< Deuteronomy 15 >

1 At the end of seven years, shalt thou make a release.
Kila mwisho wa miaka saba ni lazima mfute madeni.
2 And, this, shall be the manner of the release, Every creditor who lendeth aught to his neighbour, his hand shall release it, —he shall not exact it of his neighbour or his brother, because there hath been proclaimed a release unto Yahweh.
Hivi ndivyo itakavyofanyika: Kila mkopeshaji atafuta mkopo aliomkopesha Mwisraeli mwenzake. Hatamtaka Mwisraeli mwenzake au ndugu yake amlipe hilo deni, kwa sababu wakati wa Bwana wa kufuta madeni umetangazwa.
3 Of a foreigner, thou mayest exact it, —but, what thou hast with thy brother, thy hand shall release;
Unaweza kudai malipo kwa mgeni, lakini lazima ufute kila deni ambalo unamdai ndugu yako.
4 save, when there shall be among you no needy person, —for Yahweh will indeed bless, thee, in the land which Yahweh thy God is giving unto thee as an inheritance to possess it:
Hata hivyo, hapatakuwepo maskini miongoni mwenu, kwa kuwa katika nchi Bwana Mungu wenu anayowapa kuimiliki kama urithi wenu, atawabariki sana,
5 only if thou do hearken unto the voice of Yahweh thy God, —to observe to do—all this commandment which I am commanding thee to-day.
ikiwa tutamtii Bwana Mungu wenu kikamilifu na kuwa waangalifu kuyafuata maagizo haya yote ninayowapa leo.
6 When, Yahweh thy God, hath blessed thee, as he spake unto thee, then shalt thou lend unto many nations but thou, shalt not borrow, and, thou shalt rule over many nations but over thee, shall they not rule.
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu atawabariki kama alivyoahidi, nanyi mtawakopesha mataifa mengi lakini hamtakopa kwa yeyote. Mtatawala mataifa mengi lakini hakuna taifa litakalowatawala ninyi.
7 When there cometh to be among you a needy person any one of thy brethren within any one of thy gates, in thy land, which Yahweh thy God is giving unto thee, thou shalt not harden thy heart nor shut thy hand from thy needy brother;
Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa hiyo nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie mkono ndugu yako aliye maskini.
8 but thou shalt, open, thy hand unto him, —and, lend, him enough to meet the poverty which doth impoverish him.
Afadhali fungua mikono yako na umkopeshe kwa hiari chochote anachohitaji.
9 Take thou heed to thyself lest there be something near thine abandoned heart, saying—Drawing nigh, is the seventh year the year of release, and so thine eye be evil, against thy needy brother, and thou give not unto him, —and he cry out against thee unto Yahweh, and it become in thee a sin!
Jihadhari usijiwekee wazo hili ovu: “Mwaka wa saba, mwaka wa kufuta madeni umekaribia,” usije ukaonyesha nia mbaya kwa ndugu yako mhitaji na ukaacha kumpa chochote. Anaweza kumlalamikia Bwana dhidi yako nawe utakuwa umepatikana na hatia ya dhambi.
10 Thou shalt, give, unto him, and thy heart shall not be evil when thou givest unto him, —for on account of this very thing, will Yahweh thy God bless thee, in all that thou doest and in all whereunto thou puttest thy hand.
Mpe kwa ukarimu na ufanye hivyo bila kinyongo moyoni, ndipo kwa sababu ya hili Bwana Mungu wenu atakubariki katika kazi zako zote na kwa kila kitu utakachokiwekea mkono wako.
11 For the needy will not cease out of the midst of the land—for this cause, am I commanding thee, saying, Thou shalt open, thy hand unto thy brother to thy poor and to thy needy, in thy land.
Siku zote watakuwepo watu maskini katika nchi. Kwa hiyo ninawaamuru mwe na mikono iliyokunjuliwa kuwaelekea ndugu zenu, kuwaelekea maskini na wahitaji katika nchi yenu.
12 When thy brother a Hebrew man (or a Hebrew woman) selleth himself unto thee, then shall he serve thee six years, —and in the seventh year, shalt thou let him go out free from thee;
Kama Mwebrania mwenzako, mwanaume au mwanamke, akijiuza kwako na kukutumikia miaka sita, katika mwaka wa saba ni lazima umwache aende zake akiwa huru.
13 and when thou lettest him go out free, from thee, thou shalt not let him go out empty:
Nawe wakati utakapomwachia usimwache aende mikono mitupu.
14 thou shalt, richly load, him out of thy flock, and out of thy threshing-floor and out of thy wine-vat, —of that wherewith Yahweh thy God hath blessed thee, shalt thou give unto him;
Mpe kwa uhuru kutoka zizi lako la kondoo na mbuzi, kutoka sakafu yako ya kupuria nafaka na kutoka mashinikizo yako ya kukamulia divai. Mpe kama vile ambavyo Bwana Mungu wako alivyokubariki.
15 and thou shalt remember that a servant, thou wast in the land of Egypt, and that Yahweh thy God, redeemed thee, —for this cause, am I commanding thee this thing, to-day.
Kumbukeni kuwa ninyi mlikuwa watumwa huko Misri naye Bwana Mungu wenu aliwakomboa. Ndiyo sababu nimewapa agizo hili leo.
16 And it shall be, if he shall say unto thee, I will not go away from thee, —because he loveth thee, and thy household, because he is well off with thee,
Lakini mtumishi wako akikuambia, “Sitaki kukuacha,” kwa sababu anakupenda wewe na jamaa yako naye anaridhika nawe,
17 then shalt thou take an awl and thrust it through his ear unto the door, so shall he be thy servant all his life. And unto thine handmaid also, shalt thou do thus.
ndipo utachukua chuma kidogo utoboe sikio lake mpaka hicho chuma kiingie kwenye ubao wa mlango, naye atakuwa mtumishi wako wa maisha. Ufanye vivyo hivyo kwa mtumishi wa kike.
18 It shall not be hard in thine eyes when thou lettest him go out free, from thee; for to the double of the hire of a hireling, hath he served thee six years, —so will Yahweh thy God bless thee, in all that thou doest.
Usifikiri kuwa kuna ugumu kumwacha mtumishi wako huru, kwa sababu utumishi wake kwako kwa miaka hii sita umekuwa wa thamani mara mbili ya ujira wa mtumishi wa kuajiriwa. Naye Bwana Mungu wenu atakubarikia kwa kila kitu utakachofanya.
19 Every firstling that is brought forth in thy herd and in thy flock that is a male, shalt thou hallow unto Yahweh thy God, —thou shalt not work with a firstling of thine oxen, neither shalt thou shear a firstling of thy flock:
Wekeni wakfu kwa Bwana Mungu wenu kila mzaliwa wa kwanza wa kiume wa makundi yenu ya ngʼombe na ya mbuzi na kondoo. Maksai walio wazaliwa wa kwanza msiwafanyize kazi, wala msinyoe manyoya ya wazaliwa wa kwanza wa kondoo.
20 before Yahweh thy God, shalt thou eat it year by year, in the place which Yahweh shall choose, —thou, and thy household.
Kila mwaka ninyi na jamaa zenu mtapaswa kuwala mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua.
21 But, when there is in it any blemish, lameness or blindness, any ill blemish, thou shalt not sacrifice it unto Yahweh thy God:
Kama mnyama ana dosari, akiwa ni kilema au kipofu au kama ana kilema kibaya, kamwe usimtoe dhabihu kwa Bwana Mungu wenu.
22 within thine own gates, mayest thou eat it, —the unclean of you and the clean alike, as the gazelle and as the hart.
Itawapasa kumla ninyi wenyewe katika miji yenu. Wote wasio safi na walio safi kwa desturi za kiibada mwaweza kula kama vile mnavyokula paa au kulungu.
23 Only the blood thereof, shalt thou not eat, —on the earth, shalt thou pour it out like water.
Lakini kamwe msinywe damu; imwageni ardhini kama maji.

< Deuteronomy 15 >