< Exodus 7 >

1 Then said Yahweh unto Moses—See! I have appointed thee to be God unto Pharaoh, —and, Aaron thy brother, shall be thy prophet!
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
2 Thou, shalt speak all that which I may command thee, and, Aaron thy brother, shall speak unto Pharaoh, and he shall let the sons of Israel go out of his land.
Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
3 But, I, will suffer Pharaoh to harden his heart, —so will I multiply my signs and my wonders in the land of Egypt.
Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
4 And Pharaoh will not hearken unto you, so will I lay my hand on Egypt, —and bring forth my hosts—my people the sons of Israel out of the land of Egypt, with great judgments.
hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
5 And the Egyptians shall know that I, am Yahweh, when I have stretched forth my hand over Egypt, —and brought forth the sons of Israel out of their midst.
Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
6 And Moses and Aaron did [so], —as Yahweh commanded them, so, did they.
Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
7 Now Moses, was eighty years old, and, Aaron, eighty-three years old, —when they spake unto Pharaoh.
Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
8 And Yahweh spake unto Moses and unto Aaron saying:
Bwana akamwambia Mose na Aroni,
9 When Pharaoh shall speak unto you saying, Shew for yourselves a wonder, then shalt thou say unto Aaron, Take thy staff, and cast it down before Pharaoh let it become a sea-serpent.
“Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
10 So Moses and Aaron went in unto Pharaoh, and did so as Yahweh had commanded, —and Aaron cast down his staff before Pharaoh and before his servants and it became a sea-serpent,
Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
11 Then called Pharaoh also for the wise men and for the magicians, —and they too, the sacred scribes of Egypt with their secret arts, did in like manner;
Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
12 yea they cast down each man his staff, and they became sea-serpents, —but Aaron’s staff swallowed up their staves.
Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
13 Then waxed bold the heart of Pharaoh, and he hearkened not unto them, —as spake Yahweh.
Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
14 Then said Yahweh unto Moses, Dull, is the heart of Pharaoh, —he hath refused to let the people go.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
15 Get thee unto Pharaoh in the morning—lo! he is coming out to the waters, therefore shalt thou station thyself to meet him on the bank of the river, —and the staff which was turned into a serpent, shalt thou take in thy hand.
Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
16 Then shalt thou say unto him—Yahweh God of the Hebrews hath sent me unto thee saying, —Let my people go, that they may serve me in the desert, —And lo! thou hast not hearkened hitherto.
Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
17 Thus, saith Yahweh, Hereby, shalt thou know that, I, am Yahweh, —Lo! I, am smiting with the staff that is in my hand upon the waters that are in the river and they shall be turned to blood;
Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
18 and, the fish that is in the river shall die and the river shall be loathsome, —and the Egyptians, shall disdain, to drink water out of the river.
Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
19 And Yahweh said unto Moses, —Say unto Aaron—Take thy staff, and stretch forth thy hand over the waters of Egypt, over their streams over their rivers, and over their pools and over all their collections of water—that they may become blood, —so shall there be blood in all the land of Egypt, both in vessels of wood and in vessels of stone.
Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
20 And Moses and Aaron, did so, as Yahweh commanded, and he lifted high the staff, and smote the waters which were in the river, before the eyes of Pharaoh, and before the eyes of his servants, —and all the waters which were in the river were turned to blood;
Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
21 and the fish that was in the river, died and the river became loathsome, so that the Egyptians could not drink water out of the river, —thus came it to pass that blood was in all the land of Egypt.
Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
22 And the sacred scribes of Egypt did in like manner with their secret arts, —so the heart of Pharaoh waxed bold and he hearkened not unto them, as spake Yahweh.
Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
23 Then Pharaoh, turned away, and entered into his house—neither applied he his heart, even to this.
Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
24 And all the Egyptians digged round about the river for water to drink, —for they could not drink of the water of the river.
Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
25 And seven days were fulfilled, —after Yahweh had smitten the river.
Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.

< Exodus 7 >