< Exodus 5 >

1 And afterwards, Moses and Aaron went in and said unto Pharaoh, —Thus, saith Yahweh God of Israel, Let my people go, that they may hold a festival to me in the desert.
Baada ya mambo haya kutokea, Musa na Aruni walienda kwa Farao na kumwambia, ““Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Israeli anasema: 'Waache watu wangu waende, ili wapate kunifanyia karamu jangwani.'”
2 Then said Pharaoh, Who is Yahweh that I should hearken to his voice, to let Israel go? I know not Yahweh, and certainly. Israel, will I not let go!
Farao akasema, “Yahwe ni nani? Kwa nini mimi nisikiliz sauti yake na kuwaacha Israeli waende? Mimi simjui Yahwe; na la zaidi, sitawaacha Israeli waende.”
3 And they said, the God of the Hebrews, hath met with us, —let us go, we pray thee, a journey of three days into the desert and sacrifice to Yahweh our God, lest he fall upon us with pestilence or with sword.
Wakasema, “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Tuache twende safari jangwani kwa siku tatu ili tutoe sadaka kwa Yahwe Mungu wetu ili asituadhibu kwa mapigo au kwa upanga.”
4 And the king of Egypt said unto them, Wherefore O Moses and Aaron should ye loose the people from their works? Get you to your burdens.
Lakini mfalme wa Misri aliwaambia, “Musa na Aruni, kwa nini mnawatoa watu kazini mwao? Nendeni kazini kwenu.”
5 And Pharaoh said, Lo! many—now, are the people of the land, —and are ye to make them rest from their burdens?
Pia alisema, “Sasa kuna Waebrania wengi nchini mwetu, na ninyi mnawafanya waache kazi zao.”
6 So then Pharaoh gave command on that day, unto the taskmasters over the people and unto their overseers—saying:
Siku ile ile, Farao alitoa amri kwa wasimamizi na wanyapara wa wale watu. Akasema,
7 Ye shall no more give straw unto the people, for making the bricks as heretofore: Let them, go, themselves, so shall they gather for themselves straw:
“Tofauti na ilivyokuwa mwanzo, “Tofauti ni ilivyokuwa awali, msiwapatie tena watu majani ya kutengenezea tofali. Waacheni wao waende kujitafutia majani wenyewe.
8 Nevertheless, the fixed number of bricks, which they have been making heretofore, shall ye lay upon them, ye shall not diminish therefrom, —for idle, they are, on this account, it is that they are making an outcry, saying, We must go our way, we must sacrifice to our God.
Ingawa wanapaswa kuleta hesabu sawa ya matofali watakayotengeneza kama ilivyokuwa awali. Msipokee pungufu, kwasababu wao ni wavivu. Ndiyo maana wanapiga kelele na kusema, 'turuhusu tuende tukamtolee sadaka Mungu wetu.'
9 The service must be made heavy on the men that they may labour on it, —and let them not pay regard to words of falsehood.
Waongezeeni kazi wanaume ili wasipate tena muda wa kusikiliza maneno ya upotoshaji.”
10 Then went forth the taskmasters of the people and their overseers, and spake unto the people, —saying, —Thus, saith Pharaoh, I am not going to give you straw,
Kwa hiyo viongozi wa watu na waangalizi wao waliwajulisha watu. Walisema, “Hivi ndivyo farao amesema: 'Sitawapeni tena malighafi.
11 Ye yourselves go fetch you straw, of any ye can find, —yet hath there not been diminished from your service a single thing.
Nyinyi wenyewe mtaenda kutafuta majani popote mtakapopata, lakini kazi zenu hazitapunguzwa.
12 So the people dispersed themselves throughout all the land of Egypt, —to gather stubble for straw:
Basi watu hao wakatawanyika katika nchi yote ya Misri ili wapate kukusanya matakataka badala ya majani.
13 the taskmasters, meanwhile, being urgent saying, —Complete your works, The task of a day, in its day, as when the straw was provided.
Wasimamizi wao wakawahimiza na kusema, “Malizeni kazi zenu, sawa na wakati ule majani yalipokuwapo.”
14 Then were beaten the overseers of the sons of Israel, whom the taskmasters of Pharaoh had set over them saying: Wherefore have ye not completed your task for making bricks, as heretofore, so also, yesterday and, to-day?
Wanyapara wa Farao wakawapiga wasimamizi wa Waisraeli, watu walewale ambao waliwaweka kuwa wasimamizi wa watumishi. Wale Wanyapara wakakazana kuwauliza, “Kwanini hamjatimiza idadi ya matofali inayotakiwa kwenu, siku ya jana na hata leo kama ambavyo mlifanya siku za nyuma?”
15 Then came in the overseers of the sons of Israel, and made outcry unto Pharaoh, saying, Wherefore shouldst thou do thus to thy servants?
Basi Wanyapara wa wana wa Israeli wakamwendea Farao na kumlilia. Walisema, “Kwanini unawatendea watumishi wako hivi?
16 No straw, is given to thy servants, yet bricks, —they keep saying to us—make ye! And lo, thy servants, are beaten—thou dost, therefore, wrong thy people.
Sisi watumishi wako hatupewi majani tena, lakini bado wanatuambia sisi, “Tengenezeni tofali!' Sisi watumwa wako tunapigwa sasa, lakini kosa hilo ni la watu wako.”
17 But he said: Idle, ye are—idle, on this account, are, ye, saying, We must take our journey, we must sacrifice to Yahweh.
Lakini Farao akasema, “Ninyi ni wavivu! Wavivu ninyi! Ninyi mwasema, 'Turuhusu twende kumtolea Yahwe sadaka.'
18 Now, therefore, go labour, but, straw, shall not be given you, —yet the tale of bricks, shall ye render.
Sasa rudini kazini. Hamtapewa majani tena, lakini mnapaswa kutengeneza idadi ile ile ya matofali.”
19 Then did the overseers of the sons of Israel see themselves to be in an evil case, when it was said, —Ye shall not diminish from your bricks—the task of a day, in its day
Wanyapara wa wana wa Israeli wakagundua ya kuwa walikuwa kwenye shida kubwa mara walipoambiwa, “Hamtapunguza kamwe idadi ya matofali mnayotengeneza kila siku.”
20 So they fell upon Moses and upon Aaron, stationing themselves to meet them, —as they came forth from Pharaoh;
Wakakutana na Musa na Haruni, waliokuwa wamesimama nje ya Ikulu wakati wanatoka kwa Farao.
21 and they said unto them, Yahweh look upon you and judge, —in that ye have made us odious in the eyes of Pharaoh and in the eyes of his servants, putting a sword into their hand to slay us.
Wakawaambia Musa na Haruni, “Yahwe awatazame ninyi na kuwaadhibu, kwa sababu mmetufanya sisi kuonekana wabaya mbele ya Farao na watumishi wake. Mmetia upanga mikononi mwao ili watuue.”
22 And Moses returned unto Yahweh and said, —O My Lord wherefore hast thou caused harm to this people? Wherefore now didst thou send me?
Musa akarudi kwa BWANA na kumwambia, “Bwana, kwanini umewatenda mabaya watu hawa? Kwanini kunituma mimi kwanza?
23 seeing that from what time I came in unto Pharaoh to speak in thy name, he hath done harm to this people, and thou hast not delivered, thy people,
Tangu nilipokuja kwa Farao kusema naye kwa jina lako, amewatenda mabaya watu hawa, wala hujawaokoa watu wako hata kidogo.”

< Exodus 5 >