< Deuteronomy 23 >

1 Neither he that hath been mutilated by crushing, nor he that hath had his privy member cut off, shall enter into the convocation of Yahweh.
Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.
2 A bastard shall not enter into the convocation of Yahweh, —even to the tenth generation, shall none of his enter into the convocation of Yahweh.
Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
3 Neither an Ammonite nor a Moabite shall enter into the convocation of Yahweh, —even to the tenth generation, shall none that belong to them enter into the convocation of Yahweh, unto times age-abiding:
Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
4 because they met you not with bread and water, in the way, when ye came forth out of Egypt, —but hired against thee Balaam son of Beor from Pethor of Mesopotamia, to curse thee.
Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi.
5 Nevertheless, Yahweh thy God consented not to hearken unto Balaam, but Yahweh thy God turned, for thee, the curse into a blessing, —because Yahweh thy God loved thee.
Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda.
6 Thou shalt not seek their peace nor their welfare, —all thy days, unto times age-abiding.
Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.
7 Thou shalt not abhor an Edomite, for thy brother, he is, —thou shalt not abhor an Egyptian, for a sojourner, becamest thou in his land;
Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.
8 the sons who are born to them, of the third generation, may enter unto them in the convocation of Yahweh.
Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.
9 When thou goest forth into camp against thine enemies, then shalt thou beware of everything foul.
Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.
10 When there is in thy midst a man who is not clean through a mischance of the night, then shall he go forth unto the outside of the camp, he shall not come into the midst of the camp;
Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.
11 but it shall be, when the evening cometh on, he shall bathe himself in water, —and at the going in of the sun, he shall come into the midst of the camp.
Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.
12 And a place aside, shalt thou have, without the camp, —whither thou canst go forth abroad;
Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.
13 and a blade, shalt thou have upon thy staff, —so shall it be, that when thou wouldest sit down outside, thou shalt dig therewith, and shalt turn back and cover that which hath passed from thee:
Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.
14 for, Yahweh thy God, walketh to and fro in the midst of thy camp, to rescue thee, and to deliver up thine enemies before thee, so shall thy camps be holy, —and he shall see in thee no shameful thing, that he should turn away from following thee.
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.
15 Thou shalt not deliver up a slave unto his lord, —one who maketh his escape unto thee, from his lord:
Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.
16 with thee, shall he remain in thy midst, in the place which he shall choose in any of thy gates where it seemeth good to him, —thou shalt not oppress him.
Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.
17 There shall be no female devotee of the daughters of Israel, —neither shall there be, a male devotee, of the sons of Israel.
Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
18 Thou shalt not bring the wages of an unchaste woman, or the hire of a dog, into the house of Yahweh thy God for any vow, —for, an abomination unto Yahweh thy God, are they both.
Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.
19 Thou shalt not lend on interest to thy brother, interest of silver, interest of food, —interest of any thing that can be lent on interest:
Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.
20 to a foreigner, thou mayest lend on interest, but to thy brother, shalt thou not lend on interest, —that Yahweh thy God may bless thee, in everything where-unto thou puttest thy hand, upon the land which thou art entering to possess.
Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.
21 When thou shalt vow a vow unto Yahweh thy God, thou shalt not delay to make it good, —for Yahweh thy God would, require, it of thee, and it should be in thee sin.
Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.
22 But, if thou refrain from vowing, it shall not be in thee sin.
Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.
23 That which goeth forth out of thy lips, thou must observe and do, —according as thou didst vow unto Yahweh thy God the free-will, offering of which thou didst speak with thy mouth.
Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.
24 When thou enterest into the vineyard of thy neighbour, then mayest thou eat grapes at thy pleasure to thy fill, -but into thy vessel, shalt thou put none.
Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.
25 When thou enterest the standing corn of thy neighbour, thou mayest pluck off ears with thy hand, —but a sickle, shalt thou not wield against the standing corn of thy neighbour.
Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.

< Deuteronomy 23 >