine.
Mabawabu wa lango la Hekalu: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 139
43 The Nethinim, The sons of Ziha, the sons of Hasupha, the sons of Tabbaoth;
Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,
44 the sons of Keros, the sons of Siaha, the sons of Padon;
wazao wa Kerosi, Siaha, Padoni,
45 the sons of Lebanah, the sons of Hagabah, the sons of Akkub;
wazao wa Lebana, Hagaba, Akubu,
46 the sons of Hagab, the sons of Shamlai, the sons of Hanan;
wazao wa Hagabu, Shalmai, Hanani,
47 the sons of Giddel, the sons of Gahar, the sons of Reaiah;
wazao wa Gideli, Gahari, Reaya,
48 the sons of Rezin, the sons of Nekoda, the sons of Gazzam;
wazao wa Resini, Nekoda, Gazamu,
49 the sons of Uzza, the sons of Paseah, the sons of Besai;
wazao wa Uza, Pasea, Besai,
50 the sons of Asnah, the sons of Meunim, the sons of Nephisim;
wazao wa Asna, Meunimu, Nefusimu,
51 the sons of Bakbuk, the sons of Hakupha, the sons of Harhur;
wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,
52 the sons of Bazluth, the sons of Mehida, the sons of Harsha;
wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,
53 the sons of Barkos, the sons of Sisera, the sons of Temah;
wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,
54 the sons of Neziah, the sons of Hatipha.
wazao wa Nesia na Hatifa.
55 The Sons of the Servants of Solomon. The sons of Sotai, the sons of Hasso-phereth, the sons of Peruda;
Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Hasaferethi, Peruda,
56 the sons of Jaalah, the sons of Darkon, the sons of Giddel;
wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,
57 the sons of Shephatiah, the sons of Hattil, the sons of Pochereth-hazzebaim, the sons of Ami.
wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Ami.
58 All the Nethinim, and the Sons of the Servants of Solomon, were three hundred and ninety-two.
Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392
59 And, these, were they who came up from Tel-melah, Tel-harsha, Cherub, Addan, Immer; but they could not tell their ancestral house, nor their seed, whether, of Israel, they were:
Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:
60 the sons of Delaiah, the sons of Tobiah, the sons of Nekoda, —six hundred and fifty-two.
wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 652
61 And, of the sons of the priests, the sons of Habaiah, the sons of Hakkoz, —the sons of Barzillai, who took of the daughters of Barzillai the Gileadite to wife, and was called after their name.
Kutoka miongoni mwa makuhani: Wazao wa Hobaya, Hakosi, Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).
62 These, sought their writing wherein they were registered, but they were not found, —so they were desecrated out of the priesthood;
Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.
63 and the governor told them, that they must not eat of the most holy things, —until there should stand up a priest, with Lights and Perfections.
Mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.
64 All the gathered host together, was forty-two thousand three hundred and sixty;
Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;
65 besides, their men-servants and their maid-servants who were these, seven thousand three hundred and thirty-seven, —and there pertained to them, singing men and singing women, two hundred:
tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 200.
66 their horses, were seven hundred and thirty-six, —their mules, two hundred and forty-five;
Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245,
67 their camels, four hundred and thirty-five, —asses, six thousand seven hundred and twenty.
ngamia 435 na punda 6,720.
68 And, a portion of the ancestral chiefs, when they came to the house of Yahweh which was in Jerusalem, offered voluntarily for the house of God, to set it up on its basis.
Walipofika kwenye nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa jamaa walitoa sadaka za hiari kwa ajili ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika eneo lake.
69 According to their ability, gave they unto the treasury of the work, of gold, sixty-one thousand drams, and, of silver, five thousand manehs, —and, tunics for priests, one hundred.
Wakatoa kwa kadiri ya uwezo wao na kutia katika hazina darkoni 61,000 za dhahabu, mane 5,000 za fedha, na mavazi 100 ya ukuhani kwa ajili ya kazi hiyo.
70 So the priests and the Levites, and some of the people, and the singers and the doorkeepers and the Nethinim, took up their abode, in their cities, —and, all Israel, in their cities.
Makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, na watumishi wa Hekalu waliishi katika miji yao wenyewe, pamoja na baadhi ya watu wengine, nao Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao.

< Ezra 2 >