< Ezekiel 39 >

1 Thou therefore son of man. Prophesy against Gog, and thou shalt say, Thus saith My Lord Yahweh: Behold me! against thee O Gog Prince of Rosh, Meshech and Tubal.
“Kisha wewe, mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! ni kinyume nawe, Gogu, mkuu wa Mesheki na Tubali.
2 Therefore will I turn thee about and lead thee on, and cause thee to come up out of the remote parts of the North, - And will bring thee in upon the mountains of Israel;
Nitakugeuza na kukuongoza; nitakupandisha juu kutoka mbali kaskazini na kukuleta hata milima ya Israeli.
3 And I will smite thy bow out of thy left hand, - And thine arrows—out of thy right hand, will I cause to fall.
Kisha nitaufunga upinde wako utoke katika mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale kuanguka kutoka kwenye mkono wako wa kuume.
4 Upon the mountains of Israel, shalt thou fall, Thou and all thy hordes, and the peoples who are with thee, — To birds of prey of every wing. and the wild beast of the field, will I give thee for food:
Utaanguka juu ya milima ya Israeli-wewe na jeshi lako late na maaskari walio pamoja nawe. Nitawapatia ndege mbua na wanyama pori wa mashambani kwa ajili ya chakula.
5 Upon the, face of the field, shalt thou fall, - For I, have spoken, Declareth My Lord Yahweh.
Utaanguka juu ya uso wa shamba, kwa kuwa mimi mwenyewe nimesema hivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
6 And I will send a fire into Magog, And among them who are dwelling in the Coastlands securely, — So shalt thou know that I am Yahweh.
Kisha nitapeleka moto juu ya Magogu na kwa wale waishio salama juu ya pwani, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
7 And my holy Name, will I make known in the midst of my people Israel, And will not suffer my holy Name to be profaned any more, — So shall the nations know that, I am Yahweh, Holy in Israel.
Kwa kuwa nitalifanya jina langu takatifu lijulikane kati ya watu wangu Israeli, na sitaruhusu tena jina langu takatifu litukanwe; mataifa watajua kwamba mimi ni Yahwe, Mtakatifu katika Israeli.
8 Lo! it is coming, and shall be brought to pass, Declareth My Lord. Yahweh, -the same, is the day whereof I had spoken.
Tazama! Siku inakuja, na itachukua nafasi-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
9 Then shall go forth the dwellers of the cities of Israel and shall make fires of the weapons and burn them, Both buckler and shield, bow and arrows, and handstaff and spear, - And shall make fires of them seven years;
Hao wakaao katika miji ya Israeli watatoka nje na watatumia silaha kuwasha moto na kutengeneza moto na kuwachoma-ngao ndogo, ngao kubwa, pinde, mishale, rungu, na mikuki; watatengeneza mioto pamoja nao kwa muda wa siku saba.
10 And they shall not take wood out of the field Neither shall they cut down out of the forests, - For of the armour, shall they make fires, - So shall they spoil those who spoiled them And prey on those who preyed on them, Declareth My Lord Yahweh.
Hawatakusanya kuni kutoka mashambani wala kukata miti kutoka kwenye misitu, kwa kuwa watazichoma hizo silaha; watawateka nyara wale watakaotaka kuwateka nyara-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
11 And it shall come to pass in that day that I will give to Gog a place of memorial for burial in Israel even the valley of them that pass through east of the sea, And it shall be enough to keep back them who would pass through, - and they shall bury there Gog and all his multitude, and shall call it Ge-hamon-gog. [That is "The valley of the multitude of Gog."]
Kisha itakuwa katika hiyo siku ambayo nitaifanya sehemu huko kwa ajili ya Gogu-kaburi la Israeli, bonde kwa ajili ya wale wanaosafiri hata mashariki ya bahari. Litawazuia wale wanaotegemea kupita. Huko watamzika Gogu pamoja na kundi lake lote. Watapaita bonde la Hamon-Gogu.
12 So shall the house of Israel bury them (that they may cleanse the land) —seven months;
Kwa muda wa siku saba nyumba ya Israeli itawazika ili kuitakasa nchi.
13 Yea all the people of the land, shall bury, and it shall become to them a memorial, —the day that I get myself glory, Declareth My Lord Yahweh.
Kwa kuwa watu wa nchi watawazika; itakuwa siku ya kukumbukwa kwao wakati nitakapotukuzwa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
14 And, men to keep at it constantly, shall they tell off Men to pass throughout the land, who with the passers-by, shall continue burying, them who have been left on the face of the land to cleanse it, — At the end of seven months, shall they make search.
Kisha watawateua watu kuendelea kwenda kwenye nchi, kuwatafuta wale waliokuwa wakisafiri, lakini waliokufa na miili yao kubaki juu ya uso wa nchi, ili kwamba waweze kuwazika, kwa ajili ya kusafisha nchi. Katika siku ya mwisho ya mwezi wa saba wataanza kutafuta.
15 And when any of the passers-by, in going through the land, shall see a human bone, then shall he set up near it a sign, —until the buriers have buried it, in Ge-hamon-Gog.
Kama hawa watu wapitao kwenye nchi, watakapoona mfupa wowote wa binadamu, wataweka alama kwa huo, hadi wachimba kaburi watakapokuja na kuizika katika bonde la Hamoni Gogu.
16 Moreover, the name of a city, shall be Hamonah ["To the multitude"] so shall they cleanse the land.
Kutakuwa na mji huko unaitwa Hamona. Wataitakasa nchi kwa njia hii.
17 Thou, therefore son of man, Thus, saith My Lord Yahweh, Say to the bird of every wing. And to every wild beast of the field. Assemble yourselves and come Gather yourselves from every side, unto my sacrifice which I am sacrificing for you A great sacrifice on the mountains of Israel, - And ye shall eat flesh and drink blood:
Kwako wewe, mwanadamu, Bwana Yahwe asema hivi: Waambie ndege wote wenye mabawa na wanyama wote wa porini katika mashamba, 'Kusanyikeni pamoja na mje. Kusanyikeni kutoka pande zote kwenda kwenye dhabihu yote ambayo mimi mwenyewe ninayoifanya kwa ajili yako, dhabihu kubwa juu ya milima ya Israeli, ili kwamba mle nyama na kunywa damu.
18 The flesh of mighty men, shall ye eat, And the blood of the princes of the earth, shall ye drink.— Rams well-fed lambs and he-goats bullocks, Fatlings of Bashan all of them;
Mtakula nyama ya walio hodari na kunywa damu ya wakuu wa dunia; watakuwa kondoo waume, wana kondoo, mbuzi, na ng'ombe, wote walikuwa wanene katika Basheni.
19 And ye shall eat fat till ye are sated, And drink blood till ye are drunken, Of my sacrifice which I have sacrificed for you;
Kisha mtakula mafuta hata kuridhika kwenu; mtakunywa damu hadi kulewa; hii itakuwa dhabihu nitakayoichinja kwa ajili yenu.
20 So shall ye be sated at my table with horse and chariot team, mighty man and every man of war, — Declareth My Lord, Yahweh.
Mtatosheka kwenye meza yangu pamoja na farasi, magari ya farasi, shujaa, na kila mtu wa vita-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
21 Thus will I set my glory among the nations, And all the nations, shall see, My judgment which I have executed, —and My hand which I have laid upon them.
Nitauweka utukufu wangu kati ya mataifa, na mataifa yote yataona hukumu yangu ninayoionyesha na mkono wangu nimeuweka juu yao.
22 So shall the house of Israel know that, I Yahweh, am their God, —from that day and forward;
Nyumba ya Israeli itajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wao kutoka hiyo siku na kuendelea.
23 And the nations shall know That in their iniquity, were the house of Israel exiled because they had committed treachery against me, And so I hid my face from them, — And gave them into the hand of their adversaries, And they fell by the sword all of them.
Mataifa yatajua kwamba nyumba ya Israeli wameenda uhamishoni kwa sababu ya udhalimu wao kwa kunisaliti, hivyo naficha uso wangu kwao na kuwaweka kwenye mkono wa maadui zao ili kwamba wote waanguke kwa upanga.
24 According to their uncleanness and according to their transgressions, dealt I with them, — And so I hid my face from them.
Nimewafanyia kutokana na uchafu wao na dhambi zao, nitakapokuwa nimeuficha uso wangu kwao.
25 Therefore— Thus saith My Lord Yahweh, Now, will I bring back them of the captivity of Jacob, And have compassion upon all the house of Israel, - And will be jealous for my holy Name;
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Sasa nitawarudisha watu wa Yakobo, na kuwa na huruma juu ya nyumba yote ya Israeli, wakati nitakapoona wivu kwa ajili ya jina langu.
26 And they shall bear their confusion, and the punishment of all their treachery wherewith they have committed treachery against me, - When they dwell upon their own soil securely, with none to make them afraid;
Kisha watabeba aibu yao na uhaini mkubwa walio nihaini. Watayasahau haya yote watakapopumzika katika nchi yao katika usalama, wala hakuna mtu atakaye waogofya.
27 When I have brought them back from among the peoples, And gathered them out of the lands of their enemies, - So will I hallow myself in them, before the eyes of the many nations;
Wakati nitakapokuwa nimewarudisha kutoka kwa watu na kuwakusanya kutoka kwenye nchi za maadui zao, nitajionyesha mimi mwenyewe kuwa mtakatifu kwenye uso wa mataifa mengi.
28 And they shall know that, I Yahweh, am their God, When I have carried them into exile among the nations, And shall then gather them upon their own soil, - And shall no more leave any of them there.
Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe Mungu wao, kwa kuwa nimewapeleka utumwani kati ya mataifa, lakini kisha nitawakusanya kuwarudisha hata nchi yao. Sitamuacha hata mmoja wao kati ya mataifa.
29 Neither will I any more hide my face from them, — In that I have poured out my spirit, upon the house of Israel, Declareth My Lord Yahweh.
Sitawaficha uso wangu kwao wakati nitakapomwaga Roho wangu katika nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”

< Ezekiel 39 >