< Exodus 12 >

1 Then spake Yahweh, unto Moses and unto Aaron, in the land of Egypt saying—
Bwana akamwambia Mose na Aroni katika nchi ya Misri,
2 This month, is, to you, a beginning of months, —the first, it is, to you, of the months of the year.
“Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu, yaani mwezi wa kwanza wa mwaka wenu.
3 Speak ye unto all the assembly of Israel, saying, On the tenth of this month, then let them take to them, each man a lamb for his ancestral household, a lamb for a household.
Iambie jumuiya yote ya Israeli kwamba katika siku ya kumi ya mwezi huu, kila mtu atatwaa mwana-kondoo mmoja kwa ajili ya familia yake, mmoja kwa kila nyumba.
4 But if the household be too small for a lamb, then shall he and his neighbour that is near unto his house take one, according to the number of souls, —each man according to his eating, shall ye number for the lamb.
Ikiwa nyumba yoyote ina watu wachache wasioweza kumaliza huyo mwana-kondoo mzima, nyumba hiyo itabidi ishirikiane na nyumba ya jirani wa karibu, baada ya kuzingatia idadi ya watu waliomo. Mtaangalia ni kiasi gani cha nyama kitahitajika kulingana na mahitaji ya kila mtu.
5 A lamb without defect a male a year old, shall yours be, —from the sheep or from the goats, shall ye take it.
Wanyama mtakaowachagua, lazima wawe wa kiume wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari, mwaweza kuwachukua kati ya kondoo au mbuzi.
6 So shall it be yours, to keep, until the fourteenth day of this month, —then shall all the convocation of the assembly of Israel slay it between the two evenings.
Tunzeni wanyama hao mpaka siku ya kumi na nne ya mwezi, ambapo lazima watu wa jumuiya yote ya Israeli wachinje wanyama hao wakati wa jioni.
7 And they shall take of the blood, and put upon the two door-posts and upon the upper-beam, —upon the houses wherein they are to eat it.
Ndipo watakapochukua baadhi ya hiyo damu na kuipaka kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango ya nyumba ambamo watakula wana-kondoo hao.
8 Then shall they eat the flesh, in the same night, —roast with fire, and with unleavened cakes, with bitter herbs, shall they eat it.
Usiku huo huo watakula nyama iliyookwa kwenye moto, pamoja na mboga chungu za majani na mikate isiyotiwa chachu.
9 Do not eat of it underdone, nor cooked by boiling in water, —but roast with fire, its head with its legs, and with its inward parts.
Msile nyama mbichi wala iliyochemshwa, lakini iwe imeokwa kwenye moto, kichwa, miguu na nyama zake za ndani.
10 And ye shall let nothing thereof remain until morning, —but that which is left remaining until morning, in the fire shall ye consume.
Msibakize nyama yoyote mpaka asubuhi; nazo kama zitabakia mpaka asubuhi, lazima mziteketeze kwa moto.
11 And, thus, shall ye eat it, —your loins, girded, your sandals, on your feet, and, your staff, in your hand, —so shall ye eat it in haste, it is Yahweh’s, passing over.
Hivi ndivyo mtakavyokula: Mtajifunga mikanda viunoni, mtakuwa mmevaa viatu vyenu miguuni na kushika fimbo zenu mkononi mwenu. Mle kwa haraka; hii ni Pasaka ya Bwana.
12 I will pass along, therefore, throughout the land of Egypt this night, and will smite every firstborn in the land of Egypt, from man even to beast, —and against all the gods of Egypt, will I execute judgments—I, Yahweh.
“Usiku huo huo nitapita katika nchi yote ya Misri na kumuua kila mzaliwa wa kwanza, wa wanadamu na wa wanyama, nami nitaihukumu miungu yote ya Misri. Mimi ndimi Bwana.
13 Then shall the blood serve you for a sign, on the houses wherein ye are, then will I behold the blood, and will pass over you, —and there shall be among you no plague to destroy, when I smite the land of Egypt.
Damu itakuwa ishara kwa ajili yenu ya kuonyesha nyumba ambazo mtakuwamo; nami nitakapoiona damu, nitapita juu yenu. Hakuna pigo la uharibifu litakalowagusa ninyi nitakapoipiga Misri.
14 So shall this day serve you for a memorial, and ye shall celebrate it, as a festival to Yahweh, —to your generations—as an age-abiding statute, shall ye celebrate it.
“Siku hii itakuwa kumbukumbu kwenu, mtaiadhimisha kuwa sikukuu kwa Bwana, katika vizazi vyenu vyote: mtaishika kuwa amri ya kudumu.
15 Seven days, unleavened cakes, shall ye eat, surely, on the first day, shall ye put away leaven, out of your houses, —for whosoever eateth what is leavened, then shall that soul be cut off out of Israel, from the first day, unto the seventh day.
Kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. Katika siku ya kwanza mtaondoa chachu yote ndani ya nyumba zenu, kwa maana yeyote atakayekula chochote chenye chachu kuanzia siku ya kwanza hadi ya saba lazima akatiliwe mbali kutoka Israeli.
16 Both on the first day, a holy convocation, and on the seventh day—a holy convocation, shall there be to you, —no work, shall be done therein, save only what must be eaten by every soul, that alone, shall be done by you.
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, na kusanyiko jingine katika siku ya saba. Katika siku hizo msifanye kazi kamwe isipokuwa kutayarisha chakula cha kila mmoja; hilo ndilo tu mtakalofanya.
17 So then ye shall observe the unleavened cakes, because on this self-same day, brought I forth your hosts out of the land of Egypt, —so then ye shall observe this day to your generations, as a statute age-abiding,
“Mtaadhimisha Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, kwa sababu hiyo ndiyo siku ile niliyovitoa vikosi vyenu kutoka Misri. Mtaiadhimisha siku hii kwa vizazi vyenu vyote kuwa amri ya kudumu.
18 In the first month, on the fourteenth day of the month in the evening, shall ye eat unleavened cakes, —until the one-and-twentieth day of the month in the evening,
Katika mwezi wa kwanza mtakula mikate isiyotiwa chachu, kuanzia jioni ya siku ya kumi na nne hadi jioni ya siku ya ishirini na moja.
19 For seven days, leaven, shall not be found in your houses, —for, whosoever eateth what is leavened, then shall that soul be cut off out of the assembly of Israel, whether sojourner or native of the land.
Kwa muda wa siku saba isionekane chachu yoyote katika nyumba zenu. Yeyote alaye chochote chenye chachu ndani yake, lazima akatiliwe mbali kutoka jumuiya ya Israeli, akiwa ni mgeni au mzawa.
20 Nothing leavened, shall ye eat, —in all your dwellings, shall ye eat unleavened cakes.
Msile chochote kilichotiwa chachu. Popote muishipo, ni lazima mle mikate isiyotiwa chachu.”
21 So then Moses called for all the elders of Israel, and said unto them, —Proceed and take for yourselves one of the flock according to your families, and slay the passover.
Ndipo Mose akawaita wazee wote wa Israeli na kuwaambia, “Nendeni mara moja mkachague wanyama kwa ajili ya jamaa zenu, mkachinje mwana-kondoo wa Pasaka.
22 Then shall ye take a bunch of hyssop, and dip it in the blood which is in the basin, and strike the upper beam and the two door-posts, with the blood which is in the basin, —and, ye, shall not go forth any man out of the entrance of his house, until morning,
Chukueni kitawi cha hisopo, kichovyeni kwenye damu iliyopo kwenye sinia na kuipaka baadhi ya hiyo damu kwenye vizingiti na kwenye miimo yote miwili ya milango. Mtu yeyote asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
23 And Yahweh will pass along to plague the Egyptians, and when he beholdeth the blood upon the upper beam and upon the two door-posts, then will Yahweh pass over the entrance, and not suffer the destroyer to enter into your houses to inflict on you the plague.
Bwana apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu juu ya vizingiti na kwenye miimo ya milango, naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zenu na kuwapiga ninyi.
24 And ye shall observe this thing, —for a statute to thee and to thy sons unto times age-abiding.
“Shikeni maagizo haya yawe kanuni ya kudumu kwenu na kwa ajili ya wazao wenu.
25 And so it shall come to pass when ye shall enter into the land which Yahweh will give you as he hath spoken, —and ye shall observe this service;
Mtakapoingia katika nchi Bwana atakayowapa kama alivyoahidi, shikeni desturi hii.
26 and it shall come to pass that your sons shall say unto you, —What is this your service?
Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’
27 Then shall ye say—A passover sacrifice, it is to Yahweh, who passed-over the houses of the sons of Israel, in Egypt, when he plagued the Egyptians but our houses, he delivered. Then did the people bend their heads and bow themselves down.
Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa Bwana, ambaye alipita juu ya nyumba za Waisraeli katika nchi ya Misri na hakudhuru nyumba zetu alipowapiga Wamisri.’” Ndipo watu wa Israeli waliposujudu na kuabudu.
28 And the sons of Israel went their way and did, —as Yahweh had commanded Moses and Aaron, so, did they.
Waisraeli wakafanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
29 And it came to pass, at midnight, that Yahweh, smote every firstborn in the land of Egypt, from the firstborn of Pharaoh who sat upon his throne, unto the firstborn of the captive who was in the pit of his prison, —and every firstborn of beasts.
Ilipofika usiku wa manane, Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika Misri, kuanzia mzaliwa wa kwanza wa Farao, mrithi wa kiti cha ufalme, hadi mzaliwa wa kwanza wa mfungwa, aliyekuwa gerezani, na wazaliwa wa kwanza wa mifugo yote pia.
30 Then rose up Pharaoh by night, he, and all his servants, and all the Egyptians, and there arose a great outcry throughout Egypt, —for there was not a house, where there was not one dead.
Farao, na maafisa wake wote, na Wamisri wote wakaamka usiku, na kulikuwa na kilio kikubwa katika nchi ya Misri, kwa kuwa haikuwepo nyumba ambayo hakufa mtu.
31 So he called for Moses and for Aaron by night and said—Rise ye, go forth out of the midst of my people, both ye and the sons of Israel, —and go serve Yahweh according to your word;
Wakati huo Farao akawaita Mose na Aroni na kuwaambia, “Ondokeni! Tokeni kwa watu wangu, ninyi pamoja na Waisraeli! Nendeni mkamwabudu Bwana kama mlivyoomba.
32 also, your flocks and your herds, take ye, as ye spake and go your way, —so shall ye bless, even me.
Chukueni makundi yenu ya kondoo na mbuzi pamoja na ngʼombe, kama mlivyosema, nanyi mwende zenu. Nanyi pia mnibariki.”
33 And the Egyptians became urgent with the people, to send them in haste out of the land, —for they said—We all, are dying.
Wamisri wakawahimiza Waisraeli waondoke kwa haraka na kuacha nchi yao. Kwa kuwa walisema, “La sivyo, tutakufa wote!”
34 So the people took up their dough, ere yet it was leavened, —with their kneading-bowls, bound up in their mantles on their shoulders,
Hivyo watu wakachukua donge lao la unga kabla ya kutiwa chachu, wakaweka ndani ya mabakuli ya kukandia, wakayaviringisha katika vitambaa na kuyabeba mabegani mwao.
35 And the sons of Israel, did according to the word of Moses, —and asked of the Egyptians, articles of silver and articles of gold and mantles.
Waisraeli wakafanya kama Mose alivyowaelekeza, nao wakawaomba Wamisri wawapatie vitu vya fedha, dhahabu na nguo.
36 And Yahweh, gave the people favour in the eyes of the Egyptians and they gave them gladly, —so they spoiled the Egyptians.
Basi Bwana alikuwa amewafanya Wamisri kuwa wakarimu kwa hawa watu, wakawapatia Waisraeli vile walivyotaka kwao; kwa hiyo wakawateka nyara Wamisri.
37 Then did the sons of Israel break up from Rameses, towards Succoth, —about six hundred thousand foot of men grown, besides little ones.
Waisraeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi. Walikuwepo wanaume wapatao 600,000 waendao kwa miguu bila kuhesabu wanawake na watoto.
38 Moreover also, a mixed multitude, came up with them, —flocks also, and herds, exceeding much cattle,
Watu wengine wengi wakafuatana nao, pamoja na makundi makubwa ya mifugo wakiwemo kondoo, mbuzi na ngʼombe.
39 Then baked they the dough which they had brought out of Egypt—into round unleavened cakes for it had not been leavened, —for they had been driven out of Egypt and could not tarry, and indeed no provisions, had they made ready for themselves.
Wakatengeneza maandazi yasiyotiwa chachu kwa ule unga uliokandwa waliokuwa wameutoa Misri, donge hilo la unga halikuwa limetiwa chachu, kwa kuwa walikuwa wameondolewa Misri kwa haraka nao hawakuwa na muda wa kuandaa chakula chao.
40 Now, the time during which the sons of Israel dwelt in Egypt, was four hundred and thirty years.
Waisraeli walikuwa wameishi Misri kwa muda wa miaka 430.
41 And it came to pass at the end of four hundred and thirty years, yea it came to pass, on this self-same day, that all the hosts of Yahweh had come forth out of the land of Egypt.
Ilikuwa ni siku ya mwisho ya hiyo miaka 430, vikosi vyote vya Bwana vilipokuwa vimeondoka Misri.
42 A night of solemn observances, it is unto Yahweh, for bringing them forth out of the land of Egypt, —this same night, pertaineth to Yahweh, for solemn observances by all the sons of Israel to their generations.
Kwa sababu Bwana aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri, katika usiku huu Waisraeli wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu Bwana katika vizazi vijavyo.
43 And Yahweh said unto Moses and Aaron: This, is the statute of the passover, —No stranger, shall eat thereof;
Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Haya ndiyo masharti kwa ajili ya Pasaka: “Mgeni hataruhusiwa kula Pasaka.
44 but, every man’s servant bought with silver, —when thou hast circumcised him, then, shall he eat thereof:
Mtumwa yeyote ambaye mmemnunua aweza kuila kama mmemtahiri,
45 An alien or a hireling, shall not eat thereof.
lakini kibarua yeyote au msafiri haruhusiwi kula.
46 In one house, shall it be eaten, thou shalt not take forth out of the house any of the flesh outside; and a, bone thereof, shalt thou not break.
“Sharti iliwe ndani ya nyumba; msichukue nyama yoyote nje ya nyumba hiyo. Msiuvunje mfupa wowote.
47 All the assembly of Israel, shall keep it.
Jumuiya yote ya Israeli ni lazima waiadhimishe Pasaka hiyo.
48 And when there may sojourn with thee a sojourner who may wish to keep a passover to Yahweh, there must be circumcised to him every male and then, may he draw near to keep it, so shall he be as a native of the land, —but no uncircumcised male, shall eat thereof.
“Mgeni aishiye miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana ni lazima wanaume wote waliomo nyumbani mwake wawe wametahiriwa, ndipo aweze kushiriki kama mzawa. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa haruhusiwi kuila.
49 One law, shall there be for the native, and for the sojourner that sojourneth in your midst.
Sheria iyo hiyo itamuhusu mzawa na mgeni anayeishi miongoni mwenu.”
50 Thus did all the sons of Israel, —as Yahweh had commanded Moses and Aaron, so, did they.
Waisraeli wote walifanya kama vile Bwana alivyomwagiza Mose na Aroni.
51 And it came to pass, on this self-same day, that Yahweh brought forth the sons of Israel out of the land of Egypt, by their hosts.
Siku ile ile Bwana akawatoa Waisraeli katika nchi ya Misri kwa vikosi vyao.

< Exodus 12 >