< Ezra 10 >
1 Now, when Ezra had prayed and when he had made confession, weeping and casting himself down, before the house of God, there gathered unto him out of Israel, an exceeding large convocation—men and women and children, for the people wept with a very bitter weeping.
Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama, huku akilia na kujitupa chini mbele ya nyumba ya Mungu, umati mkubwa wa Waisraeli, wanaume, wanawake na watoto walikusanyika kumzunguka. Nao pia wakalia sana.
2 Then responded Shecaniah son of Jehiel of the sons of Elam, and said unto Ezra, We, have been faithful with our God, and have married foreign women from among the peoples of the land, —yet, now, there is hope for Israel concerning this thing.
Kisha Shekania mwana wa Yehieli, mmoja wa wazao wa Elamu, akamwambia Ezra, “Tumekosa uaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni kutoka mataifa yanayotuzunguka. Lakini pamoja na hili, bado liko tumaini kwa ajili ya Israeli.
3 Now, therefore, let us solemnize a covenant unto our God—to put away all the women and such as have been born of them, in the counsel of my lord, and them who tremble at the commandment of our God, —and, according to the law, let it be done.
Sasa na tufanye agano mbele za Mungu wetu kuwafukuza hawa wanawake wote pamoja na watoto wao, kulingana na maonyo ya bwana wangu pamoja na wale ambao wanaogopa amri za Mungu wetu. Hili na lifanyike sawasawa na hii Sheria.
4 Arise, for, upon thee, resteth the thing, but, we, are with thee, —be strong, and act.
Inuka, suala hili lipo mikononi mwako. Sisi tutaungana nawe, uwe na ujasiri ukatende hili.”
5 Then arose Ezra and made the rulers of the priests, the Levites, and all Israel, swear to do according to this word—and they sware.
Basi Ezra akainuka na kuwaapisha makuhani viongozi, Walawi na Israeli yote kufanya lile lililokuwa limependekezwa. Nao wakaapa.
6 Then arose Ezra from before the house of God, and went into the chamber of Jehohanan son of Eliashib, —and, when he came thither, bread, did he not eat, and, water, did he not drink, for he was mourning over the unfaithfulness of them of the Exile.
Ndipo Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu akaenda kwenye chumba cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Wakati alipokuwa hapo, hakula chakula wala hakunywa maji, kwa sababu aliendelea kuomboleza kuhusu kukosa uaminifu kwa watu wa uhamishoni.
7 Then made they a proclamation throughout Judah and Jerusalem, unto all the Sons of the Exile, to gather themselves together unto Jerusalem;
Ndipo lilipotolewa tangazo Yuda yote na Yerusalemu kwa watu wote waliokuwa uhamishoni kukusanyika Yerusalemu.
8 and, whosoever should not come within three days, according to the counsel of the rulers and the elders, all his goods should be devoted, —and, himself, be separated from the convocation of them of the Exile.
Yeyote ambaye hangejitokeza kwa muda wa siku tatu angepoteza mali yake yote, kulingana na uamuzi wa maafisa na wazee, naye mtu huyo angefukuzwa kutoka kusanyiko la watu waliokuwa uhamishoni.
9 Then were gathered together all the men of Judah and Benjamin unto Jerusalem, within three days, the same, was the ninth month, on the twentieth of the month, —and all the people remained in the broadway of the house of God, trembling concerning the thing, and because of the heavy rains.
Katika muda wa siku tatu, watu wote wa Yuda na Benyamini wakawa wamekusanyika huko Yerusalemu. Kwenye siku ya ishirini ya mwezi wa tisa, watu wote walikuwa wameketi ndani ya uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakiwa na majonzi mno kwa tukio hilo na kwa sababu ya mvua kubwa.
10 Then arose Ezra the priest, and said unto them, Ye, have acted unfaithfully, and have married foreign women, —to add unto the guilt of Israel.
Ndipo Kuhani Ezra aliposimama akawaambia, “Mmekosa uaminifu, mmeoa wanawake wa kigeni, mkaongezea hatia ya Israeli.
11 Now, therefore, make confession unto Yahweh God of your fathers, and do his pleasure, —and separate yourselves from the peoples of the land, and from the foreign women.
Sasa tubuni kwa Bwana, Mungu wa baba zenu mkafanye mapenzi yake. Jitengeni na mataifa wanaowazunguka na wake zenu wa kigeni.”
12 Then responded all the convocation and said, with a loud voice, —Thus, according to thy word concerning us, must it be done.
Kusanyiko lote likajibu kwa sauti kubwa: “Uko sawa kabisa! Ni lazima tufanye kama unavyosema.
13 Nevertheless, the people, are many, and, the season, is that of the heavy rains, and we are not able to stand outside, —and, the business, is not one for a single day, nor yet for two, for we have abundantly transgressed, in this thing.
Lakini hapa pana watu wengi na ni wakati wa mvua, hivyo hatuwezi kusimama nje. Hata hivyo, shauri hili haliwezi kumalizika kwa siku moja au mbili, kwa sababu tumefanya dhambi kubwa katika jambo hili.
14 Let, we beseech thee, our rulers take up their station for all the convocation, and, all who, throughout our cities, have married foreign women, let them come in at times appointed, and, with them, the elders of every city, and the judges thereof, until the glow of the anger of our God be turned from us, concerning this matter.
Maafisa wetu na wafanye kwa niaba ya kusanyiko lote. Kisha kila mmoja katika miji yetu ambaye ameoa mwanamke wa kigeni aje kwa wakati uliopangwa, akiwa pamoja na wazee na waamuzi wa kila mji, hadi hasira kali ya Mungu wetu katika shauri hili itakapoondolewa kwetu.”
15 Only Jonathan son of Asahel and Jahzeiah son of Tikvah, made a stand against this, —and, Meshullam and Shabbethai the Levite, helped them.
Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa peke yao, wakiungwa mkono na Meshulamu na Shabethai Mlawi, ndio waliopinga jambo hili.
16 But the Sons of the Exile, did thus, and Ezra the priest separated to himself certain men—ancestral heads by their ancestral houses, and all of them by name, —and they took their seats on the first day of the tenth month to search into the matter;
Basi watu wa uhamishoni wakafanya kama ilivyokuwa imependekezwa. Kuhani Ezra akachagua wanaume waliokuwa viongozi wa jamaa, mmoja kutoka kila mgawanyo wa jamaa, nao wote wakachaguliwa kwa majina. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi waliketi kuchunguza mashauri hayo.
17 and they made an end with all the men who had married foreign women, —by the first day of the first month.
Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kushughulikia wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.
18 Now there were found, of the sons of the priests, who had married foreign women, —of the sons of Jeshua son of Jozadak, and his brethren, Maaseiah, and Eliezer, and Jarib, and Gedaliah;
Miongoni mwa wazao wa makuhani, wafuatao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni: Kutoka wazao wa Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zake: Maaseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia.
19 and they gave their hand, that they would put away their wives, —and, being guilty, [they offered] a ram of the flock for their guilt.
(Wote walitoa nadhiri kwa kuandika kwa mikono yao kuwafukuza wake zao, kwa hatia yao, kila mmoja akatoa kondoo dume kutoka kundini mwake kama sadaka ya hatia.)
20 And, of the sons of Immer, Hanani, and Zebadiah.
Kutoka wazao wa Imeri: Hanani na Zebadia.
21 And, of the sons of Harim, Maaseiah and Elijah and Shemaiah, and Jehiel, and Uzziah.
Kutoka wazao wa Harimu: Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli na Uzia.
22 And, of the sons of Passhur, Elioenai, Maaseiah, Ishmael, Nethanel, Jozabad, and Elasar.
Kutoka wazao wa Pashuri: Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Elasa.
23 And, of the Levites, Jozabad and Shimei, and Kelaiah, the same, is Kelita, Pethahiah, Judah, and Eliezer.
Miongoni mwa Walawi: Yozabadi, Shimei, Kelaya (ndiye Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri.
24 And, of the singers, Eliashib. And, of the doorkeepers, Shallum and Telem and Uri.
Kutoka waimbaji: Eliashibu. Kutoka mabawabu: Shalumu, Telemu na Uri.
25 And, of Israel, of the sons of Parosh, Ramiah and Izziah and Malchijah and Mijamin and Eleazar, and Malchijah, and Benaiah.
Miongoni mwa Waisraeli wengine: Kutoka wazao wa Paroshi: Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya na Benaya.
26 And, of the sons of Elam, Mattaniah, Zechariah, and Jehiel and Abdi, and Jeremoth, and Elijah.
Kutoka wazao wa Elamu: Matania, Zekaria, Yehieli, Abdi, Yeremothi na Eliya.
27 And, of the sons of Zattu, Elioenai, Eliashib, Mattaniah and Jeremoth, and Zabad, and Aziza.
Kutoka wazao wa Zatu: Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi na Aziza.
28 And, of the sons of Bebai, Jehohanan, Hananiah, Zabbai, Athlai.
Kutoka uzao wa Bebai: Yehohanani, Hanania, Zabai na Athlai.
29 And, of the sons of Bani, Meshullam, Malluch, and Adaiah, Jashub, and Sheal, Jeremoth.
Kutoka wazao wa Bani: Meshulamu, Maluki, Adaya, Yashubu, Sheali na Yeremothi.
30 And, of the sons of Pahath-moab, Adna and Chelal, —Benaiah, Maaseiah, Mattaniah, Bezalel, and Binnui, and Manasseh.
Kutoka wazao wa Pahath-Moabu: Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui na Manase.
31 And, [of] the sons of Harim, Eliezer, Isshijah, Malchijah, Shemaiah, Shimeon;
Kutoka wazao wa Harimu: Eliezeri, Ishiya, Malkiya, Shemaya, Shimeoni,
32 Benjamin, Malluch, Shemariah.
Benyamini, Maluki, na Shemaria.
33 Of the sons of Hashum, Mattenai, Mattattah, Zabad, Eliphelet, —Jeremai, Manasseh, Shimei.
Kutoka wazao wa Hashumu: Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei.
34 Of the sons of Bani, Maadai, Amram, and Uel;
Kutoka wazao wa Bani: Maadai, Amramu, Ueli,
35 Benaiah, Bedeiah, Cheluhu;
Benaya, Bedeya, Keluhi,
36 Vaniah, Meremoth, Eliashib;
Vania, Meremothi, Eliashibu,
37 Mettaniah, Mattenai, and Jaasu;
Matania, Matenai na Yaasu.
38 and Bani, and Binnui, Shimei;
Kutoka wazao wa Binui: Shimei,
39 and Shelemiah, and Nathan, and Adaiah;
Shelemia, Nathani, Adaya,
40 Machnadebai, Shashai, Sharai;
Maknadebai, Shashai, Sharai,
41 Azarel, and Shelemiah, Shemariah;
Azareli, Shelemia, Shemaria,
42 Shallum, Amariah, Joseph.
Shalumu, Amaria na Yosefu.
43 Of the sons of Nebo, Jeiel, Mattithiah, Zabad, Zebina, —Iddo, and Joel, Benaiah.
Kutoka wazao wa Nebo: Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.
44 All these, had taken foreign women, —and had begotten of them children.
Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni, na baadhi yao walikuwa wamezaa nao watoto.