< Ezekiel 29 >
1 In the tenth year, in the tenth month, on the twelfth of the month, came the word of Yahweh unto me, saying:
Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la Bwana likanijia kusema:
2 Son of man, Set thy face against Pharaoh, king of Egypt, And prophesy against him, and against Egypt all of it:
“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote.
3 Speak, and thou shalt say— Thus, saith My Lord Yahweh Behold me! against thee O Pharaoh king of Egypt, The great Crocodile that lieth along in the midst of his rivers: Who saith— My river is, mine own, Since I myself made it me!
Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri, joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako. Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe; niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.”
4 Therefore will I put hooks in thy jaws, And cause the fish of thy rivers to stick fast in thy scales, - And will bring thee up out of the midst of thy rivers, And, all the fish of thy rivers, to thy scales, shall stick fast;
Lakini nitatia ndoana katika mataya yako nami nitawafanya samaki wa vijito vyako washikamane na magamba yako. Nitakutoa katikati ya vijito vyako, pamoja na samaki wote walioshikamana na magamba yako.
5 And I will stretch thee out towards the desert, Thee and all the fish of thy rivers, On the face of the field, shalt thou lie Thou shalt not be carried away nor shalt thou be gathered, To the wild beast of the earth and to the bird of the heavens, have I given thee for food.
Nitakutupa jangwani, wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako. Utaanguka uwanjani, nawe hutakusanywa au kuchukuliwa. Nitakutoa uwe chakula kwa wanyama wa nchi na ndege wa angani.
6 So shall all the inhabitants of Egypt know that I, am Yahweh, Because they were a staff of reed to the house of Israel:
Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli.
7 Whensoever they took hold of thee by the hand, thou didst run through, and tear open for them every hand, —And whensoever they leaned upon thee, thou didst break, and caused all their loins to halt.
Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka.
8 Therefore, Thus saith My Lord Yahweh, Behold me! bringing upon thee a sword, - And I will cut off out of thee, man and beast;
“‘Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao.
9 And the land of Egypt shall become an astonishment and a desolation, So shall they know that, I, am Yahweh, —Because he said— The river is mine own, Since, I, myself made it!
Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana. “‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,”
10 Therefore, behold me! against thee and against thy rivers, - And I will make the land of Egypt to be most desolate an astounding desolation, from Migdol to Syene even up to the boundary of Ethiopia:
kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia.
11 The foot of man shall not pass through it, Nor shall the foot of beast, pass through it, Neither shall it be inhabited forty years:
Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini.
12 So will I make the land of Egypt a desolation in the midst of lands made desolate And her cities—in the midst of cities that have been laid waste, shall become a desolation forty years, - And I will disperse the Egyptians among the nations, And scatter them throughout the lands.
Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine.
13 For thus, saith My Lord Yahweh, — At the end of forty years, will I gather the Egyptians from among the peoples whither I had dispersed them;
“‘Lakini hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa.
14 And I will turn the captivity of the Egyptians, And will cause them to return To the land of Pathros Upon the land of their nativity, - And they shall become, there a kingdom abased:
Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu.
15 More than [any of] the kingdoms, shall she be abased, And shall lift herself up no more over the nations, —Yea I will make them too small to rule over the nations.
Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine.
16 So shall it become no more unto the house of Israel a security. Calling to mind iniquity, by their turning to follow them, - And they shall know that, I, am The Lord Yahweh.
Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana Mwenyezi.’”
17 And it came to pass in the twenty-seventh year in the first month on the first of the month, that the word of Yahweh came unto me saying:
Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la Bwana likanijia, kusema:
18 Son of man Nebuchadrezzar king of Babylon, hath made his army undergo a long service against Tyre, Every head, hath been made bald, and, Every shoulder, worn bare, — But pay, hath he had none nor hath his army, out of Tyre, for the service wherewith he hath served against it.
“Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro.
19 Therefore, Thus, saith My Lord Yahweh, Behold me! giving to Nebuchadrezzar king of Babylon, the land of Egypt, — And he shall carry off her multitude And capture her spoil And seize her prey, So shall she become pay for his army.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake.
20 As a reward for his labour wherewith he hath served, have I given to him the land of Egypt, —in that they wrought for me, Declareth My Lord, Yahweh.
Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema Bwana Mwenyezi.
21 In that day, will I cause to bud a horn for the house of Israel, And to thee, will I give an opening of mouth in their midst, So shall they know that, I, am Yahweh.
“Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”