< Exodus 7 >

1 Then said Yahweh unto Moses—See! I have appointed thee to be God unto Pharaoh, —and, Aaron thy brother, shall be thy prophet!
Yahweh akasema na Musa, “Ona, nimekufanya kama mungu kwa Farao. Aruni kaka yako atakuwa nabii wako.
2 Thou, shalt speak all that which I may command thee, and, Aaron thy brother, shall speak unto Pharaoh, and he shall let the sons of Israel go out of his land.
Utasema kila kitu nitacho kuamuru kusema. Aruni kaka yako ata sema na Farao iliawaachie watu wa Israeli watoke kwenye nchi yake.
3 But, I, will suffer Pharaoh to harden his heart, —so will I multiply my signs and my wonders in the land of Egypt.
Lakini nitaufanya moyo wa Farao mgumu, na nitaonyesha ishara nyingi za nguvu zangu, maajabu mengi, katika nchi ya Misri.
4 And Pharaoh will not hearken unto you, so will I lay my hand on Egypt, —and bring forth my hosts—my people the sons of Israel out of the land of Egypt, with great judgments.
Lakini Farao hata kusikiliza, kwahiyo nitaueka mkono wangu juu ya Misri na kutoa makundi yangu ya wanaume wapiganaji, watu wangu, wazao wa Israeli, watoke nchi ya Misri kwa matendo makubwa ya hukumu.
5 And the Egyptians shall know that I, am Yahweh, when I have stretched forth my hand over Egypt, —and brought forth the sons of Israel out of their midst.
Wamisri watajua kuwa mimi ni Yahweh nitapo nyoosha mkono wangu kwa Misri na kuwatoa Waisraeli kutoka miongoni mwao.”
6 And Moses and Aaron did [so], —as Yahweh commanded them, so, did they.
Musa na Aruni wakafanya hivyo; walifanya kama Yahweh alivyo waamuru.
7 Now Moses, was eighty years old, and, Aaron, eighty-three years old, —when they spake unto Pharaoh.
Musa alikuwa na miaka themanini, na Aruni miaka themanini na tatu walipo ongea na Farao.
8 And Yahweh spake unto Moses and unto Aaron saying:
Yahweh akamwambia Musa na Aruni,
9 When Pharaoh shall speak unto you saying, Shew for yourselves a wonder, then shalt thou say unto Aaron, Take thy staff, and cast it down before Pharaoh let it become a sea-serpent.
“Wakati Farao atakapo waambia, 'Fanya muujiza,' utamwambia Aruni, 'Chukuwa gongo lako na ulirushe chini mbele ya Farao, ililigeuke nyoka.”'
10 So Moses and Aaron went in unto Pharaoh, and did so as Yahweh had commanded, —and Aaron cast down his staff before Pharaoh and before his servants and it became a sea-serpent,
Kisha Musa na Aruni wakaenda kwa Farao, na wakafanya kama Yahweh alivyo waamuru. Aruni akarusha chini gongo lake mbele ya Farao na watumishi wake, na likageuka nyoka.
11 Then called Pharaoh also for the wise men and for the magicians, —and they too, the sacred scribes of Egypt with their secret arts, did in like manner;
Kisha naye Farao akawaita wazee wenye hekima na wachawi. Wakafanya jambo hilo hilo kwa uchawi wao.
12 yea they cast down each man his staff, and they became sea-serpents, —but Aaron’s staff swallowed up their staves.
Kila mtu akarusha chini gongo lake, na magongo yakawa nyoka. Lakini gongo la Aruni lilimeza nyoka zao.
13 Then waxed bold the heart of Pharaoh, and he hearkened not unto them, —as spake Yahweh.
Moyo wa Farao ulikuwa mgumu, na akusikiliza, kama Yahweh alivyo tabiri.
14 Then said Yahweh unto Moses, Dull, is the heart of Pharaoh, —he hath refused to let the people go.
Yahweh akasema na Musa, “Moyo wa Farao ni mgumu, na anakataa kuacha watu waende.
15 Get thee unto Pharaoh in the morning—lo! he is coming out to the waters, therefore shalt thou station thyself to meet him on the bank of the river, —and the staff which was turned into a serpent, shalt thou take in thy hand.
Nenda kwa Farao asubui anapoenda kwenye maji. Simama kwenye chanzo cha mto kukutana naye, na uchukuwe mkononi mwako gongo ambalo liligeuka nyoka.
16 Then shalt thou say unto him—Yahweh God of the Hebrews hath sent me unto thee saying, —Let my people go, that they may serve me in the desert, —And lo! thou hast not hearkened hitherto.
Mwambie, 'Yahweh, Mungu wa Waebrania, amenituma kwako, “Acha watu wangu waende, iliwaniabudu nyikani. Mpaka sasa haujanisikiliza.”
17 Thus, saith Yahweh, Hereby, shalt thou know that, I, am Yahweh, —Lo! I, am smiting with the staff that is in my hand upon the waters that are in the river and they shall be turned to blood;
Yahweh anasema hili: “Kwa hili utajua kuwa mimi ni Yahweh. Ninaenda kupiga maji ya mto wa Misri kwa gongo langu lililo mikono mwangu, na mto utageuzwa kuwa damu.
18 and, the fish that is in the river shall die and the river shall be loathsome, —and the Egyptians, shall disdain, to drink water out of the river.
Samaki walio kwenye mto watakufa, na mto utanuka. Wa Misri Hawataweza kunywa maji yalio kwenye mto.”'''
19 And Yahweh said unto Moses, —Say unto Aaron—Take thy staff, and stretch forth thy hand over the waters of Egypt, over their streams over their rivers, and over their pools and over all their collections of water—that they may become blood, —so shall there be blood in all the land of Egypt, both in vessels of wood and in vessels of stone.
Kisha Yahweh akasema na Musa, “Mwambie Aruni, 'Chukuwa gongo lako na unyooshe mkono kwenye maji ya Misri, na juu ya mito yake, mifereji, visima, na madimbwi yote, ili maji yao ya damu. Fanya hivi ilikuwe na damu nchi nzima ya Misri, hadi kwenye vyombo vyote vya mbao na mawe.”'
20 And Moses and Aaron, did so, as Yahweh commanded, and he lifted high the staff, and smote the waters which were in the river, before the eyes of Pharaoh, and before the eyes of his servants, —and all the waters which were in the river were turned to blood;
Musa na Aruni walifanya kama Yahweh alivyo waamuru. Aruni alinyanyua gongo na kupiga maji ya mto, machoni pa Farao na watumishi wake. Maji yote kwenye mto yaligeuga damu.
21 and the fish that was in the river, died and the river became loathsome, so that the Egyptians could not drink water out of the river, —thus came it to pass that blood was in all the land of Egypt.
Samaki kwenye mto wakafa, na mto ukaanza kunuka. Wamisri hawakuweza kunywa maji kwenye mto, na damu ilikuwa kila mahali katika nchii ya Misri.
22 And the sacred scribes of Egypt did in like manner with their secret arts, —so the heart of Pharaoh waxed bold and he hearkened not unto them, as spake Yahweh.
Lakini wachawi walifanya vivyo hivyo na uchawi wao. Kwaiyo moyo wa Farao ukawa mgumu, na akakataa kuwasikiliza Musa na Aruni, kama Yahweh alivyo sema itatokea.
23 Then Pharaoh, turned away, and entered into his house—neither applied he his heart, even to this.
Kisha Farao akarudi na kwenda nyumbani kwake. Wala hakutilia maanani hili.
24 And all the Egyptians digged round about the river for water to drink, —for they could not drink of the water of the river.
Wamisri wote walichimba pembeni ya mto kwa ajili ya maji ya kunywa, lakini hawakuweza kunywa maji ya mto.
25 And seven days were fulfilled, —after Yahweh had smitten the river.
Siku saba zilipita baada ya Yahweh kushambulia mto.

< Exodus 7 >