< Exodus 36 >

1 Thus shall Bezaleel and Oholiab work, and every man that is wise-hearted, in whom Yahweh hath put wisdom and understanding, to know how to work any manner of workmanship for the holy service, —according to all that Yahweh hath commanded.
Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu Bwana aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile Bwana alivyoagiza.”
2 So then Moses called upon Bezaleel, and upon Oholiab, and upon every man that was wise-hearted, in whose heart Yahweh had put wisdom, —every one whose heart lifted him up, to draw near unto the work, to do it.
Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye Bwana alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi.
3 And they took, from the presence of Moses, all the heave-offering which the sons of Israel had brought in for the work of the holy service to do it, —howbeit, they, brought in unto him yet more free-will offerings, morning by morning.
Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi.
4 Then came in all the wise men who were doing all the holy work, —man by man from his work which, they, were doing;
Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao,
5 and spake unto Moses, saying, More than enough, are the people bringing in, —[more] than is needed for the service pertaining to the work; which Yahweh hath commanded to be done.
wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo Bwana ameagiza ifanyike.”
6 So Moses gave commandment and they passed a proclamation throughout the camp, saying, Let, neither man nor woman, make any more material for the holy heave-offering. So the people were restrained from bringing in.
Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi,
7 For the material was enough for all the work, to make it, —and to spare.
kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.
8 Then did all the wise-hearted among the workers of the material make the habitation of ten curtains, of fine-twined linen, and blue and purple and crimson, with cherubim the work of the skilful weaver, did he make them.
Watu wote wenye ustadi miongoni mwa wafanyakazi wote wakatengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye mapazia hayo.
9 The length of each curtain, was twenty-eight cubits, and the breadth four cubits, for each curtain, —one measure, had all the curtains.
Mapazia yote yalitoshana kwa ukubwa: kila moja lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
10 And he joined the [first] five curtains, one to another, —and the [other] five curtains, joined he one to another,
Wakayaunganisha mapazia matano pamoja, pia wakafanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
11 And he made loops of blue upon the border of the first curtain, at the edge of the set, —thus, made he in the border of the other curtain at the edge of the second set:
Kisha wakatengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, pia wakafanya vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
12 Fifty loops, made he in the first curtain, and fifty loops, made he in the edge of the curtain that was in the second set, —the loops being, opposite, one to another.
Wakatengeneza pia vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vikaelekeana.
13 And he made fifty clasps of gold, —and joined the curtains one to another with the clasps, and so the habitation became, one.
Kisha wakatengeneza vifungo hamsini vya dhahabu, na wakavitumia kufunga na kuunganisha zile fungu mbili za mapazia pamoja ili maskani ipate kuwa kitu kimoja.
14 And he made curtains of goat’s-hair, for the tent over the habitation, eleven curtains, did he make them:
Wakatengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
15 the length of each curtain, was thirty cubits, and, four cubits, was the breath of each curtain, —one measure, had the eleven curtains.
Mapazia hayo kumi na moja yalikuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
16 And he joined five of the curtains by themselves, —and the six curtains, by themselves.
Wakaunganisha mapazia matano kuwa fungu moja, na hayo mengine sita kuwa fungu lingine.
17 And he made fifty loops upon the border of the curtain that was outmost in the one set and fifty loops, made he upon the border of the curtain of the second set.
Kisha wakatengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
18 And he made fifty clasps of bronze, —to join together the tent, that it might become one.
Wakatengeneza vifungo hamsini vya shaba ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
19 And he made a covering to the tent, of rams’ skins dyed red, —and a covering of badgers’ skins, above.
Kisha wakatengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
20 And he made the boards for the habitation, of acacia wood, for standing up:
Wakatengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
21 ten cubits, the length of each board, and a cubit and a half the breadth of each board:
Kila mhimili ulikuwa na urefu wa dhiraa kumi, na upana wa dhiraa moja na nusu,
22 two tenons to each board, united one to another, —thus, made he for all the boards of the habitation.
zikiwa na ndimi mbili zilizokuwa sambamba kila mmoja na mwingine. Wakatengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
23 And he made the boards for the habitation, twenty boards, for the south side southwards;
Wakatengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
24 and, forty sockets of silver, made he, under the twenty boards, two sockets, under the first board, for its two tenons, and, two sockets, under the next board for its two tenons.
na wakatengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
25 And for the second side of the habitation to the north quarter, made he twenty boards;
Kwa upande wa kaskazini wa maskani wakatengeneza mihimili ishirini
26 and their forty sockets of silver, two sockets, under the first board, and, two sockets, under the next board.
na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
27 And, for the hinder part of the habitation westward, made he six boards;
Wakatengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
28 and two boards, made he for the corners of the habitation, —in the hinderpart.
na mihimili miwili ikatengenezwa kwa ajili ya pembe za maskani za upande uliokuwa mbali.
29 Thus were they to be double beneath, and at the same time, should they be entire, at the top thereof, into each ring, thus, did he for them both, for the two corners.
Katika pembe hizi mbili mihimili yake ilikuwa miwili kuanzia chini mpaka juu, na ikaingizwa kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili ilifanana.
30 Thus were there to be eight boards, and, their sockets of silver, were sixteen sockets, two sockets apiece under each board.
Kwa hiyo kulikuwa na mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
31 And he made bars of acacia wood, —five, for the boards of the first side of the habitation,
Wakatengeneza pia mataruma kwa mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
32 and five bars, for the boards of the other side of the habitation, and, five bars, for the boards of the habitation at the hinderpart westward.
matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
33 And he made the middle bar, —to run along in the midst of the boards, from end to end.
Wakatengeneza taruma la katikati, likapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
34 And the boards, overlaid he with gold and their rings, made he of gold, as receptacles for the bars, and he overlaid the bars with gold.
Wakaifunika hiyo mihimili kwa dhahabu, na wakatengeneza pete za dhahabu za kushikilia hayo mataruma. Pia wakayafunika hayo mataruma kwa dhahabu.
35 And he made the veil, of blue and purple and crimson and fine-twined linen, —of the work of a skilful weaver, made he it, with cherubim.
Wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi akatirizi makerubi kwenye hilo pazia.
36 And he made for it four pillars of acacia, and overlaid them with gold their hooks of gold, and cast for them, four sockets of silver.
Wakatengeneza nguzo nne za mti wa mshita kwa ajili yake na kuzifunika kwa dhahabu. Wakatengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya nguzo hizo, na kusubu vitako vinne vya fedha.
37 And he made a screen for the opening of the tent, of blue and purple and crimson and fine twined linen, the work of an embroiderer;
Kwa ajili ya ingilio la hema wakatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
38 and the five pillars thereof and their hooks, and he overlaid their capitals and their cross-rods, with gold, but, their five sockets, were of bronze.
Pia wakatengeneza nguzo tano zenye kulabu. Wakafunika ncha za juu za hizo nguzo pamoja na tepe zake kwa dhahabu, na pia wakatengeneza vitako vyake vitano vya shaba.

< Exodus 36 >