< Deuteronomy 8 >

1 All the commandment which I am commanding thee to-day, shalt thou, observe, to do, —that ye may, live, and multiply, and enter in and possess the land, which Yahweh sware unto your fathers.
Uwe mwangalifu kufuata kila agizo ninalokupa wewe leo, ili mweze kuishi, kuongezeka na mweze kuingia mkamiliki nchi ambayo Bwana aliahidi kwa kiapo kwa baba zenu.
2 So then, thou shalt remember all the way in which Yahweh thy God caused thee to journey these forty years in the desert, —that he might humble thee to put thee to the proof to know what was in thy heart, —whether thou wouldest keep his commandments or not.
Kumbuka jinsi Bwana Mungu wenu alivyowaongoza katika njia yote katika jangwa kwa miaka hii arobaini, kukunyenyekeza na kukujaribu ili ajue lililoko moyoni mwako, kwamba utayashika maagizo yake au la.
3 So he humbled thee, and suffered thee to hunger, and fed thee with manna which thou hadst not known, neither had thy fathers known, —that he might lead thee to consider that not on bread alone, shall the son of earth live, but on whatsoever cometh from the bidding of Yahweh, shall the son of earth live.
Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Bwana.
4 Thy mantle, hath not fallen with age from off thee, and, thy foot, hath not become swollen, —these forty years.
Nguo zenu hazikuchakaa wala miguu yenu haikuvimba kwa miaka hii arobaini.
5 Thou must consider, then with thy heart, —that as a man chasteneth his son, Yahweh thy God, hath been chastening thee.
Mjue basi ndani ya mioyo yenu kama mtu anavyomwadibisha mwanawe, ndivyo Bwana Mungu wako atawaadibisha ninyi.
6 Thou shalt therefore keep the commandments of Yahweh thy God, —to walk in his ways and to revere him.
Shikeni maagizo ya Bwana Mungu wenu mtembee katika njia zake na kumheshimu.
7 For, Yahweh thy God, is bringing thee into a good land; a land of ravines of water, of fountains and depths, coming forth in valley, and in mountain:
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi yenye vijito na mabwawa ya maji, yenye chemchemi zinazotiririka mabondeni na katika vilima;
8 a land of wheat and barley, and vine and fig-tree, and pomegranate, —a land of olive oil, and honey:
nchi yenye ngano na shayiri, mizabibu na mitini, mikomamanga, mafuta ya zeituni na asali;
9 a land wherein not in scarcity, shalt thou eat food, thou shalt lack nothing therein, —a land whose stones are iron, and out of whose hills thou mayest hew copper.
nchi ambayo chakula hakitapungua na hamtakosa chochote; nchi ambayo miamba yake ni chuma na mnaweza kuchimba shaba kutoka kwenye vilima.
10 So then thou shalt eat and be satisfied, —and bless Yahweh thy God, for the good land which he hath given unto thee.
Wakati mtakapokwisha kula na kushiba, msifuni Bwana Mungu wenu kwa ajili ya nchi nzuri aliyowapa.
11 Take heed to thyself, lest thou forget Yahweh thy God, —so as not to keep his commandments and his regulations and his statutes, which I am commanding thee to-day;
Jihadharini msimsahau Bwana Mungu wenu, mkashindwa kushika maagizo yake, sheria na amri zake ambazo ninawapa leo.
12 lest thou eat, and be satisfied, —and goodly houses, thou build and inhabit;
Angalia wakati mtakapokuwa mmekula na kushiba, mkajenga nyumba nzuri na kukaa humo,
13 and thy herd and thy flock, increase, and silver and gold, increase unto thee, —and all that thou hast, increase;
na wakati makundi yenu ya ngʼombe na mbuzi na kondoo yatakapoongezeka na fedha na dhahabu yenu itakapoongezeka na vyote mlivyo navyo vitakapozidishwa,
14 and so thy heart be lifted up, —and thou forget Yahweh thy God, who brought thee forth out of the land of Egypt out of the house of servants;
basi mioyo yenu isiwe na kiburi mkamsahau Bwana Mungu wenu aliyewatoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.
15 who caused thee to journey through the great and terrible desert, of fiery serpents and scorpions, and thirsty wastes where was no water, —who brought forth for thee water out of the flinty rock;
Aliwaongoza kupitia jangwa lile kubwa na la kutisha, nchi ile ya kiu isiyo na maji, yenye nyoka wa sumu na nge. Aliwatolea maji kutoka kwenye mwamba mgumu.
16 who fed thee with manna in the desert, which thy fathers had not known, —that he might humble thee, and that he might put thee to the proof, to do thee good in thy hereafter,
Aliwapa mana ya kula jangwani, kitu ambacho baba zenu hawakukijua, ili kuwanyenyekesha na kuwajaribu ninyi ili mwishoni apate kuwatendea mema.
17 and lest thou shouldest say in thy heart, —Mine own strength and the might of mine own hand, have gotten me this wealth.
Mnaweza kusema, “Uwezo wangu na nguvu za mikono yangu ndizo zilizonipatia utajiri huu.”
18 But thou shalt remember Yahweh thy God, that it was, he, who had been giving thee strength to get wealth, —that so he might establish his covenant which he sware to thy fathers (as at this day).
Lakini kumbukeni Bwana Mungu wenu, ndiye ambaye huwapa uwezo wa kupata utajiri, na hivyo kulithibitisha Agano lake, ambalo aliwaapia baba zenu, kama ilivyo leo.
19 But it shall be if thou forget, Yahweh thy God, and go after ether gods, and serve them, and bow thyself down to them, I testify against you to-day, that ye shall perish:
Ikiwa mtamsahau Bwana Mungu wenu, mkaifuata miungu mingine, mkaiabudu na kuisujudia, ninashuhudia dhidi yenu leo kwamba hakika mtaangamizwa.
20 like the nations which, Yahweh, is causing to perish from before you, so, shall ye perish, because ye would not hearken unto the voice of Yahweh your God.
Kama mataifa Bwana aliyoyaangamiza mbele yenu, ndivyo ninyi mtakavyoangamizwa kwa kutokumtii Bwana Mungu wenu.

< Deuteronomy 8 >