< Deuteronomy 16 >
1 Observe the month of Abib, when thou shalt keep a passover unto Yahweh thy God, —for in the month of Abib, did Yahweh thy God bring thee forth out of Egypt by night:
Angalia mwezi wa Abibu, na uishike pasaka ya Yahwe Mungu wako, kwa kuwa katika mwezi wa Abibu Yahwe Mungu wako alikuleta toka Misri usiku.
2 therefore shalt thou sacrifice a passover unto Yahweh thy God of flock or herd, —in the place which Yahweh shall choose to make a habitation for his name there.
Utamtolea dhabibu ya pasaka Yahwe Mungu wako na baadhi ya mifugo na wanyama kwenye eneo ambalo Yahwe atachagua kama patakatifu pake.
3 Thou shalt not eat therewith any thing leavened, seven days, shalt thou eat therewith unleavened cakes the bread of humiliation, —for in haste, camest thou forth out of the land of Egypt, that thou mayest remember the day when thou camest forth out of the land of Egypt, all the days of thy life.
Hautakula mkate wa chachu pamoja nayo, siku saba utakula mkate usio na chachu, mkate wa mateso; kwa kuwa mlitoka katika nchi ya Misri kwa haraka. Fanya haya katika siku zako zote za maisha yako ili uweze kukumbuka akilini siku mliotoka nchi ya Misri.
4 And there shall not be seen with thee leaven in any of thy bounds seven days, —neither shall there remain all night of the flesh which thou shalt sacrifice in the evening, on the first day, unto the morning.
Hakuna chachu inapaswa kuonekana miongoni mwenu ndani ya mipaka yenu wakati wa siku saba; wala nyama yoyote mnayotoa dhabihu jioni kwa siku ya kwanza inabaki mpaka asubuhi.
5 Thou mayest not sacrifice the passover, —within any of thine own gates which Yahweh thy God is giving unto thee;
Msitoe dhabihu ya pasaka kati ya malango yenu ya ndani ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa.
6 but in the place which Yahweh thy God shall choose to make a habitation for his name, there, shalt thou sacrifice the passover in the evening, —at the going in of the sun, at the very time thou camest forth out of Egypt.
Badala yake, toa dhabihu katika eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kama patakatifu pake. Hapo mtatoa dhabihu ya pasaka jioni wakati jua linazama, kwa wakati huo wa mwaka mlitoka Misri.
7 Therefore shalt thou cook and eat it in the place which Yahweh thy God, shall choose, —and shalt turn away in the morning, and go thy way unto thy tents.
Mtapaswa kuichoma na kuila katika eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua; asubuhi mtageuka na kwenda kwenye mahema yenu.
8 Six days, shalt thou eat unleavened cakes, —and, on the seventh day, shall be a closing feast, unto Yahweh thy God, thou shalt do no work.
Kwa siku sita mtakula mkate usiotia chachu; katika siku ya saba kutakuwa na kusanyiko makini kwa ajili ya Yahwe Mungu wenu; katika siku hiyo hamtafanya kazi.
9 Seven weeks, shalt thou count unto thee, —from the beginning of thrusting in the sickle into the standing corn, shalt thou begin to count, seven weeks.
Mtahesabu wiki saba kwa ajili yenu; tangu wakati mlipoanza kuweka mundu kwenye nafaka iliyosimama mtapaswa kuanza kuhesabu wiki saba.
10 So shalt thou keep the festival of weeks unto Yahweh thy God, in the measure of the freewill offering of thy hand which thou shalt give, —as Yahweh thy God shall bless thee.
Mtapaswa kushika wiki za sherehe ya Yahwe Mungu wenu pamoja na mchango wa sadaka ya utayari kutoka mkono wako ambayo utatoa, kulingana na Yahwe alivyokubariki.
11 So shalt thou rejoice before Yahweh thy God—thou, and thy son and thy daughter and thy servant and thy handmaid, and the Levite who is within thy gates, and the sojourner, and the fatherless and the widow who are in thy midst, —in the place which Yahweh thy God shall choose, to make a habitation for his name there.
Utafurahi mbele ya Yahwe Mungu wako- wewe, kijana wako, binti wako, mjakazi wako wa kiume, mjakazi wako wa kike, Mlawi aliye katika malango yako, na mgeni, yatima, na mjane alio miongoni mwenu, katika eneo ambalo Yahwe Mungu wako atachagua kwa ajili ya patakatifu pake.
12 So shalt thou remember that a servant, thou wast in Egypt, —and shalt observe and do these statutes.
Utakumbuka akilini kwamba ulikuwa mtumwa Misri; unapaswa kuangalia na kuzishika amri hizi.
13 The festival of booths, shalt thou keep for thyself seven days, —when thou hast gathered in out of thy threshing-floor and out of thy wine-vat.
Unapaswa kushika sherehe za vibanda kwa siku saba baada ya kuwa mmekusanya mavuno toka kwenye sakafu ya mapura na kutoka kwenye kinu chako cha divai.
14 And thou shalt rejoice in thy festival, —thou, and thy son and thy daughter, and thy servant and thy handmaid, and the Levite and the sojourner, and the fatherless and the widow, who are within thy gates.
Utafurahi wakati wa sherehe- wewe, kijana wako, binti wako, mjakazi wako wa kiume, mjakazi wako wa kike, Mlawi, na mgeni, na yatima na mjane walio ndani ya malango yako.
15 Seven days, shalt thou keep festival unto Yahweh thy God, in the place which Yahweh shall choose, —for Yahweh thy God, will bless thee, in all thine increase and in all the work of thy hands, —therefore shalt thou do nothing but, rejoice.
Kwa siku saba unapaswa kuangalia sherehe ya Yahwe Mungu wako katika eneo ambalo Yahwe atachagua, kwa sababu Yahwe Mungu wako atakubariki katika mavuno yako yote na kazi ya mikono yako yote, na unapaswa kuwa na furaha kabisa.
16 Three times in the year, shall each one of thy males see the face of Yahweh thy God, in the place which he shall choose, at the festival of unleavened cakes and at the festival of weeks and at the festival of booths, —and none shall see the face of Yahweh empty-handed:
Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote wanapaswa kuonekana mbele za Yahwe Mungu wako katika eneo ambalo atachagua: katika sherehe ya mkate usiotiwa chachu, katika sherehe za wiki, na sherehe ya vibanda; na hawataonekana mbele za Yahwe mikono mitupu;
17 every man according as his hand can give, —according to the blessing of Yahweh thy God, which he hath bestowed upon thee.
badala yake, kila mtu atatoa kama awezavyo, kwamba mtajua baraka kwamba Yahwe Mungu wako amekupa.
18 Judges and officers, shalt thou appoint thee in all thy gates, which Yahweh thy God is giving unto thee, by thy tribes, —and they shall judge the people, with righteous judgment,
Unapaswa kufanya waamuzi na maakida ndani ya malango yako ambayo Yahwe Mungu wako anakupa; watachukuliwa toka kila kabila, and watahukumu watu kwa hukumu ya haki.
19 Thou shalt not wrest judgment, thou shalt not take note of faces, —nor shalt thou accept a bribe, for the bribe, blindeth the eyes of wise men, and perverteth the words of righteous men.
Haupaswi kuiondoa haki kwa nguvu; haupaswi kuonesha upendeleo wala kuchukua rushwa, kwa kuwa rushwa upofusha macho ya hekima na kupotosha maneno ya haki.
20 What is right, what is right, shalt thou pursue, —that thou mayest live and possess the land, which, Yahweh thy God, is giving unto thee.
Unapaswa kufata baada ya haki, baada ya haki peke yake, ili kwamba uishi na kurithi nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupa.
21 Thou shalt not plant thee, as a sacred stem, any tree, —near unto the altar of Yahweh thy God which thou shalt make for thyself;
Haupaswi kujitengenezea Asherahi, aina yoyote ya mti, kando ya madhabahu ya Yahwe Mungu wako ambayo utakayojitengenezea.
22 neither shalt thou set thee up a pillar, —which Yahweh thy God, doth hate.
Wala usijitengenezee jiwe takatifu la nguzo, ambalo Yahwe Mungu wako anachukia.