< Exodus 21 >

1 Now, these are the regulations which thou shalt put before them.
Sasa hizi ni amri utakazoweka kabla yao:
2 When thou shalt acquire a servant who is a Hebrew, six years, shall he serve, —but in the seventh shall he go out freely—for nought.
'kama mtanunua mtumishi wa kiebrania, atatumikia kwa miaka sita, na mwaka wa saba ataachiwa huru bila kilipwa chochote.
3 If, by himself, he came in, by himself, shall he go out, —if he was married, then shall his wife go out with him.
Kama alikuja mwenyewe, ataenda huru kwa ridhaa yake;
4 If his lord gave him a wife, and she have borne him sons or daughters, the wife and her children shall be her lords, and, he shall go out by himself.
kama bwana wake atampa mke na kumzalia mwana na binti, mke pamoja na watoto wake watabaki mali ya bwana wake, na ataenda zake huru.
5 But, if the servant shall plainly say, I love my lord, and my wife and my sons, —I will not go out free,
Lakini kama mtumishi atasema waziwazi, “Nampenda bwana wangu, mke wangu, na watoto; sitaenda nje,”
6 then shall his lord bring him near unto God, and shall bring him near unto the door, or unto the door-post, —and his lord shall pierce his ear with an awl, so shall he serve him all his life.
“kisha bwana wake atapaswa kumleta kwa Mungu. Bwana wake atapaswa kumleta katika mlango au katika muhimili wa mlango, na bwana wake atatoboa sikio lake na sindano. Kisha mtumishi wake atamtumikia kwa maisha yake yote.
7 And when a man shall sell his daughter to be a handmaid, she shall not go out according to the out-going of the men-servants,
Kama mwanaume ata muuza binti wake kama mtumishi wa kike, ata weza kwenda huru kama watumishi wa kiume wanavyo enda.
8 If she is uncomely in the eyes of her lord, who hath not assigned her in marriage, then shall he suffer her to be redeemed: to a strange people, shall he not have power to sell her in that he hath dealt treacherously with her.
Kama hamridhishi bwana wake, aliye mtenga kwa ajili yake, kisha lazima amnunue tena. Hana ruhusa ya kumuuza kwa watu wengine wa kigeni. Hana ruhusa hiyo, sababu amemtendea kwa hila.
9 And if, to his son, he assign her, according to the custom for daughters, shall he do for her.
Ikiwa bwana wake atamposa awe mke wa mwanae, atamtendea kama desturi zipasavyo sawa na binti zake.
10 If he take to himself another, her food her clothing, and her marriage-right, shall he not withdraw.
Ikiwa atajitwalia mke mwingine, asimpunguzie huyo chakula chake, nguo na haki zake za unyumba.
11 But if these three, he will not do for her, then shall she go out for nought, without silver.
Lakini asipofanyiwa mambo haya matatu, basi anaweza kwenda bure pasipo kutolewa mali.
12 He that smiteth a man, so that he die, shall surely be put to death.
Mtu awaye yote ampigaye mtu hata akafa, inampasa mtu huyo auawe pia.
13 But he who hath not lain in wait, but, God, hath occasioned him to come to his hand, then will I appoint for thee a place, whither he may flee.
Lakini kama hakumvizia, ila kwa bahati mbaya, basi nitamfanyia mahali pa kukimbilia.
14 But, when a man shall act presumptuously against his neighbour to slay him with guile, from mine altar, shalt thou take him to die.
Lakini mtu akimwendea mwenzake kwa kujikinai, kusudi apate kumwua kwa hila; huyo utamwondoa hata kama ni madhabahuni pangu, ili auawe.
15 And, he that smiteth his father or his mother, shall, surely be put to death.
Yeyote atakaye mpiga baba au mama yake lazima auawe.
16 And, he that stealeth a man of the sons of Israel, and selleth him, or he be found in his hand, shall, surely be put to death.
Yeyote atakaye mteka mtu na kumuuza, au mtu amekutwa kama mali yake, huyo mtekaji lazima auawe.
17 And he who revileth his father or his mother, shall, surely be put to death.
Yeyote atakaye mlaani baba au mama yake lazima auawe.
18 And when men strive together, and one shall smite the other, with a stone or with his fist, —and he die not, but shall fall to his bed; —
Kama wanaume watapigana na mmoja akimpiga mwengine kwa jiwe au ngumi, na huyo mtu asife, lakini alazwe kitandani;
19 if he rise and shall walk abroad on his staff, then shall he that smote him be acquitted, —only, for his loss of time, he shall pay, and, shall surely heal, him.
kisha akapona na anaweza kutembea kwa gongo lake, yeye aliye mpiga lazima alipe muda aliye mpotezea; na lazima alipe matibabu yake yote. Lakini huyo mtu hana hatia ya mauaji.
20 And when a man shall smite his servant or his handmaid with a rod, and he die under his hand, he shall, surely be avenged;
Kama mwanaume akimpiga mtumishi wake wa kiume au wa kike kwa gongo, na kama mtumishi huyo akifa kwa madhara ya pigo, kisha huyo mtu lazima ahadhibiwe.
21 nevertheless if, for a day or for two days, he continue, he shall not be avenged, for, his silver, he is.
Walakini, mtumishi huyo akiishi siku moja au mbili, bwana aruhusiwi kuadhibiwa, kwa kuwa atateseka kupoteza mtumishi huyo.
22 And when men strive together and push against a woman with child, and she miscarry, but there is no other mischief, he shall, surely be fined, according as the woman’s husband shall lay upon him, but he shall give it through judges.
Kama wanaume wakipigana pamoja na wakamuumiza wanamke mwenye mimba na kuiharibu, lakini hakuna majeraha mengine kwake, kisha huyo mwanaume mwenye hatia lazima alipe kama mme wa mwanamke anavyo taka kwake, na kulipa kama hakimu anavyo kusudia.
23 But, if mischief follow, then shalt thou give life for life;
Lakini kama kuna majeraha makubwa, lazima utoe uhai kwa uhai, jicho kwa jicho,
24 eye for eye, tooth for tooth, —hand for hand, foot for foot,
jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
25 brand for brand, wound for wound, —stripe for stripe.
kuchoma kwa kuchoma, jeraha kwa jeraha, au mkwaruzo kwa mkwaruzo.
26 And, when a man smiteth the eye of his servant, or the eye of his handmaid, and destroyeth it, he shall send him forth, free, for his eye;
Kama mwanaume akipiga jicho la mtumishi wake kiume au mtumishi wake wa kike na kuliharibu, kisha lazima amuache mtumishi aende pasipo fidia ya jicho.
27 or, if, the tooth of his servant or the tooth of his handmaid, he knock out, he shall send him forth, free, for his tooth.
Kama akitoa jino la mtumishi wake wa kiume au mtumishi wake wa kike, lazima amuache mtumishi kwenda huru kama fidia ya jino.
28 And when an ox goreth a man or a woman, and death ensueth, the ox shall, surely be stoned and his flesh shall not be eaten, and the owner of the ox, shall be quit.
Kama ng'ombe akimpiga mwanaume au mwanamke akafa, ng'ombe lazima apigwe mawe, na nyama yake hairuhusiwi kuliwa; lakini mmiliki wa ng'ombe lazima awe huru kwa hatia.
29 But, if, the ox, was wont to gore before that time and it hath been attested to his owner, and he hath not proceeded to put him under guard, and he causeth the death of man or woman, the ox, shall be stoned, and, his owner also, shall be put to death.
Lakini kama ng'ombe alikuwa na tabia ya kupiga hapo awali, na mmiliki wake alionywa lakini hakumzuia, na ng'ombe ameua mwanaume au mwanamke, huyo ng'ombe lazima apigwe mawe, na mmiliki wake lazima auawe pia.
30 If, a sin-covering, be laid on him, then shall he give a ransom for his life, according to whatsoever may be laid on him:
Kama malipo ya uhai yanaitajika, lazima alipe chochote anachotakiwa kulipa.
31 if, a son, he gore or, a daughter, he gore, according to this regulation, shall it be done to him;
Kama ng'ombe amempiga mwana wa mwanaume au binti wake, mmiliki wa ng'ombe anapaswa kufanya kama masharti yanavyo mlazimu.
32 if, a servant the ox gore, or a handmaid, thirty shekels of silver, shall he give to his lord, and, the ox, shall be stoned.
Kama ng'ombe akimpiga mtumishi wa kiume au wakike, mmiliki wa ngombe lazima alipe shekeli thelathini za fedha, na ng'ombe lazima apigwe mawe.
33 And when a man openeth a pit, or when a man diggeth a pit, and doth not cover it, —and there falleth thereinto an ox or an ass,
Kama mwanaume akifungua shimo, au kama mwanume akichimba shimo na asifunike, na ng'ombe au punda akaanguka ndani,
34 the owner of the pit, shall make it good, silver, shall he pay back to the owner thereof, —and the dead beast, shall be his.
mmiliki wa shimo lazima alipe madhara. Lazima atoe hela kwa mmiliki wa mnyama aliye kufa, na mnyama aliye kufa atakuwa wake.
35 And when the ox of one man thrusteth the ox of his neighbour so that it dieth, then shall they sell the live ox and divide the silver thereof, and the dead ox also, shall they divide,
Kama ng'ombe wa mwanaume akimuumiza ng'ombe wa mwanume mwengine hadi kufa, kisha lazima wamuuze ng'ombe aliye hai na kugawana gharama, na pia lazima wagawane ng'ombe aliye kufa.
36 Or if it was known that, an ox, was, wont to gore, before that time, and his owner proceeded not to put him under guard, he shall surely make good, —an ox for the ox, and, the dead one, shall be his.
Lakini kama ilijulikana kama ng'ombe alikuwa na tabia ya kupiga hapo awali, na mmiliki wake hakumfunga ndani, hakika lazima alipe ng'ombe kwa ng'ombe, na mnyama aliye kufa atakuwa wake.

< Exodus 21 >