< Ezekiel 30 >

1 And the word of Yahweh came unto me, saying:
Neno la Yahwe likanijia, kusema,
2 Son of man Prophesy. and thou shalt say, Thus saith My Lord Yahweh, — Howl ye. Alas for the day!
“Mwanadamu, toa unabii na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Maombolezo. “Ole unakuja siku hiyo.”
3 For near, is a day, Yea near, is a day pertaining to Yahweh, A day of cloud, A time of nations, shall it be!
siku ikaribu. Siku ikaribu kwa ajili ya Yahwe. Itakuwa siku ya mawingu, mda wa hukumu kwa ajili ya mataifa.
4 Then shall come a sword into Egypt, And there shall be a pang in Ethiopia When the deadly wounded one falleth in Egypt, - And they take away her multitude, and, her foundations, are broken down.
Kisha upanga utakuja dhidi ya Misri, na huko kutakuwa na maumivu makali katika Kushi wakati wauaji wa watu watakapoanguka katika Misri-wakati watakapochukua utajiri, na wakati misingi yake itakapoharibiwa.
5 Ethiopia and Libya and Lydia, and all the mixed multitude and Cub, and the sons of the land of the covenant with them—by the sword, shall they fall.
Kushi, Putu, na Ludi, na wageni wote, pamoja na watu wa nyumba ya agano-wote wataanguka chini kwa upanga.
6 Thus saith Yahweh, Then shall fall the supporters of Egypt, Then shall come down the pride of her strength, —From Migdol to Seweneh, by the sword shall they fall therein, Declareth My Lord, Yahweh.
Yahwe asema hivi: Basi wale wanaoisaidia Misri wataanguka, na kiburi cha uweza wake kitashuka chini. Kutoka Migdoli hata Sewene maaskari wao wataanguka kwa upanga-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
7 So shall they be made desolate in the midst of lands that are desolate, - And: his cities—in the midst of cities that are laid waste, shall be found.
Wataogofya kati ya nchi zilizotupwa, na miji yao itakuwa miongoni mwa miji yote iliharibika.
8 So shall they know that, I am Yahweh, - By my setting a fire in Egypt, When all her helpers shall be broken.
Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapouweka moto katika Misri, na wakati wasaidizi wake wote watakapoharibiwa.
9 In that day, shall messengers go forth from before me making haste, to cause dread unto Ethiopia so confident, - And a pang shall be upon them in the day of Egypt, For lo! it cometh.
Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele yangu katika meli ili kuitia hofu Kushi iliyo salama, na kutakuwa na maumivu makali miongoni mwao katika siku ya kuangamizwa Misri. Kwa kuwa tazama! inakuja.
10 Thus, saith My Lord Yahweh, — Therefore will I cause to cease the multitude of Egypt, by the hand of Nebuchadrezzar king of Babylon:
Bwana Yahwe asema hivi: Nitaufanya mwisho wa watu wa Misri kwa mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
11 He, and his people with him the terrible ones of the nations are about to be brought in to destroy the land, - Therefore shall they unsheathe their swords against Egypt, and fill the land with the slain;
Yeye na jeshi lake pamoja naye, hofu ya mataifa, italetwa kuiharibu nchi; watafuta panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi pamoja na watu waliokufa.
12 And I will make the rivers dry, and will sell the land into the hand of wicked one.—and make the land desolate with the fulness thereof, by the hand of foreigners, I, Yahweh! have spoken.
Nitaifanya mito kuwa nchi kavu, na nitaiuza nchi kwenye mkono wa watu waovu. Nitaifanya nchi na viijazavyo ukiwa kwa mkono wa wageni-mimi, Yahwe, nimesema.
13 Thus saith My Lord Yahweh, Therefore will I destroy the manufactured gods and Cause to cease the worthless goals, out of Noph, And prince out of the land of Egypt, shall none arise any more, - And I will cause fear in the land of Egypt.
Bwana Yahwe asema hivi: Nitaziharibu sanamu, na nitaleta mwisho wa sanamu za ubatili za Nofu. Hakutakuwa na mkuu katika Misri, na nitaweka hofu katika nchi ya Misri.
14 Then will I bring desolation upon Pathros, and Set a fire in Zoan, and Execute judgments upon No: and
Kisha nitaifanya Pathrosi ukiwa na kuweka moto katika Soani, nitatekeleza matendo ya hukumu katika No.
15 Pour out mine indignation upon Sin the stronghold of Egypt, and Will cut off the multitude of No.
Kwa kuwa nitamwaga ghadhabu yangu juu Sini, ngome ya Misri, na kuwakatilia mbali watu wa mataifa.
16 So will I set a fire in Egypt, Sore anguish shall take Sin. And, No, shall be for rending asunder, And Noph, be in straits every day,
Kisha nitaweka moto katika Misri; Sini itakuwa katika dhiki kuu, No itavunjika, na Nofu itakabiliana na maadui kila siku.
17 The young men of Aven and Pi-beseth, by the sword, shall fall; And lo! into captivity, shall they themselves wend their way.
Vijana katika Oni na Pi-besethi wataanguka kwa upanga, na miji yao itaenda utumwani.
18 And in Tehaphnehes, hath the day become dark, Because I have broken, there the yoke-bars of Egypt, And there shall be made to cease therein the pride of her strength, — She, a cloud, shall cover her! And her daughters into captivity, shall wend their way.
Huko Tapanesi, siku itabadilika kuwa usiku nitakapo ivunja nira ya Misri huko, na kiburi cha uwezo wake kitaisha. Kutakuwa na wingu likimfunika, na binti zake wataenda utumwani.
19 Thus will I execute judgments on Egypt; And they shall know that, I, am Yahweh.
Nitatekeleza matendo ya hukumu katika Misri, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
20 And it came to pass in the eleventh year in the first month on the seventh of the month, that the word of Yahweh came unto me saying:
Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, katika siku ya saba ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
21 Son of man, The arm of Pharaoh king of Egypt, have I broken, - And lo! it hath not been bound up-To apply healing remedies To put on a bandage for binding it up. To make it strong to grasp the sword.
“Mwanadamu, nimeuvunja mkono wa Farao, mfalme wa Misri. Tazama! Haukufungwa, au kufungwa kwa kitambaa cha bendeji ili upone, hivyo basi uweze kuwa imara kushika upanga.
22 Therefore, Thus, saith My Lord Yahweh-Behold me! against Pharaoh king of Egypt, Therefore will I break his arms, That which is strong, and That which is broken, - So will I cause the sword to fall out of his hand.
Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama, mimi niko juu ya Farao, mfalme wa Misri. Kwa kuwa nitauvunja mkono wake, wote yule aliye hodari na yule aliyevunjika, nitaufanya upanga wangu kuanguka kutoka kwenye mkono wake.
23 And I will disperse the Egyptians among the nations, — And scatter them throughout the lands;
Kisha nitaitawanya Misri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbali mbali.
24 And will uphold the arms of the king of Babylon, And put my sword into his hand, - And will break the arms of Pharaoh, And he shall utter the groans of one thrust through, before him.
Nitaunyoosha mikono kwa mfalme wa Babeli na kuweka upanga wangu katika mkono wake ili kwamba niweze kuiharibu mikono ya Farao. Atagugumia mbele ya mfalme wa Babeli kwa mgumio wa mtu anayekufa.
25 Yea I will uphold the arms of the king of Babylon, But the arms of Pharaoh shall fall, And they shall know that I am Yahweh By my putting my sword into the hand of the king of Babylon, And he shall stretch it out against the land of Egypt.
Kwa kuwa nitainyoosha mikono ya mfalme wa Babeli, wakati mkono wa Farao utakapoanguka. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapoweka upanga wangu kwenye mkono wa mfalme wa Babeli; kwa kuwa ataishambulia nchi ya Misri kwa huo.
26 So will I disperse the Egyptians among the nations, And scatter them throughout the lands, And they shall know that, I, am Yahweh.
Hivyo nitaitawanya miongoni mwa mataifa na kuyatawanya kwenye nchi tofauti tofauti. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe.”'

< Ezekiel 30 >